WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, April 12, 2010

POMBE YA KIENYEJI YAUA WATU 7 NA WENGINE 10 WAISHIA KUPOFUKA


Mmoja wa watu waliopoteza macho yao baada ya kunywa Chang'aa akiwa amelazwa hospitali.

Pombe ya kienyeji maarufu nchini Kenya kama Chang'aa imesababisha vifo vya zaidi ya watu 7 na kupofuka macho kwa watu wengine 10.
Zaidi ya watu saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 10 wamebaki vipofu baada ya kunywa pombe maarufu nchini Kenya kwa jina la Chang'aa.

Wakazi wengi wa kitongoji cha Shauri Moyo jijini Nairobi nchini Kenya walikimbizwa hospitali wakiwa hawajiwezi baada ya kunywa Chang'aa (Gongo).

Katika tukio hilo lililotokea jana ijumaa, watu watatu walifariki kwenye eneo la tukio wakati watu watano walipofuka macho hapohapo ya kubwia kilevi hicho cha kienyeji ambacho ni kinyume cha sheria kukutwa nacho.

Mkuu wa kituo cha polisi cha Buruburu alisema kuwa watu wengi zaidi waliwahishwa kwenye hospitali ya Kenyatta baada ya kunywa pombe hiyo.

Baada ya kunywa pombe hiyo, watu walianza kutoa mapovu mdomoni huku wakilalamika maumivu makali ya tumbo.

Hadi kufikia leo watu waliopoteza macho yao wamefikia 10 huku jumla ya watu 7 tayari wameishapoteza maisha yao.

No comments:

Post a Comment