WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Wednesday, April 28, 2010

OBAMA NA AGA KHAN WAGUSWA NA MUUNGANO TANZANIA



RAIS Barack Obama wa Marekani na Aga Khan Kiongozi wa wa Ismailia duniani wamemtumia Rais Jakaya Kikwete salamu za pongezi kwa kwa kusherehekea sikukuu ya Muungano iliyoadhimishwa jana nchini kote.

Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu jana ikinukuu taarifa ya ubalozi wa Marekani hapa nchini ilielezea kuwa salamu hizo kutoka kwa viongozi hao zilitumwa jana.

“Mpendwa Rais, kwa niaba ya watu wa Marekani, nakutumia salamu zangu za dhati kukupongeza wewe na watu wa Tanzania, wakati mnaposherehekea Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26, April,” ilieleza sehemu hiyo ya taarifa iliyopitia Ubalozi wa Marekani hapa nchini.

“Ni matumaini yangu kwamba miaka ijayo italetea Watu wa Tanzania Amani na mafanikio ya kudumu,” Rais Obama alimueleza Rais Kikwete katika salamu hizo na kuelezea nia yake na matarajio ya baadaye kuwa nchi hizo zitaimarisha mahusiano baina yao.

“Natarajia tutaimarisha na kuwa na mahusiano thabiti baina ya nchi zetu,” salamu za Rais Obama ilieleza.

Naye Kiongozi wa wa Ismailia duniani alimueleza Rais Kikwete furaha yake na kutoa salamu za heri kwa Rais Kikwete na Watanzania wote.

“Wa-Ismailia Imamat na Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan, kwa pamoja tunaahidi kufanya kazi kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania na Jumuiya za Kiraia katika kuchangia katika ukuaji wa nchi na nafasi kwa watu wote wa Taifa,” alieleza na kumshukuru Rais Kikwete kwa ushirikiano wake.

“Tunathamini ushirikiano wako na wa Serikali yako katika kuunga mkono na kutia moyo shughuli za Jumuiya ya Aga Khan,” Salamu za Aga Khan zilielezea.

Jana maelfu ya watu walioenda kushuhudia sherehe za maadhimisho ya Miaka 46 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar walionyesha hisia zao wakati marais wastaafu, Ali Hassani Mwinyi na Benjamini Mkapa walipoingia.

Umati huo ulilipuka shangwe za kelele na vifijo wakati viongozi hao walipoingia kwenye uwanja huo mkongwe kwa nyakati tofauti kabla ya Rais Jakaya Kikwete kuingia na kuzunguka uwanja mzima akipunga mkono.

Mkapa, ambaye aliongoza serikali ya awamu ya tatu ambayo ilijipatia sifa ya kuinua uchumi na kuboresha miundombinu, ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia uwanjani katika siku hiyo iliyokuwa na jua la vipindi.

Baada ya Mkapa, ambaye aliongoza nchi kwa sera aliyoiita ya "ukweli na uwazi", kuingia uwanjani hapo kwa gari la kifahari aina ya Range Rover (Vogue), kelela za shangwe na vigelegele zililipuka kutoka kwenye umati wa watu.

Mkapa aliyeingia uwanjani hapo majira ya saa 3:15 alipishana kwa takriban dakika 15 na kiongozi wa serikali ya awamu ya pili, Mwinyi ambaye pia aliamsha kelele za shangwe kutoka kwa watu waliohudhuria.

Kama ilivyokuwa kwa Mkapa, Mwinyi ambaye aliingia uwanjani hapo na gari aina ya Toyota Landcruiser (VX) alishangiliwa kwa nguvu tofauti na ilivyokuwa kwa viongozi wa serikali ya sasa, akiwemo Rais Kikwete.

WAALIMU WAWILI WAUAWA KWA RISASI TARANGIRE

WALIMU wawili wa Shule ya Msingi ya Tarangire mkoani Manyara, Joyce Paulo, 30, na Anna Nkya, 24, wameuawa kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori kutoka Hifadhi ya Taifa ya Tarangire kutokana na kilekilichoelezwa kuwa niugomvi wa mapenzi.

Imeelezwa kuwa askari aliyefanya mauaji hayo alikuwa lindoni kwenye hifadhi hiyo, lakini akaamua kuacha kazi yake na kwenda hadi nje ya hifadhi kutekeleza mauaji hayo ya mtu anayesadikiwa kuwa ni mkewe na mgoni wake.

Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi saa 3:00 usiku eneo la Tarangire lililo kwenye Kata ya Ngaiti baada askari huyo, ambaye ametajwa kuwa ni Paulo Keregesi kuvamia nyumba waliokuwa wanaishi walimu hao na kuwamiminia risasi zilizokatisha maisha yao.

Diwani wa Kata ya Ngaiti inayopakana na hifadhi hiyo, Olais Ole Koine alisema kabla ya mauaji hayo, Keregesi alikuwa ametengana na mkewe Joyce, ambaye mwalimu na ambaye amezaa naye watoto wawili.

Diwani huyo alisema taarifa ambazo wamepata mara baada ya mauaji hayo zinaeleza kuwa askari huyo na mkewe Joyce ambao wote ni wenyeji wa mkoani Mara walikuwa na ugomvi kwa takriban miezi miwili iliyopita.

Alisema, hata hivyo, walikwenda nyumbani kwao kusuluhishwa lakini waliporudi mwanamke huyo hakurejea kwa mumewe anayeishi ndani ya hifadhi hiyo na akaamua kuishi na mwalimu mwenzake nje ya hifadhi hiyo.

"Baada ya hali hiyo ndio juzi majira ya saa 3:00 usiku askari huyo aliyekuwa lindoni na silaha alivamia nyumba ya walimu na kwa kupitia dirishani aliwapiga risasi na wakafariki papo hapo na baadaye akatoweka," alisema Diwani Koine.

