WATU watano wamefariki dunia baada ya malori mawili yaliyokuwa yamebeba mafuta na betri kulipuka baada ya kugongana huko eneo la Vigwaza Kibaoni mkoni Pwani.
Ajali hiyo mbaya iliyosabaabisha mafgari matatu kuwaka moto na kutekekteza watu hao ilitokea jana katika barabara ya Morogoro, majira ya saa 8 usiku.
Katika eneo la tukio ilidaiwa lori la mafuta lililigonga kwa nyuma gari jingine lililokuwa limeegeshwa pembeni ya barabara kwa ajili ya matengenezo na kusababisha moto mkubwa kuwaka hapo.
Kamanda wa polisi mkoani Pwani, Absaloom Mwakyoma alisema ajali hiyo ilihusisha malori mawili aina ya Scania, moja ambalo lilikuwa na trela na ambalo lilibeba mafuta liligonga kwa nyuma lori ambalo lilikuwa limesheheni mzigo wa betri za redio mali ya Said Daniel, mfanyabishara wa Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Alisema wakati moto huo unalipuka chini ya lori alikuwepo utingo wa gari ambalo lilikuwa katika matengenezo Omary Mumbi, mkazi wa Buguruni, alikuwepo dereva wa gari hilo Adam Amulike[ 35], mkazi wa Temeke na dereva mwingine aliyefika kusaidia kutengeneza gari hilo na wote hao waliteketea kwa moto huo
Pia katika ajali hiyo ulimuunguza dereva na utingo wa lori lililosababisha ajali, ambao majina yao hayakuweza kupatikana wote waliteketea kabisa wakiwa ndani ya gari lao.
Alisema wakati moto huo unaendelea kuwaka magari yalisimama na kutoendela na safari lakini lori jingine aina ya Scania lililokuwa na trela lenye tanki ambalo halikuwa na mafuta lilifanya ubinshi kujaribu kupita eneo hilo na baadae kushindwa kuendela na safari baada ya moto kushika kwenye gari hilo na matairi matano ya upande wa kulia kuungua.