WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Friday, June 18, 2010

Hakuna mgombea binafsi- Mahakama


MAHAKAMA YA RUFAA ya Tanzania jana ilitengeua na kuondoa suala la mgombea binafsi na haitatumika katika uchaguzi tarajio kwa kuwa suala hilo limeonekana kuwa ni la kisiasa zaidi na si la kisheria.
Uamuzi huo uliotolewa jana na jopo la majaji saba na kusomwa na Jaji Mkuu, Agustino Ramadhani, na kusema mgombea binafsi hataruhusiwa katika uchaguzi ujao wa Oktoba mwaka huu.

Akisoma hukumu hiyo, katika ukumbi wa mahakama kuu, Jaji Ramadhani alisema baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili zilizowasilishwa mahakamani, mahakama imegundua kuwa suala la mgombea binafsi ni la kisiasa, hivyo mahakama haina mamlaka ya kulitolea uamuzi.

Alisema uamuzi wa kuwa na mgombea binafsi ni suala la kisiasa linapaswa kuzingatia historia na matakwa ya nchi husika, hivyo mahakama imependekeza suala hilo lirudishwe bungeni ili lijadiliwe kwa kina zaidi na kutolewa uamuzi huko kwa kuwa bunge ndicho chombo kitachokuwa na mamlaka ya kufanya mabadiriko ya katiba za nchi

“Kwa mujibu wa ibara ya 98 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bunge ndilo lenye jukumu la kufanya marekebisho ya vipengele vya katiba au sheria yeyote”

Mara baada ya hukumu hiyo kutolewa mahakamani hapo mmoja wa wadai wa ugombea binafsi, Mchungaji Chisptopher Mtikila alipohojiwa na vyombo vya habari kuhusiana na hukumu hiyo alisema, hakustushwa sana na maamuzi ya jopo hilo la majaji kwa kuwa tayari alikwishaanza kuona dalili ya mahakama kumpendelea Rais Jakaya Kikwete ili arudi madarakani.

Alisema ka kuwa hakuridhika na maamuzi hayo, anakusudia kuwasilisha rufaa mbele ya Mahakama ya Rufaa ya Afrika Mashariki ili litolewe uamuzi ambao anaamini utakuwa wa haki.

Kwa upande wa baadhi ya wananchi waliohudhuria hukumu hiyo wanasheria na wanaharakati mbalimbali walionekana dhahiri kusikitishwa na maamuzi hayo na kusema kuwa mahakama hiyo haijali maslahi ya wananchi na wanyonge wan chi hii.

Walisema maamuzi hayo wamepokea kwa masikitiko makubwa za kusitisha mgombea binafsi na kusema kuwa mahakama imeshindwa kushughulikia mambo ya msingi yalnayohitaji majibu kutoka kwenye chombo hicho na wameona maamuzi hayo ni kama kutowatendea haki wananchi.

Ili Kupinga Obama Kuwa Rais, Alichoma Moto Kanisa la Watu Weusi


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani anakabiliwa na kifungo cha miezi 108 jela baada ya kukiri kulichoma moto kanisa la watu weusi ili kupinga Barack Obama kuwa rais mweusi wa Marekani.
Benjamin Haskell, 23, wa Massachusetts nchini Marekani amekiri kosa lake la kulichoma moto kanisa la Wamarekani weusi ili kupinga kuchaguliwa kwa Barack Obama kuwa rais wa kwanza mweusi wa Marekani.

Benjamin alikiri jana kulichoma moto kanisa la Macedonia Church of God in Christ mnamo novemba 5 mwaka 2008, ikiwa ni ndani ya masaa machache baada ya Obama kuchaguliwa kuwa rais.

Benjamin alilimwagia petroli kanisa hilo kabla ya kulipiga kiberiti na kuliteketeza.

"Leo tunatoa ujumbe kuwa watu wanaofanya uhalifu kwa sababu za chuki, watachunguzwa na baadae ya kushtakiwa", alisema Carmen Ortiz mwanasheria mkuu wa Massachusetts.

Benjamin huenda akahukumiwa kwenda jela miezi 108 (miaka 9) baada ya kukiri kosa lake la kuhatarisha maisha ya waumini 300 wa kanisa hilo na kuliharibu jengo la kidini kwasababu ya chuki zake ubaguzi wa rangi.