Alisema wamepata taarifa kuwa askari huyo aliyekuwa na bunduki aina ya AK 47 aliiterekeza eneo la Mdori na kukimbia na baadaye alituma ujumbe mfupi wa simu kueleza kuwa anahusika na mauaji hayo na kwamba ameiacha pikipiki mjini Babati.

"Muda huu tunajiandaa kuja Arusha ili kupanga taratibu za kusafirisha marehemu kwani Mwalimu Nkya ni mwenyeji wa Machame na Joyce ni mwenyeji wa Serengeti," alisema Diwani Koine.

Polisi mkoani Manyara wamethibitisha kupokea taarifa za tukio hilo na wanamsaka askari huyo. Mkuu wa hifadhi ya Tarangire, Erastus Lufungulo, ambaye kwa sasa yupo likizo, pia amethibitisha kupata taarifa za mauaji hayo.
"Naomba uwasiliane na mkurugenzi mkuu wa Tanapa kama kuna maelezo mnahitaji kuhusu huyo askari," alisema Lufungulo.

Hata hivyo, meneja uhusiano wa Tanapa, Pascal Shelutete alisema jana kuwa bado hawajapata taarifa kamili za tukio hilo na aliomba kupewa muda zaidi ili atoe maelezo zaidi.

ZAIDI YA WAFUNGWA 3000 WAACHIWA HURU

RAIS Jakaya Kikwete, ametoa msamaha kwa wafungwa zaidi ya 3,101 waliuokuwa wanatumikia vifungo kwenye magereza mbalimbali nchini.

Rais alitoa msamaha huo jana wakati wa maadhimisho ya miaka 46 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika viwanja vya Uhuru jijini Dar es Salaam.

Wafungwa walionufaika na msahama huo ni waliokuwa wanatumikia vifungo visivyozidi miaka mitano jela, wengine ni wafungwa wenye magonjwa kama ya Ukimwi, kifua kikuu na saratani ambao wanaelekea kuwa katika siku za mwisho za maisha yao, baada ya kuthibitishwa na jopo la wataalamu wea afya ngazi ya wilaya na mkoa.

Wengine ni wazee wenye umri wa miaka 70 na zaidi, wakiwemo wajawazito, wanawake wenye watoto wanaonyonya, walemavu wa mwili na akili pia.

Msamaha huo hautawahusu wafungwa wanaotokana na makundi ya waliohukumiwa kunyongwa, wenye makosa ya kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya, kupokea na kutoa rushwa, unyang'anyi wa kutumia silaha, ubakaji, kunajisi, kulawiti na wizi wa magari kwa kutumia silaha.

Wengine ambao hawatanufaika na msamaha huo ni wale waliowapa mimba wanafunzi wa shule za msingi na kusababisha washindwe kuendelea na

NVUA KUBWA YALETA BALAA DAR


JANA jiji la Dar es salaam lilitawaliwa na shida na mapungungufu makubwa katika huduma mbalimbali kutokana na mvua kubwa iliyonyesha siku nzima hali iliyofanya wakazi wa jiji kuteseka kutokana na hali hiyo.
Mbali na kuwa na dmapungufu katika huduma nyingine tofautitofauti shida kubwa zaidi ilikuwa ni upande wa usafiri ambao ulikuwa haupatikani kutokana na mvua hiyo.


NIFAHAMISHE ilishuhudia makundi ya watu yakihaha huku na huku, na yakipita barabarani mithili ya maandamano yakitembea kwa miguuu kurudi majumbani mwao kwa kukoseskana kwea huduma hiyo.


Hali hiyo ilidumu siku nzima katika kila kituo cha mabasi jijini ambapo mabasi yalikuwa hayafiki mjini na wakazi hao kulazimika kurudi kwa miguu majumbani mwao.


Jopo la waandishsi wa nifahamishe nao dhahama hiyo iliwakumba kwa kile kilichowakuta wamefika kituoni Posta majira ya saa 11 ya jioni na hadi ilipofika majira ya saa moja kasorobo hawajapata usafiri na kulazimika watembee kwa miguu kuhamia katika kituo cha nyuma cha Akiba na hali ilikuwa hivyohivyo.

Hali ilivyozidi kuwa tata zaidi waliamua warudi nyuma na kuelekea kituo cha fire ili waweze kupata usafiri na wageuze na mabasi lakini hali hiyo walidumu nayo kwa takribani dakika 45 kituoni hapo bila kuwa na dalili yoyote ya kupata usafiri.

Hiyo ndiyo hali iliyokuwa jana katika jiji la Dar es Salaam kwa wakazi wengi waishio humo wakionekana kurudi kwa miguu kutokana na adha iliyokuwepo

Mapacha Wenye Mguu Mmoja Wanavyowasilimisha Wanakijiji


apacha Pheinbom na Shevoboh wa nchini Cameroon walipozaliwa wakiwa wameungana kuanzia kifuani kushuka chini, wanakijiji waliwaona ni kama mkosi mkubwa kwa jamii lakini baada ya mapacha hao kutenganishwa na madaktari wa Saudi Arabia, mapacha hao wamebadilisha maisha ya wanakijiji na wanakijiji wengi wanabadili dini kuwa waislamu.
Mapacha Pheinbom na Shevoboh walipozaliwa wakiwa wameungana walionekana kama mkosi lakini baada ya kutenganishwa na madaktari wa Saudi Arabia, maisha yao yamebadilika na wamefanikiwa kuwa chachu ya mabadiliko ya maisha katika kijiji chao.

Walipozaliwa wakiwa wameungana kuanzia kifuani kushuka chini, madaktari wa uzazi katika hospitali ya Babanki Tungo, kaskazini magharibi mwa Cameroon waliikimbia Hospitali kutokana na mshtuko wa uzazi huo wa aina yake kijijini hapo.

Baadhi ya wanakijiji waliamini kuwa watoto hao ni adhabu toka kwa mungu kwa baba wa watoto hao ambaye alikuwa na wake wawili na jumla ya watoto 13.

