WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Friday, March 26, 2010

APOTEZA MAISHA KWA MOTO KISA KUKATALIWA


Mwanaume mmoja wa nchini Uingereza ambaye alitoswa na mkewe wa ndoa ya miaka 14 ambaye alipata mwanaume mwingine nje, amefariki dunia kutokana na moto aliouanzisha ili kuichoma moto nyumba yake ili mkewe asiambulie kitu watakapoachana. Wakati Timothy Flood alipoimiminia petroli nyumba yake ili ndoa yake na mkewe itakapovunjika, mkewe asiambulie kitu, hakungundua kuwa kuna kiasi kidogo cha petroli kilimwagikia kwenye nguo zake.

Na wakati alipoipiga kiberiti nyumba yake alishangaa kujikuta na yeye mwenyewe akiwaka moto.

Timothy ambaye ni baba wa watoto watatu alijaribu kuuzima moto uliokuwa ukimteketeza kwa kutumia maji ya mvua lakini hadi wakati anaokolewa alikuwa ameishangua asilimia 90 ya mwili wake na alifariki dunia siku mbili baadae hospitalini.

Timothy mwenye umri wa miaka 42, aliamua kuichoma moto nyumba yake baada ya mkewe kuamua kuivunja ndoa yao alipoanza uhusiano na mwanaume aliyesoma naye shule.

Ingawa Timothy na mkewe, Catherine, 39, walikuwa wakiendelea kuishi kwenye nyumba moja walikuwa hawazungumzi wala kujuliana hali.

Mgogoro mkubwa ulikuwa kwenye nyumba yao ambapo Catherine alimtaka Timothy aondoke amuachie yeye nyumba hiyo.

Timothy kwa kuhofia kuwa watakapoachana rasmi kisheria kutokana na sheria mkewe anaweza akapewa nyumba kwa sababu ya watoto wao,
aliamua kuichoma moto ili wakose wote.

Mahakama katika mji wa Newport, kusini mwa Wales iliambiwa kuwa Timothy ili kuichoma moto nyumba hiyo alinunua lita 51 za petroli na viberiti kadhaa ili kuhakikisha kuwa hakitoki kitu.

Siku ya tukio, alimpeleka mkewe kwa wazazi wake na ndipo aliporudi na kuipiga moto nyumba hiyo baada ya kumtumia meseji mkewe akimwambia "Nimeishapata suluhisho la kuishi bila wewe".

Moto mkubwa ulizuka ambao uliiteketeza sehemu kubwa ya nyumba hiyo.

Majirani wanasema kuwa Timothy alisikika akipiga kelele za kuomba msaada wakati moto aliouanzisha akitegemea kuiteketeza nyumba yake ulipokuwa ukimchoma yeye mwenyewe.

Timothy alifariki siku mbili baadae hospitalini baada ya ndugu zake kukubali kuzizima mashine zilizokuwa zikimsaidia aendelee kuishi.

DR,SLAA AMFURISHA KIKWETE

BAADA ya Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa kuibana serikali kuhusu vipengele vilivyoongezwa kinyemela katika muswada uliosaniwa na Rais Jakaya Kikwete kwa mbwembwe wiki iliyopita, taarifa mpya zinasema Rais amefura, akitaka maelezo ya kina ya walioingiza vipengele hivyo.

Tanzania Daima lilipozungumza na mmoja wa wasaidizi wa Rais Kikwete kuhusu sakata hilo jana, alidokeza kwa maneno machache, na kwa msisitizo, akisema: “Rais amefura.”

Msaidizi huyo wa rais alisema kutokana na kasoro hiyo ya kwanza ya aina yake kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii, Rais Kikwete ametaka maelezo ya kina ili kubaini waliohusika kuchomeka vipengele hivyo.

Naye Dk Slaa, ambeye ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amezidi kuibana serikali akiitaka irejeshe bungeni Muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi ili kifungu kilichochomekwa kinyemela kiondolewe.

Alisema hilo ni hitaji la lazima la kisheria; na kwamba serikali isipofanya hivyo katika mkutano ujao wa 19 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, itachukuliwa hatua za kisheria. Alitaka waliohusika wawajibishwe.

Dk. Slaa, mmoja wa wabunge wanaosoma sana na wenye upeo mkubwa bungeni, ndiye aliyeibua sakata la kasoro hiyo wiki hii.