Mke Amuua Mume Kwasababu ya Kombe la Dunia


Kombe la dunia linaloendelea nchini Afrika Kusini limekuwa sababu ya kifo cha mwanaume mmoja nchini humo ambaye alifariki baada ya kupigwa na mkewe na watoto wake wakati alipolazimisha kuangalia mechi kwenye TV wakati mkewe na watoto wake walitaka kuangalia nyimbo za dini.
David Makoeya mwenye umri wa miaka 61 hakutaka kuikosa mechi ya jumapili iliyopita kati ya Ujerumani na Australia.

Mke wake na watoto wake wao walitaka kuangalia programu ya nyimbo za dini za kikristo kwenye luninga.

Polisi wanasema kuwa Makoeya alikuwa akigombania remote control na familia yake ili aweze kuangalia mechi ya kombe la dunia.

Familia yake walikataa kubadilisha channel ya mambo ya dini waliyokuwa wakiiangalia na hapo ndipo mzozo ulipoanzia.

"Alisema, Hapana nataka kuangalia mpira", msemaji wa polisi Mothemane Malefo alisema.

Huku akiwa na hasira, Makoeya alinyanyuka na kuelekea kwenye TV ili aweze kubadilisha channel lakini hakufika mbali kwani mkewe na watoto wake walianza kumshushia kipigo.

Mke wa Makoeya mwenye umri wa miaka 68, Francina, akishirikiana na mtoto wake wa kiume Collin mwenye umri wa miaka 36 na binti yake Lebogang mwenye umri wa miaka 23 walimshushia kipigo cha nguvu baba yao.

"Inaonekana walikipigiza kichwa chake kwenye ukuta, walipiga simu polisi baada ya kumjeruhi vibaya sana... wakati polisi wanafika eneo la tukio, Makoeya alikuwa ameishafariki", alisema Malefo.

Mke wa Makoeya na wanae ambao wanaishi kwenye kijiji cha Makweya, walitiwa mbaroni jumapili usiku.

Binti yake aliachiwa kwa dhamana ya dola 200 wakati mkewe na mtoto wake wa kiume wanaendelea kunyea debe rumande.

Ndugu wa familia hiyo wamesikitishwa na kifo cha Makoeya wakisema kuwa Makoeya hakuwa mtu mwenye vurugu alikuwa mtulivu na mwenye furaha kwa familia yake.

VIDEO - Wivu Wapelekea Amchome Moto Mpenzi Wake


Kutokana na wivu mwanamke mmoja nchini Marekani alimchoma moto mpenzi wake na kisha kujichoma moto na yeye mwenyewe na kutokana na moto huo nyumba ilishika moto na kupelekea vifo vya watu wengine watatu.
Agnes Bermudez, 50, anatuhumiwa kumuua mpenzi wake William Salazar, 32, katika tukio la kutisha lililotokea siku ya akina baba duniani mwaka 2008.

Agnes ambaye hivi sasa kesi yake inaendelea mahakamani, alimchoma moto mpenzi wake huyo na kisha yeye mwenyewe alijipiga kibiriti.

Agnes hakufariki kutokana na moto aliouanzisha lakini aliungua vibaya sura yake kiasi cha kumfanya asitambulike.

Sababu ya Agnes kumchoma moto mpenzi wake ni wivu wa kimapenzi. Agnes alimshutumu Salazar kuwa anatembea na mwanamke mwingine nje.

Video ya tukio hilo imetolewa mahakamani kama ushahidi wa tukio hilo la kusikitisha.

Video inamuonyesha Agnes na Salazar wakitoka nje ya nyumba yao wakikimbilia kwenye duka lililopo chini ya jengo lao.

Salazar anaonekana akikimbia kuingia ndani ya duka akitafuta maji wakati Agnes alilala chini mbele ya duka hilo huku akiungua na moto.

Wasamaria wema walifanikiwa kuwamwagia maji na kuokoa maisha yao hata hivyo Salazar alifariki siku nne baadae hospitalini.

Moto ulioanzishwa na Agnes ulishika pia nyumba zingine zilizopo kwenye jengo hilo na kupelekea vifo vya watu watatu.

Chini ni VIDEO ya tukio hilo iliyoonyeshwa mahakamani.