Wanakijiji wengine waliamini kuwa watoto hao ni fimbo ya adhabu kwa kijiji kizima kwani siku chache baada ya kuzaliwa kwa watoto hao mkuu wa kijadi wa kijiji hicho aliuliwa kwa kuchomwa moto akiwa hai na wanakijiji wenye hasira.

Hali ilibadilika baada ya mfalme wa Saudia kukubali kulipa gharama za kuwatenganisha watoto hao mapacha wa kike.

Baada ya operesheni ya masaa 16 iliyofanyika nchini Saudia, madaktari walifanikiwa kuwatenganisha mapacha hao na hivi sasa kila mmoja ana tumbo lake mwenyewe isipokuwa wamebaki na mguu mmoja mmoja.

Ikiwa ni miaka mitatu tangia operesheni hiyo ilipofanyika, mapacha hao wanajiandaa kwenda tena Saudi Arabia kufundishwa jinsi ya kutumia miguu ya bandia kutembea kama watu wengine.

Kijiji cha Babanki Tungo awali kilikuwa ni kijiji kilichojaa waumini wengi wa kikristo lakini hivi sasa hali imebadika baada ya serikali ya Saudi Arabia kuamua kujenga hospitali, shule ya msingi, shule ya chekechea pamoja na kituo cha kiislamu kwenye kijiji hicho.

Wazazi wa mapacha hao ndio waliokuwa wa kwanza kubadili dini na wamekuwa mstari wa mbele katika kutoa mafundisho ya dini ya waislamu yaliyopelekea kusilimu kwa wanakijiji wengi.

Wazee wa kijiji wanahofia kuwa kijiji hicho ambacho awali kilikuwa ni cha kikristo kidogo kidogo kinaanza kubadilika kuwa kijiji cha kiislamu.

Baba wa mapacha hao ambaye awali alikuwa akiitwa Ngong James Akumbu, hivi sasa anaitwa "Abdallah", wakati mama yao aliyeitwa Emerencia hivi sasa anaitwa "Aisha".

"Kabla ya shule kufunguliwa, nilikuwa sina kazi, nilikuwa na wapenzi wengi na nilikuwa mlevi", alisema mwalimu Kum Edwin ambaye naye amebadili dini na hivi sasa anaitwa "Abdallah Wagf".

"Hivi sasa sinywi tena pombe na nimeamua kutafuta mwanamke wa kuoa kwasababu kuwa na wapenzi wengi si tabia nzuri", aliongeza mwalimu Edwin.

"Hivi sasa watu wa kijiji cha Babanki Tungo wanawaona mapacha Pheinbom na Shevoboh kama baraka toka kwa mungu na sio mkosi kama tulivyofikiria awali", alimalizia kusema mwalimu Edwin.

KORTINI KWA UTAPELI ETI WANAO UWEZO WA KUMFUFUA MTU

WAKAZI wawili wa Jiji la Dar es Salaam, wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na tuhuma za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu baada ya kudai wana uwezo wa kumfufua mtoto aliyekufa na kudai hakufa kihalali.
Watuhumiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jana, na kusomewa mashtaka na mwendesha mashtaka wa Polisi, Nassoro Sisiwaya mbele ya Hakimu Suzane Kihawa wa mahakama hiyo.

Sisiwaya alidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja walijipatia fedha taslimu za kitanzania Shilingi milion 3.6 kutoka kwa Amina Juma kwa makubaliano kwamba wana uwezo wa kumfufulia mtoto aliyekufa wa mlalamikaji huyo.

Alidai kuwa washtakiwa hao walitenda kosa hilo, Mei 5 mwaka jana katika eneo la Kimara Baruti na kwamba walidai wana uwezo wa nguvu za kichawi za kuweza kumfufua marehemu huyo na kumrudisha akiwa hai.

Washtakiwa hao ni Shabani Juma (46), mkazi wa Tandale kwa Tumbo ambaye ni mganga wa jadi na Godfrey Zakaria (26) mkazi wa Tandale fundi wa umeme wa magari wote walimuahidi mama huyo kuwa mtoto huyo angefufuka kwa kuwa hakufa kihalali.

Ilidaiwa upelelezi wa shauri hilo umeisha kamilika na kesi itaanza kusikilizwa Mei 17 mwaka huu.

Washtakiwa wako nje kwa dhamana.

THE DEATH OF OUR BELOVED FATHER JOHN IBRAHIM KADIGI


MR. MR. JOHN IBRAHIM KADIGI of Ngudu Mwanza/Morogoro, left his walk of life at the age of 84 on April 21, 2010 at SAIFEE Hospital in Mumbai India, where he went for medical treatment. He survived by his wife Ruth. Sons - Julius and Methuselah/Fimbo. Daughters - Mary, Stelah Mngodo, Eunice, Jane, Katherine, Hellen Mwaituka and Happy Holm. Grandchildren - Jeff, John, James, Jeremiah, Junior, Hellen and David. The family is still on arrangements for taking his body from India to Tanzania for burrial. He will be greatly missed by all his family and friends.

The memorial and fundraising service took place on Sunday April 25, 2010 at 2970 Lorna Rd, Birmingham AL 35216, at 3:00 - 5:00pm. Below are the numbers of what we have raised so far.

OUR GOAL IS TO RAISE $4,000

CHECKS COLLECTED $1,135
CASH COLLECTED $ 540
TOTALS $1,675

WE STILL NEED $2,325

Below are bank accounts information that you can use for sending your donation

BANK NAME: REGIONS BANK
ACCOUNT NO: 0106703879

BANK NAME: WACHOVIA / WELLS FARGO BANK
ACCOUNT NO: 8453467477

For the word of comforty please visit the family at 1106 Colonial Dr. Alabaster AL 35007 or call the Kadigis at (205) 664 - 1197
Job 1:21 "Naked I came from my mother's womb, and naked I will depart. The LORD gave and the LORD has taken away; may the name of the LORD be praised."