Jana alisema: “Naomba serikali ichukue hatua kuwasilisha Miscellaneous Amendment katika mkutano wa 19, yaani Bunge la Aprili, ili kifungu hiki ambacho ni kinyume na demokrasia kiondolewe kwenye Sheria ambayo rais ameisaini, vinginevyo tutachukua hatua za kisheria.

“Kama ilivyoripotiwa na gazeti la Tanzania Daima, Mhe. Spika jana wakati anajibu kwenye taarifa ya saa mbili usiku ya TBC1 ni dhahiri alionyesha kuwa hajasoma na hakuwa ameelewa vizuri kinacholalamikiwa.

“(Kama) Angekuwa amesoma, Spika angekuwa mwangalifu kutamka aliyoyatamka. Mheshimiwa Spika anakiri kulikuwa na mjadala, lakini hakutamka mjadala ulihusu nini na wala hakumnukuu Mwenyekiti wa siku hiyo ambayo alikuwa Mhe. Naibu Spika alitoa maagizo gani.

“Ni hatari kwa viongozi wetu kutoa matamko kwa mambo mazito bila kufanya utafiti angalau mdogo. Mhe. Spika atakubali kuwa kwenye Hansard, hakuna popote ambapo imejadiliwa achilia mbali kukubaliwa kuwa ‘Timu ya Kampeni itathibitishwa na Msajili (kwa
mgombea urais) au Katibu Tawala (kwa mgombea ubunge) au na Mtendaji wa Kata kwa (mgombea udiwani).’ Hii ni dhana mpya kabisa, siyo tu haijajadiliwa wala haikufikiriwa kama Hansard inavyoonyesha.”

Dk. Slaa alitoa kauli hii ya jana wakati akijibu kauli ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye juzi alizungumza kupitia kituo cha Televisheni cha TBCI, akitetea udhaifu huo wa kuchomeka kipengele hicho kiholela.

Dk. Slaa alifafanua kuwa kilichojadiliwa ambacho yeye alishiriki ni hoja aliyoleta Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge kutaka kufanyia mabadiliko pendekezo la serikali kwa kifungu cha 7(2).

Alisema katika kifungu hicho, Chenge alitaka makundi ya sanaa yaingizwe baada ya neno voters.

“Hivyo ni vyema naye Spika akiri tu kuwa utaratibu wa kutunga sheria umekiukwa. Haifai kubishana kwa sababu ya kubishana wakati Hansard ndiyo ushahidi wa wazi wa jambo hilo.

“Mimi ndiye namwomba Mwanasheria Mkuu, rafiki na ndugu yangu, aisome vizuri kwa kuwa yeye ndiye hajasoma. Amesema vizuri kututaja ambao tulikuwa na mjadala ukumbini, sasa anionyeshe mahali popote katika mjadala huo ni wapi approving authority ilijadiliwa, na kuwa hiyo approving authority iwe Msajili, DAS na WEO.

“Hivyo, ni ustaarabu tu kukiri kuwa kifungu hiki kimechomekwa na kuwa akubali,” alisema Dk. Slaa.

Hata hivyo, tayari Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema juzi aliliambia gazeti hili kwamba iwapo itabainika kuwa kauli ya Dk. Slaa ni ya kweli, serikali itaomba radhi na kupeleka muswada bungeni kwa ajili ya masahihisho hayo.

Dk. Slaa alidai Rais Kikwete amepotoshwa katika baadhi ya vipengele, kikiwamo kipengele kinachohusu uthitibishwaji wa wajumbe wanaounda timu za kampeni kwa ajili ya wagombea urais, wabunge na udiwani.

Alisema Bunge halikukubaliana kuhusu kipengele hicho, wala hakimo katika kumbukumbu za Bunge; na kwamba kiliongezwa baadaye, kabla ya Rais Kikwete kusaini muswada huo kuwa sheria.

Kifungu kinachodaiwa kuchomekwa ni cha 7 (3), ambacho hakikuwepo kabisa kwenye muswada uliojadiliwa na kupitishwa bungeni.

Kwa mujibu wa sheria hiyo, kifungu kidogo cha pili, kinaeleza maana ya timu ya kampeni kuwa ni kundi la watu lililoundwa na mgombea wakati wa zoezi la uteuzi lenye madhumuni ya kumwakilisha au kumsaidia mgombea kwenye kampeni za uchaguzi ambaye amepitishwa kuwania.

