WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, April 19, 2010

UREMBO WASABABISHA KIFO SIKU YA KUZALIWA KWAKE


Mwanamke wa nchini Uingereza aliyesherehekea kutimiza umri wa miaka 34 kwa kutoboa ulimi wake kuweka kichuma amefariki siku mbili baadae kutokana na sumu iliyotokana na kichuma hicho.
Amanda Taylor alipuuza kauli za familia yake kumpinga kuweka kichuma cha inchi moja kwenye ulimi wake na aliamua kuutoboa ulimi wake kuweka kichuma hicho ili kusherehekea kutimiza umri wa miaka 34.

"Kwa muda mrefu alifikiria kuutoboa ulimi wake kuweka kichuma", alisema mama yake Lorraine Taylor mwenye umri wa miaka 61.

"Siku nne kabla ya siku yake ya kuzaliwa aliniambia kuwa anataka kuweka kichuma kwenye ulimi wake siku ya kuzaliwa kwake", aliendelea kusema mama yake.

"Nilimpinga na kumuonya asifanye hivyo lakini alisema kuwa marafiki zake wote wameishaweka vichuma kwenye ndimi zao".

Kwa shingo upande mama yake alimpa ruhusa Amanda kutoboa ulimi wake lakini siku mbili baadae Amanda alikutwa nyumbani kwake akiwa amefariki.

Uchunguzi wa awali ulionyesha kuwa alifariki kutokana na damu yake kuingia sumu iliyotokana na kichuma alichowekewa kwenye ulimi wake.

Uchunguzi zaidi kuhusiana na kifo chake unaendelea.

No comments:

Post a Comment