If you have any question or you need some more information please write to us at admin@themissionband.org or call

REV. FRED MWAITUKA - (205) 919 - 9978
REV. DEO LUBALA - (205) 477 - 1361
ISACK MAYALA (205) 267 - 2137 of Ngudu Mwanza/Morogoro, left his walk of life at the age of 84 on ApIGIril 21, 2010 at SAIFEE Hospital in Mumbai India, where he went for medical treatment. He survived by his wife Ruth. Sons - Julius and Methuselah/Fimbo. Daughters - Mary, Stelah Mngodo, Eunice, Jane, Katherine, Hellen Mwaituka and Happy Holm. Grandchildren - Jeff, John, James, Jeremiah, Junior, Hellen and David. The family is still on arrangements for taking his body from India to Tanzania for burrial. He will be greatly missed by all his family and friends.

The memorial and fundraising service took place on Sunday April 25, 2010 at 2970 Lorna Rd, Birmingham AL 35216, at 3:00 - 5:00pm. Below are the numbers of what we have raised so far.

OUR GOAL IS TO RAISE $4,000

CHECKS COLLECTED $1,135
CASH COLLECTED $ 540
TOTALS $1,675

WE STILL NEED $2,325

Below are bank accounts information that you can use for sending your donation

BANK NAME: REGIONS BANK
ACCOUNT NO: 0106703879

BANK NAME: WACHOVIA / WELLS FARGO BANK
ACCOUNT NO: 8453467477

For the word of comforty please visit the family at 1106 Colonial Dr. Alabaster AL 35007 or call the Kadigis at (205) 664 - 1197
Job 1:21 "Naked I came from my mother's womb, and naked I will depart. The LORD gave and the LORD has taken away; may the name of the LORD be praised."

If you have any question or you need some more information please write to us at admin@themissionband.org or call

REV. FRED MWAITUKA - (205) 919 - 9978
REV. DEO LUBALA - (205) 477 - 1361
ISACK MAYALA (205) 267 - 2137

Monday, April 26, 2010

SHEREHE ZA MUUNGANO ZILIVYOKUWA SEATTLE WASHINGTON

WADAU WAKISEREBUKA KAMA KAWA NDANI ZA SEHEREHE ZA MUUNGANO SEATTLE.HAPA KWANZIA MAVAZI,LUGHA,CHAKULA STORI YAANI NI TANZANIA TUUUUUU














WAALIMU KUCHAPWA BAKORA NA SUNGUSUNGU KISA KUCHELEWA KWENYE KIKAO


Chama cha walimu Tanzania kimesema kitaishtaki serikali kufuatia tukio la walimu wanne kuchacharazwa bakora mbele ya hadhara na sungusungu kwa kosa la kuchelewa kwenye kikao.
Chama cha walimu Tanzania, kimesema kuwa kimesikitishwa na tukio la kuwadhalilisha walimu kwa kuwacharaza bakora mbele ya hadhara.

Tukio hilo limetokea mkoani Shinyanga ambapo sungusungu waliwacharaza bakora walimu wanne akiwemo mwalimu mmoja mwanamke ambaye alikuwa ni mjamzito.

Walimu hao walicharazwa bakora kwa kosa la kuchelewa kwenye kikao cha walimu na wazazi.

Afisa mmoja wa umoja wa walimu mkoani Shinyanga alisema kuwa wamechoshwa na tabia za mamlaka za dola kuwacharaza bakora walimu na wanatarajia wahusika watafikishwa mahakamani.

Mwaka jana mkuu wa wilaya ya Bukoba, Albert Mnali alisimamishwa kazi baada ya kuwaamuru polisi wawachape bakora walimu 32 kutokana na matokeo mabaya ya mitihani ya darasa la saba.

Mkuu huyo wa wilaya aliamuru polisi mmoja kuwachapa viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizo Bukoba, kutokana na wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba.

Sunday, April 25, 2010

MAITI ZA WATU KUUZWA KWENYE SUPERMAKET UJERUMANI



Yule daktari bingwa wa mifupa wa Ujerumani ambaye mwaka jana aliandaa maonyesho ya maiti zikifanya mapenzi, ameamua kufungua supermarket ambapo atauza vipande vya miili ya watu.
Baada ya kuandaa maonyesho mwaka jana akizionyesha maiti katika hali mbalimbali za kujamiiana, Dr. Gunther von Hagens wa nchini Ujerumani ameamua kuwauzia watu maiti za watu alizo nazo.

Hagens anafungua supermarket ya maiti za binadamu mjini Guben, Brandenburg, ambayo imepangwa kufunguliwa rasmi mei 28 mwaka huu.

Fuvu la binadamu likiwa limening'inizwa kwenye chuma litauzwa euro 1,200.

Hagens pia ana mpango wa kufungua tovuti ya duka hilo ili aweze pia kufanya mauzo online.

Hagens ambaye anajulikana zaidi kama "Dr Death" (Dokta Kifo), ni mtaalamu maarufu wa elimu ya mwili na viungo vya binadamu na wanyama (Anatomy).

Hagens anatumia njia aliyoigundua yeye mwenyewe inayojulikana kitaalamu kama "plastination" ambapo maiti hutolewa ngozi yote na kisha majimaji yote kwenye maiti kukaushwa.

Hagens hutumia plastiki zilizotengenezwa kwa madini ya silicon kuziweka maiti hizo katika maumbile mbali mbali kuonyesha maisha ya kila siku ya mwanadamu.

Hagens alisema kuwa maiti anazozitumia kwenye kazi zake ni za watu waliojitolea miili yao kwake kabla hawajafariki. Hagens aliongeza zaidi kuwa yeye mwenyewe ameishajitolea maiti yake itumike namna hiyo akishafariki.

