
Kusema ukweli waafrika Mungu katujalia akili nyingi sana lakini hali zetu duni za kiuchumi ndizo siku zote zinazoturudisha nyuma siku zote.
Angalia video ya mwanafunzi huyu wa nchini Togo ambaye kwa kutumia vifaa toka kwenye televisheni mbovu ameweza kutengeneza robot kama yale ambayo makampuni ya nchini Japan yamekuwa yakifanya utafiti kuyaboresha.
Sam Todo ambaye ni mwanafunzi wa nchini Togo alitumia vifaa toka kwenye televisheni mbovu na vifaa vingine vya umeme kuweza kutengeneza robot ambalo linaweza kutembea na kupunga mikono kwa kutumia remote control.
Bila shaka kijana kama huyu kama angeweza kupata vifaa vya kisasa au angepata mfadhili wa kukuza kipaji chake angeweza kufanya mambo makubwa kuliko haya.
Angalia video yake chini.
VIDEO - Waafrika Tupo Fiti Sana Basi tu..
No comments:
Post a Comment