“(a) Kwa kesi ya urais watathibitishwa na Msajili, (b) Kwa kesi ya Mbunge watathibishwa na Katibu Tawala wa Wilaya na (c) Kwa kesi ya Diwani watathibitishwa na Katibu Tarafa...,” ilieleza sehemu ya sheria hiyo iliyosainiwa na Rais Kikwete ambayo nakala yake tunayo.

Muswada huo wa sheria ulioasisiwa na Rais Kikwete mwenyewe, ulipitishwa kwa mbinde Februari 12 mjini Dodoma huku ukiibua malumbano makubwa baina ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Werema, na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, pamoja na wabunge wengine kuhusu vipengele mbalimbali vya muswada huo.

MREMA AFUNGUA KESI MAHAKAMANI,ADAI BIL 1/-

HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema amefungua kesi ya madai ya sh bilioni moja dhidi ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Kesi hiyo ya madai namba 32/10 imefunguliwa na mwenyekiti huyo anayeongoza chama chenye wafuasi wasiozidi 500,000 nchini kote kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya chama hicho Magomeni, Dar es Salaam jana, Mrema alieleza dhamira yake ni kutaka kupata uthibitisho kutoka kwa spika huyo wa Bunge kama amefilisika na kwa sasa anahongwa na makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kadhalika, Mrema anadai kwamba kitendo cha Sitta kuieleza jamii kupitia gazeti kwamba amechanganyikiwa na amepewa fedha kwa ajili ya kuipigia debe CCM kina lengo la kumdhoofisha katika kampeni zake za kuwania ubunge wa Vunjo kwa tiketi ya TLP.

“Katika barua niliyopeleka kwa Spika nilitaka aniombe radhi kwa uzito ule ule katika kipindi cha siku saba na kunilipa fidia, lakini akawa kimya kwa muda wote huo,” alisema Mrema na kuongeza kwamba washitakiwa wengine katika kesi hiyo ambayo haijapangiwa jaji ni gazeti lililochapisha habari hiyo na mhariri wake akiamini kuwa ndiyo chombo kilichotumika kumchafua na kumpotezea hadhi aliyojijengea.

“Hivi kweli mimi nimechanganyikiwa? Kwanini anivunjie hadhi yangu?… Nimekuwa Naibu Waziri Mkuu wa nchi hii, nimefanya mengi sana nilipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, kwa miaka 30 nimeitumikia Tanzania,” alisema Mrema.

NYUKI WENYE HASIRA WAUA MIFUGO NA KUJERUHI WATU 40


Nyuki wenye hasira walikitesa kijiji kizima nchini Niger kwa masaa kadhaa na kuua mifugo kadhaa pamoja na kuwafanya watu zaidi ya 40 wakimbizwe hospitali wakiwa majeruhi. Kundi la nyuki waliokuwa na hasira baada ya mzinga wao kwenye mti kung'olewa, walikitesa kijiji kimoja kusini mwa nchi ya Niger kwa kuwashambulia watu na mifugo kwa masaa kadhaa.

Watu zaidi ya 40 wakiwemo watoto 14 waliwahishwa hospitali baada ya kushambuliwa na nyuki wakati mzinga wa nyuki uliokuwa kwenye mti mkubwa kwa zaidi ya miaka 50 ulipodondoshwa chini kutokana na upepo mkali.

Punda mmoja na farasi mmoja walifariki dunia huku ng'ombe na mbuzi 95 wakiachwa wakiwa wamepooza miili yao baada ya kudungwa sindano za nyuki hao wenye hasira.

Kwa mujibu wa radio Anfani ya nchini Niger, nyuki walikivamia kijiji cha Dake-Garka katika mji wa Birni-N'Konni baada ya tawi la mti lililokuwa na mzinga wao, lilipoangushwa chini na upepo mkali.

Iliripotiwa kuwa masaa kadhaa baada ya uvamizi wa nyuki hao, wanakijiji walikuwa bado wanahofia kurudi kwenye majumba yao kwa kuhofia mashambulizi ya nyuki.

CALIFORNIA NEW LAW WONT HURT ECONOMY

SAN FRANCISCO

California's economy will not be damaged by the state's 2006 climate change law, a state agency said in a report yesterday that counters the business community's arguments that the economically troubled state will lose more jobs and businesses.

The analysis by the state Air Resources Board, the chief regulator of the law, forecast higher energy prices from new regulations and a cap-and-trade system for greenhouse gases, but said greater energy efficiency would keep costs manageable in the trend-setting environmental state.