Mwaka jana Hagens aliingia kwenye mzozo mkubwa wakati alipofungua maonyesho mjini Berlin akiyaweka maumbile ya maiti katika staili mbalimbali za kujamiiana.

Miaka miwili iliyopita Hagens alijaribu kufungua duka la kuuza vipande vya miili ya watu lakini alilazimika kuahirisha mpango wake kutokana na upinzani mkubwa toka kwa makanisa na watu mbalimbali.

Safari hii Hagens amesema ameweka nia ya kweli ya kufungua supermarket hiyo ya maiti za binadamu na amesema hatauahirisha mpango wake kwa sababu yoyote ile.

RAIS WA AFRIKA KUSINI JACOB ZUMA APIMA UKIMWI NA KUWEKA MAJIBU WAPI


Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ambaye mwaka 2006 alifanya mapenzi na mwanamke mwenye ukimwi bila ya kutumia kinga na kuzusha uvumi kuwa na yeye ni muathirika, amepima ukimwi na kuweka majibu yake hadharani.
Rais Zuma amewathibitishia watu kuwe yupo fiti na wala hajaathirika kutokana na vipimo vya HIV alivyofanya mwezi huu ambavyo majibu yake yamewekwa hadharani wananchi wayaone.

"Baada ya kuliangalia suala hili kwa umakini nimeamua kuweka wazi majibu yangu ya vipimo vya HIV .. ili kusisitiza uwazi miongoni mwa watu", alisema Zuma.

Rais Zuma alipima 'Ngoma' aprili nne mwaka huu na majibu yalikuwa ni NEGATIVE. Alisema kuwa kabla ya hapo alishafanya vipimo mara tatu na majibu yalikuwa pia NEGATIVE.

Rais Zuma alifanya vipimo hivyo katika kuiunga mkono kampeni ya kuwahimiza watu wapime ukimwi na wazitambulishe hali zao kama wameathirika.

Kampeni hiyo ina malengo ya kuwapima 'ngoma' jumla ya watu milioni 15 ifikapo mwishoni mwa mwezi juni mwakani.

Mwaka 2006, Rais Zuma alifikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumbaka mwanamke mwenye ukimwi.

Hata hivyo rais Zuma alikanusha kumbaka mwanamke huyo na kusema kuwa alifanya mapenzi na mwanamke huyo kwa hiari yake mwenyewe.

Rais Zuma alikiri pia wakati huo kuwa alifanya mapenzi na mwanamke huyo bila kutumia kinga ingawa alikuwa akijua fika kuwa mwanamke huyo ni muathirika.

Rais Zuma alisema kuwa siku zote hutumia kondomu lakini siku hiyo alikuwa hana kondomu na mwanamke huyo ndiye aliyeanza uchokozi uliopandisha mashetani yake ya ngono.

Kipindi hicho, Rais Zuma aliamsha hasira za wanaharakati wa kupambana na maambukizi ya ukimwi alipoiambia mahakama kuwa alienda kuoga punde baada ya kumaliza kufanya mapenzi na mwanamke aliyeathirika ili kujiepusha na maambukizi ya gonjwa hilo.

Thursday, April 22, 2010

DENI LA TANZANIA LAZIDI KUONGEZEKA


DENI la Taifa limeongezeka maradufu na kufikia shilingi trillion 7.6

Hayo yaliwekwa wazi na katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Ludovick Otouh, alipokuwa akiwajulisha waandishi wahabari.

Amesema deni la taifa limeongezeka kwa kasi kutoka kiasi cha sh trilioni 6.4 mwaka 2007/08 hadi kufikia shilingi trilioni 7.6 katikka mwaka wa fedha wa 2008/09
.
Amesema kuwa deni hilo limeongezeka kwa tofauti ya shilingi trillion 1.1 kutoka lile la mwaka wa fedha wa jana.

Amesema kutokana na hali hiyo, kuna umuhumu wa serikali kusimamia vizuri makusanyo na matumizi ya fedha zake.

Amesema deni hilo limeongezeka hivyo kutokana na serikali kujiingiza katika bajeti kubwa kuliko uwezo wenyewe.

Vilevile amesema serikali imeshindwa kudhibiti matumizi ya juu, kutokuwa makini na mikataba mbalimbali, pamoja na kuzamini mambo mbalimbali kinyume na uwezo halisi.


Hivyo amesema katika taarifa zilizowasilishwa na maofisa masuuli, zilieleza bayana kuwa wizara, idara, walaka na sekretarieti za mikoa hazikuzingatia kikamilifu sheria ya manunuzi ya umma namba 21 ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2005 ambapo jumla ya sh bilioni 12.8 zilionyesha kasoro mbalimbali za ukiukwaji wa taratibu za manunuzi.

Pia alisema katik ukusanyaji wa mapato matokeo ya ukaguzi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), unaonyesha kuwa misamaha mingi iliyotolewa kwa taasisi mbalimbali na watu binafsi yenye thamani ya sh bilioni 752.3 imerudisha nyuma mapato ya serikali.

MSICHANA ABAKWA NA BOSS WAKE

MSICHANA mmoja jina lake halitaweza kuchapishwa kwa leo amebakwa na mwajiri wake usiku wa kuamkia leo
Msichana huyo alifanyawa unyama huo usiku wa kuamikia leo, huko maeneo ya Mbezi anapofanyia kazi yake hiyo aliyodumu nayo kwa muda wa mwaka mmjoa na nusu sasa.

Msichana huyo alionekana akilia na mwandishi wa habari hii huko Kimara, majira ya saa kumi na mbili asubuhi, alipokuja kuomba ushauri kwa ndugu yake wa kutoka kijiji kimoja huko Iringa.

