WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Friday, April 16, 2010

MTU MWENYA BAHATI MBAYA KULIKO WOTE NCHINI UINGEREZA


Mkulima wa nchini Uingereza Mick Wilary ambaye anadaiwa kuwa ndiye mtu mwenye bahati mbaya kuliko wote nchini Uingereza kutokana na ajali kibao zinazomkumba, amepata ajali kwa mara nyingine tena iliyoivunja miguu yake yote miwili.
Mick Wilary, mwenye umri wa miaka 58 anadaiwa kuwa ndiye mtu ambaye hana tabasamu kutokana na bahati mbaya zinazomkumba na kumfanya akumbwe na ajali mbaya zinazoyatia maisha yake hatarini.

Mick ameishakumbwa na ajali mbaya zaidi ya 30 na ajali hizo zimepelekea kuvunjika kwa mifupa ya viungo vyake 15.

Katika tukio la hivi karibuni, Mick anaendelea kupatiwa matibabu hospitalini baada ya miguu yake kupondwa na tingatinga.

Katika tukio hilo dereva wa tingatinga akiliendesha tingatinga hilo modeli ya JCB bila ya kuwa mwangalifu, alimgonga Mick na kumbamiza ukutani.

Katika tukio hilo mguu wa kushoto wa Mick ulivunjika na kupinda kuelekea mabegani wakati mguu wake wa kulia ulijeruhiwa na kugeuka ukiangalia nyuma.

Hata hivyo pamoja na ajali hiyo mbaya ya kutisha, madaktari katika hospitali ya Newcastle wamefanikiwa kuiokoa miguu yake na wamesema kuwa ndani ya miezi sita Mick ataweza tena kuitumia miguu yake kutembea.

Ajali ya kuvunjika kwa miguu yake imetokea ikiwa ni miezi michache baada ya kuvunjika kwa enka za miguu yake yote miwili baada ya kuteleza na kuanguka chini alipokanyaga kiazi mviringo.

Miongoni mwa ajali mbaya zilizowahi kumkumba Mick ni kupasuka kwa fuvu la kichwa chake kwenye sakafu alipopigwa mweleka na paka.

Mick pia ameishawahi kuvunjika mbavu, shingo na mikono katika mfululizo wa ajali mbaya zinazoendelea kumkumba ambazo zimeifanya sura yake ikose tabasamu wakati wote.

No comments:

Post a Comment