It concluded that the measure will yield modest job gains statewide, will have a negligible effect on the state's overall economy -- the eighth largest in the world -- and could benefit some sectors like alternative energy businesses.

In sharp contrast to a 2008 report that was panned as shallow and full of faulty assumptions, the Wednesday analysis was received with cautious approval from academics at Stanford and other universities who consulted on the process.

Business groups however said the state was still making rosy assumptions.

In 2006, California's Legislature passed and Republican Governor Arnold Schwarzenegger signed a law committing the state to developing regulations to reduce greenhouse gas emissions -- blamed for global climate change -- to 1990 levels by 2020.

"These policies can shift the driver of economic growth from polluting energy sources to clean energy and efficient technologies, with little or no economic penalty," the report said.

Thousands of manufacturing, mining and utilities industry jobs will be lost, but service, finance, and other sectors will gain similar numbers, leaving the most populous US state about the same in terms of total jobs, income and growth, the report said. Five scenarios found a maximum effect of tens of billions of dollars on state output of $2.5 trillion in 2020.

Much will depend on what happens outside California, including whether California is at the leading edge of a move away from fossil fuels.

"It might hasten the arrival of regional, national or other international policies, and I think that is what California is betting on," said Stanford economist Larry Goulder, one of the academics on the panel advising state researchers.

California aims to reduce greenhouse gas emissions through a variety of steps such as tighter standards on car fuel efficiency, standards on energy efficiency in buildings, and a "cap and trade" market for pollution credits.

Under cap-and-trade, carbon dioxide and other greenhouse gas emissions would be capped. Companies would need permits for the pollution they send into the atmosphere and those permits could be traded on a regulated market.

Three US senators -- Democrat John Kerry, Republican Senator Lindsey Graham and independent Senator Joseph Lieberman -- are working to resuscitate climate change legislation in the US Senate after the House of Representatives passed its version of the measure last year.

A parallel study by consultancy Charles River Associates, which worked at the request of the Air Resources Board, put the cost of the climate law at a few hundred dollars per person in 2020 and said success would depend on the state giving itself room to respond to issues, such as high gasoline prices.

"It is clear that flexibility matters," said Charles River consultant Paul Bernstein.

Many businesses still fear tens or hundreds of thousands of jobs could be lost, spurred by higher energy prices from the law, known locally as AB32.

"Their conclusion is that AB32, the most far-reaching regulation in history, won't impact jobs in California," Shelly Sullivan, spokeswoman for the AB 32 Implementation Group, which includes several chambers of commerce, said skeptically.

Goulder and the other economists called the new report "valuable information" and said it addressed key concerns by creating a better scenario if the law did not take effect and scenarios if parts of the law did not work as planned.

Mary Nichols, chair of the Air Resources Board, told reporters that the new analysis was better than 2008.

"We made all the changes and found that the results were pretty much the same as they had been the first time around, which is very modest, almost undetectable overall effect on gross state product by 2020 but some modest improvement in areas of job growth and personal income," she said.

AJALI MBAYA DAR, HIACE YAKANDAMIZWA NA LORI




ZAIDI ya watu nane wamepoteza maisha papohapo kwa ajali mbaya iliyotokea huko maeneo ya Kibamba Darajani nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Ajali hiyo ilitokea jana, majira ya saa 11 alfajiri ambapo ilihusisha gari aina ya lori lililokuwa na namba za usajili T 189 na basi dogo la abiria aina Toyota Hiace lililokuwa na namba za usajili T 616 AJW.


Ajali hiyo imetokea baada ya lori hilo lililokuwa likitoka Dar es Salaam kuelekea Pwani kupoteza mwelekeo na kuingia kulia zaidi na kuivaa basi hilo uso kwa uso lililokuwa na abiria na kulilalia na kupoteza maisha ya watu hao.

Hiace hiyo ilikuwa inatoka Lugoba mkoani Pwani ilikuwa inaelekea Dar es Salaam na ndipo ilipovamiwa na lori hilo na abiria wote waliokuwemo humo kufariki dunia papohapo na kati yao kulikuwa na mamda mjamzito.


Hata hivyo ilidaiwa kuwa lori hilo lilikuwa imeshindwa kuhimili breki na kudaiwa halikuwa na breki na ndicho chanzo kikuu cha ajali hiyo mbaya.

Hata hivyo mara baada ya kutokea kwa ajali hiyo dereva wa lori na utingo wake wlikimbia na kuacha lori hilo papohapo na hawakujulikana mara moja walikimbilia wapi kwa muda huo.