Ndugu yake huyo ambaye ni jirani na mwandishi wa habari hii alidai mdogo wake huyo aliweza kulazimishwa afanye mapenzi na bosi wake huyo ambaye ni mwajiriwa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania na alifanikiwa kumbaka pasipo hiari yake

Alidai msichana huyo kuwa mwajiri wake huyo alimwingilia chumbani majira ya sa saba usiku, na kumtaka afanye nae mapenzi na alishindwa kutoroka kwa kuwa alimzidi nguvu kwa hali ya kuwa yeye ni mwanaume.

Alidai aliweza kuingia katika chumba hicho kwa kuwa chumba hicho hakikumaliza mlango kwani walihamia hivi karibuni bila nyumba hiyo kumalizika ipasavyo.

Alidai mara baada ya kuingia chumbani humo alimuamsha msichana huyo na kushangaa kulikuwa na tatizo gani punde alimuamuru afanya matendo anayoyahitaji na kukataa huku akilia na baba huyo kumuahidi kuwa pindi atakapokubali atamsomesha na kumuhamisha hapo nyumbani.

Mbali na ahadi hiyo binti huyo aliendaelea kugoma huku akilia na kumkatalia ndipo baba huyo alimlazimisha na kumbaka.

Alidai kuwa baba huyo alifanikiwa kumbaka kwa kuwa mke wake alisafiri kwenda kwao mkoani Mbeya kwa mama yake alikwenda huko kwa kuwa alikwenda kujifungua kwao ili akapate uangalizi wa karibu.

Alidai mke wake alisafiri mwanzoni mwa mwezi huu na alimuacha mdogo wake wa waishi nae na kwa jana mdogo wake huyo hakurudi nyumbani na ndiyo baba huyo alitumia fursa hiyo kufanikisha adhama yake.

Hata hivyo kwa maelezo ya haraka haraka alimwambia dada yake huyo anaogopa kurudi tena na atarudi endapo bosi wake kike atakaporudi kwa kuwa aliihitaji kazi yake kwani ndiyo ilikuwa ikimsaidia kujikimu matatizo yake madogomadogo.

JESHI LA POLISI LACHAPISHA KITABU CHA MUONGONZO KWA WAPIGA KURA


JESHI la Polisi Nchini, limetoa kitabu maalum kinachofafanua na kumuongoza mwananchi mchakato mzima wa uchaguzi kwa lengo la kuwezesha uchaguzi, huo kufanyika kwa utulivu na amani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam , Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema alisema kitabu cha Haki na wajibu wa Mpigakura, kimebeba ujumbe mzito unaohusu kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.


Mwema alisema ni haki ya kila Mtanzania aliyetimiza vigezo wa kupiga kura kitabu hicho kitamuongoza katika kuhakikisha kuwa sheria za nchi hazikiukwi kabla na baada ya uchaguzi

Alisema kitabu hicho kinalenga kuufanya uchaguzi huo uwe wa haki katika kuchagua viongozi na kutekeleza wajibu wa usalama, amani na utulivu vinadumu katika jamii.

Alisema kitabu hicho kinaelezea umuhimu wa kujiandikisha kupiga kura, uteuzi wa wagombea katika vyama vya siasa, kampeni za wagombea na vyama vyao na matangazo yatakayowekwa na vyama vya siasa na wagombea.

Mambo mengine ni wajibu na umuhimu wa polisi katika mchakato wa uchaguzi, haki na wajibu wa mpigakura, siku ya uchaguzi, jinsi ya kupiga kura, kusubiri matokeo, kupokea matokeo na uvunjaji wa sheria wakati wa uchaguzi.


Pia alisema “askari polisi watakaovujisha siri za taarifa mbalimbali zinazohusu mitaa katika uchaguzi watachukuliwa hatua kali, pia na mwananchi yeyote atakayehatarisha hatari ama kugundulika kuvunja amani sheria itafata mkondo wake” alisema.

Monday, April 19, 2010

APIGIWA KURA YA U MEAYA WAKATI WAMESHA FARIKI


Wapiga kura nchini Marekani wamemchagua mtu aliyefariki awe meya wao mpya.
Carl Geary alifariki mwezi mmoja uliopita kutokana na shambulio la moyo wakati akipiga kampeni za kuwania umeya wa mji mdogo wa Tracy City, Tennessee nchini Marekani.

Lakini pamoja na kwamba watu wengi walikuwa wakijua kuwa ameishafariki, marehemu Carl alishinda uchaguzi kwa kupata kura nyingi sana mara tatu zaidi ya mpinzani wake.

Mjane wa marehemu Bi Susan Geary alisema kuwa matokeo ya uchaguzi hayamjashangaza kwani aliyatarajia.

"Siku aliyofariki watu walikuwa wakinipigia simu kutoa salamu za rambirambi wakisema kuwa watampigia kura kwenye uchaguzi".

Carl aliyefariki akiwa na umri wa miaka 55, alijulikana sana kwa misimamo yake thabiti ya kisiasa.

Pamoja na kwamba alishazikwa wiki kadhaa zilizopita, Carl alishinda uchaguzi kwa kupata kura 285 huku mpinzani wake akiambulia kura 85.

Mmoja wa wafanyabiashara katika mji huo alisema kuwa watu waliamua kumpigia kura Carl ili kuonyesha upinzani wao kwa meya aliyopo madarakani Bi. Barbara Brock.

"Nilikuwa nikijua kuwa ameishafariki, najua watu wataona kama ni upuuzi lakini tulitaka tupate meya mwingine sio huyu aliyepo", alisema Chris Rogers, mmiliki wa mgahawa mmoja uliopo mjini humo.

"Kama uchaguzi utarudiwa tena wiki ijayo nitampa kura yangu tena marehemu".

Maafisa wa mji huo wamesema kuwa manispaa itafanya kikao kuamua nani awe meya.

