
Hii ni moja kati ya kauli alizozitoa Rais Kikwete wakati wa hotuba yake aliyoitoa juzi jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na wazee kjatika ukumbi wa Diamond Jubilee.
Rais alitoa kauli hiyo baada ya kuonekana kukerwa na viongozi wa Tucta wanaoandaa mgomo nchi nzima.
“ Mgomo huo una lengo la kuongezewa mshahara tu au kuna lingine? Alihoji rais, mimi naona mnataka kuninyima kura zenu, basi kama mmepanga hivyo mninyime tu, wengine watanipa” alisema Rais
“Mana sitaki kuwaongopea kuwa tutalipa kima hicho kama mnataka kugoma na mshahara huo kama hatutawapa basi, ninyimeni kura zenu wengine watanipigia” alisema
Pia aliwasihi wafanyakazi hao atakayegoma atakuwa amejifukuzisha kazi na kukosa haki yake ya msingi katika miaka yake aliyoitumika serikali.
Pia alisema kwa yeyote atakayefika kazini na akae na asiendelee na kazi pia atakuwa amejifukuzisha mwenyewe na hakutakuwa na msamaha na atakayethubutu kuandamana sheria itafata mkondo wake.
No comments:
Post a Comment