Katika hali ya kushangaza wananchi bado hawajifunzi na baadhi ya maelfu waliokimbilia katika ajali hiyo kuonekana kuzoa mafuta ya taa yaliyomwagika barabarani na kusahau kuwa siku za karibuni watu walipoteza maisha kutokana na matukio kama hayo walikuw wnazoa mafuta na ghafla lori kulipuka na kupoteza maisha na wengine walipata vilema vya maisha kutokana na

MAHABUSU WAJIPAKA KINYESI MAHAKAMANI DAR.

MAHABUSU watano jana walitoa kioja cha mwaka katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni walijipaka kinyesi kwa kugoma kurudi mahabusu. Washitakiwa hao wanaokabiliwa na kesi ya wizi wa kutumia silaha wote kwa pamoja walichukua uamuzi huo baada ya kugoma kurudi mahabusu kwa kutaka wafutiwe mashitaka yao ambayo yamedumu wka muda mrefu.


Hivyo washitakiwa hao walipotakiwa na askari magereza kutoka mahabusu na kuelekea mahakamani walichukua vinyesi na kujipaka mwilini.


Hali ilikuwa tata walipofika mahakamani hapo hali iliyoradhimu hakimu kushindwa kuendelea kusikiliza shauri hilo kwa siku hiyo.


Mahabusu hao walionekana kugoma kupanda basi maalum linalowarudisha rumande kwa madai ya kutaka kufutiwa shauri hilo hali iliyofanya wapakiwe kwenye gari dogo na kupelekwa kituo cha polisi Magomeni.

EASTER SPECIAL AT MENAI BAY BEACH BUNGALOWS!!!


SUNSET VIEW AT MENAI BAY BEACH BUNGALOWS!!! IT'S LOVELY

YOU WILL GET A CHANCE TO RELAX AND ENJOY ON THE LOCALLY BEDS.

SINGLE ROOM AT MENAI FRESH WEATHER AND CLEAN!!!



DOUBLE ROOM

MENAI BUNGALOWS FROM OUTSIDE
NAI BAY BEACH BUNGALOWS

Menai Bay Beach Bungalows (Unguja Ukuu) Consisting of five beach bungalows set in a shady palm grove direct on the beach.

THE BEACH BUNGALOWS.
The hotel Menai consists of ten rooms in bungalows, built of local materials. The rooms are equipped with double or king size beds, mosquito nets, 4 rooms with fans & 6rooms with fan and Air Conditions.
The private verandah overlooks the lush tropical gardens and the Indian Ocean beyond. All rooms have their own bathroom with toilet, washing basin, shower and hair dryers.

THE BEACH RESTAURANT (NEW MASAI RESTAURANT)
Is situated direct on the beach under a huge baobab tree. Our specialty is all kind of fresh caught seafood, prepared in international or traditional local style.
Enjoy romantic sunsets over the bay while sipping a glass of wine.

We are proud of our lush tropical garden.
1000 years old Baobab trees, Mango and Almond trees, Bougainvilleas and Barbados Pride illuminate the hotel ground.

EASTER SPECIAL OFFER FOR TANZANIAN AND EST AFRICANS.
ROOMS WITH FANS
SINGLE ROOM ON BB Tshs. 25,000 per night
DOUBLE ROOM ON BB Tshs. 30,000 per night
TRIPLE ROOM ON BB Tshs. 50,000 per night
ROOMS WITH AC
SINGLE ROOM ON BB Tshs. 30,000 per night
DOULBE ROOM ON BB Tshs. 35,000 per night
TRIPLE ROOM ON BB Tshs. 55,000 per night
HB SUPPLEMENT
ADULT ON HB Tshs. 15,000 per person
CHILD ON HB Tshs. 10,000 per child
FB SUPPLEMENT
ADULT ON FB Tshs. 20,000 per person
CHILD ON FB Tshs. 15,000 per child
Includes 1 soda, a glass of juice or bottle of water
during the meal.
TWO NIGHTS STAY – you get free tour to Jozani Forest where you can see Red Colobus Monkeys and etc.

BEACH PARTY ON 3RD APRIL 2010
ENTRANCE FEE: TSHS 5,000 FOR MEN (includes 1 drink)
LADIES FREE.

Enjoy with us UNFORGETTABLE HOLIDAY in an untouched nature far off the beaten track.
Contact: +255 0 777 422008 / 0 715 422009 / 0 769 662662