UREMBO WASABABISHA KIFO SIKU YA KUZALIWA KWAKE


Mwanamke wa nchini Uingereza aliyesherehekea kutimiza umri wa miaka 34 kwa kutoboa ulimi wake kuweka kichuma amefariki siku mbili baadae kutokana na sumu iliyotokana na kichuma hicho.
Amanda Taylor alipuuza kauli za familia yake kumpinga kuweka kichuma cha inchi moja kwenye ulimi wake na aliamua kuutoboa ulimi wake kuweka kichuma hicho ili kusherehekea kutimiza umri wa miaka 34.

"Kwa muda mrefu alifikiria kuutoboa ulimi wake kuweka kichuma", alisema mama yake Lorraine Taylor mwenye umri wa miaka 61.

"Siku nne kabla ya siku yake ya kuzaliwa aliniambia kuwa anataka kuweka kichuma kwenye ulimi wake siku ya kuzaliwa kwake", aliendelea kusema mama yake.

"Nilimpinga na kumuonya asifanye hivyo lakini alisema kuwa marafiki zake wote wameishaweka vichuma kwenye ndimi zao".

Kwa shingo upande mama yake alimpa ruhusa Amanda kutoboa ulimi wake lakini siku mbili baadae Amanda alikutwa nyumbani kwake akiwa amefariki.

Uchunguzi wa awali ulionyesha kuwa alifariki kutokana na damu yake kuingia sumu iliyotokana na kichuma alichowekewa kwenye ulimi wake.

Uchunguzi zaidi kuhusiana na kifo chake unaendelea.

VIDEO YA MUAFRICA TOKA TOGO ATENGENEZA ROBOT


Kusema ukweli waafrika Mungu katujalia akili nyingi sana lakini hali zetu duni za kiuchumi ndizo siku zote zinazoturudisha nyuma siku zote.
Angalia video ya mwanafunzi huyu wa nchini Togo ambaye kwa kutumia vifaa toka kwenye televisheni mbovu ameweza kutengeneza robot kama yale ambayo makampuni ya nchini Japan yamekuwa yakifanya utafiti kuyaboresha.

Sam Todo ambaye ni mwanafunzi wa nchini Togo alitumia vifaa toka kwenye televisheni mbovu na vifaa vingine vya umeme kuweza kutengeneza robot ambalo linaweza kutembea na kupunga mikono kwa kutumia remote control.


Bila shaka kijana kama huyu kama angeweza kupata vifaa vya kisasa au angepata mfadhili wa kukuza kipaji chake angeweza kufanya mambo makubwa kuliko haya.

Angalia video yake chini.


VIDEO - Waafrika Tupo Fiti Sana Basi tu..

SKENDO YA NGONO NDANI YA TIMU YA TAIFA UFARANSA



Skendo kubwa la ngono limeikumba timu ya taifa ya soka ya Ufaransa ambapo baadhi ya nyota wa timu hiyo ya taifa wanadaiwa kufanya mapenzi na machangudoa wenye umri mdogo.
Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya soka ya Ufaransa wamehusishwa kwenye skendo la kufanya mapenzi na makahaba wenye umri chini ya miaka 18.

Mchezaji nyota wa Ufaransa, Franck Riberry na Sidney Govou ni wachezaji wawili waliotajwa ambao tayari wameishahojiwa na polisi kuhusiana na skendo hilo.

Riberry anayeichezea Bayern Munich ya Ujerumani ana mke lakini naye amenaswa katika skendo hilo akidaiwa kufanya mapenzi na msichana kahaba mwenye umri chini ya miaka 18.

Taarifa zilisema kuwa wachezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa "Les Bleus" walikuwa wakienda sana kwenye klabu moja ya starehe ya jijini Paris ambapo walikuwa wakiandaliwa makahaba wenye umri chini ya miaka 18. Mmoja wa makahaba hao inadaiwa alikuwa na umri wa miaka 14.

Wachezaji wengine nyota wa Ufaransa nao wamehusishwa na skendo hilo lakini majina yao yamewekwa kapuni.

Mmoja wa wachezaji hao alikiri kufanya mapenzi na msichana mwenye umri mdogo lakini alijitetea kuwa wakati huo alikuwa akiamini kuwa mwanamke aliyeletewa ni mtu mzima.

Kuwadi "Pimp" anayedaiwa kuwaandalia wachezaji machangudoa hao ametiwa mbaroni na baadhi ya wasichana hao wanaendelea kuhojiwa na polisi.

Skendo hilo limekuja ikiwa ni miezi miwili tu kabla ya Ufaransa kuja barani Afrika kwaajili ya fainali za kombe la dunia.

BINGWA WA ZAMANI WA NDONDI AJINYONGA


Bingwa wa zamani wa dunia wa ndondi za uzito mwepesi za mashirikisho ya ndondi ya WBC na WBA, Edwin Valero amejinyonga kwa kutumia nguo zake ikiwa ni masaa 48 baada ya kutupwa mahabusu kwa tuhuma za kumuua mke wake.
Edwin Valero, raia wa Venezuela ambaye alikuwa bingwa wa dunia wa mashirikisho ya WBA na WBA katika uzito mwepesi, amejinyonga mwenyewe kwa kutumia nguo zake ndani ya selo ya polisi alipokuwa akishikiliwa kwa tuhuma za kumuua mkewe kwa kumchomachoma na kisu.

Polisi walimtia mbaroni Valero siku ya jumapili baada ya kuukuta mwili wa mkewe Jennifer, 24, kwenye chumba cha hoteli moja mjini Valencia, Venezuela.

Valero alikuwa akitambulika kama shujaa wa Venezuela kutokana na rekodi yake nzuri kwenye ndondi. Alishinda mapambano yake yote 27 ya kimataifa kwa knockout.

Taarifa zinasema kuwa Valero mwenye umri wa miaka 28, aliondoka hotelini hapo majira ya alfajiri ya siku ya jumapili akiwaambia walinzi wa hoteli kuwa amemuua mke wake aliyezaa naye watoto wawili.

Valero inaripotiwa kuwa alikuwa na makosa kadhaa ya uvunjaji wa sheria. Alipigwa marufuku kuendesha gari nchini Marekani na mwezi uliopita alishtakiwa kwa kumshambulia mkewe na kisha kuwatishia maisha madaktari waliokuwa wakimpatia tiba mkewe.

Friday, April 16, 2010

OSAMA BIN LADEN ATISHIA USALAMA KOMBE LA DUNIA


Kundi la Al-Qaeda linaloongozwa na Osama Bin Laden limetishia usalama kwenye kombe la dunia nchini Afrika kwa kuahidi kufanya shambulizi la kigaidi litakaloua mamia ya watu wakati wa mechi kati ya Marekani na Uingereza.
Kundi la Al-Qaeda limetishia kuwaua mamia ya watu watakaohudhuria mechi kati ya Marekani na Uingereza kwenye kombe la dunia nchini Afrika Kusini mwezi juni mwaka huu.

Kundi linalojiita Al-Qaeda in the Islamic Maghreb, limetoa taarifa kwenye website likisema kuwa watu wa kujitoa mhanga wakiwa na mabomu ambayo si rahisi kugundulika kwenye mitambo ya ulinzi, wako tayari kujilipua kwenye mechi kati ya Uingereza na Marekani kwenye uwanja wa Rustenburg juni 12 mwaka huu.

Kundi hilo liliweka taarifa hiyo kwenye tovuti inayoitwa "Mushtaqun Lel Jannah" (Njia ya kuelekea peponi).

"Al-Qaeda watakuwepo kwenye mechi za kombe la dunia", ilisema taarifa hiyo ya Al-Qaeda.

"Litakuwa ni jambo la kufurahisha sana wakati wa mechi kati ya Marekani na Uingereza ikirushwa live kwenye luninga wakati sauti ya mlipuko itakaposikika kwenye majukwaa na kuugeuza uwanja mzima juu chini", iliendelea kusema taarifa hiyo ya Al-Qaeda.

Uingereza na Marekani zipo kwenye kundi moja la C pamoja na Algeria na watapimana ubavu juni 12 kwenye uwanja wa King Bafokeng mjini Rustenburg unaochukua watazamaji 44,500.

Maafisa wa Marekani wamesema kuwa vitisho hivyo vya Al-Qaeda vinachukuliwa kwa uangalifu mkubwa katika kuhakikisha usalama kwenye fainali hizo za kombe la dunia zitakazochukua mwezi mmoja.

Maafisa wa usalama wa Uingereza wamekataa kusema chochote.

Mwezi oktoba mwaka jana, maafisa wa usalama wa Afrika Kusini walisema kuwa wamefanikiwa kulizima jaribio la shambulizi la kigaidi lililokuwa limepangwa lifanyike wakati wa fainali hizo.

Iliripotiwa kuwa maafisa wa Afrika Kusini kwa kushirikiana na maafisa wa Marekani walifanikiwa kuwatia mbaroni watu wanaodaiwa kuwa ni wanachama wa Al-Qaeda nchini Somalia na Msumbiji ambao walikuwa wakijiandaa kufanya shambulizi wakati wa fainali za kombe la dunia.

Serikali ya Afrika Kusini imetangaza kuwa jumla ya polisi 44,000 watalinda usalama kwenye fainali hizo.

WATU 10 WAFARIKI DUNIA BAADA YA MTUMBUI KUPINDUKA

WATU kumi wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kutoka nchini Msumbiji kupinduka katikati ya Mto Ruvuma.
Ajali hiyo ya kusikitisha ilitokea jana , majira ya saa 7:00 mchana katika Kijiji cha Kiromba Mtwara.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mtwara, Steven Buyuya alisema watu hao walikuwa wakirejea kutoka Msumbiji ambako walikuwa wakitoka katika shughuli zao za kilimo na walipofika eneo hilo upepo mkali uliwakumba na kupoteza mwelekeo na mtumbwi huo ukazama majini.


Kamanda alisema mtumbwi huo ulikuwa umebeba abiria 12 na walionusurika ni nahodha na abiria mmoja ambao ni Idrisa Nkerewe aliyekuwa nahodha na Abdallah Kaisi, 32 abiria

Alisema kuwa tayari miili ya watu watatu imeshapatikana na majina na maeneo wanapoishi yametambulika.

MTU MWENYA BAHATI MBAYA KULIKO WOTE NCHINI UINGEREZA


Mkulima wa nchini Uingereza Mick Wilary ambaye anadaiwa kuwa ndiye mtu mwenye bahati mbaya kuliko wote nchini Uingereza kutokana na ajali kibao zinazomkumba, amepata ajali kwa mara nyingine tena iliyoivunja miguu yake yote miwili.
Mick Wilary, mwenye umri wa miaka 58 anadaiwa kuwa ndiye mtu ambaye hana tabasamu kutokana na bahati mbaya zinazomkumba na kumfanya akumbwe na ajali mbaya zinazoyatia maisha yake hatarini.

Mick ameishakumbwa na ajali mbaya zaidi ya 30 na ajali hizo zimepelekea kuvunjika kwa mifupa ya viungo vyake 15.

Katika tukio la hivi karibuni, Mick anaendelea kupatiwa matibabu hospitalini baada ya miguu yake kupondwa na tingatinga.

Katika tukio hilo dereva wa tingatinga akiliendesha tingatinga hilo modeli ya JCB bila ya kuwa mwangalifu, alimgonga Mick na kumbamiza ukutani.

Katika tukio hilo mguu wa kushoto wa Mick ulivunjika na kupinda kuelekea mabegani wakati mguu wake wa kulia ulijeruhiwa na kugeuka ukiangalia nyuma.

Hata hivyo pamoja na ajali hiyo mbaya ya kutisha, madaktari katika hospitali ya Newcastle wamefanikiwa kuiokoa miguu yake na wamesema kuwa ndani ya miezi sita Mick ataweza tena kuitumia miguu yake kutembea.

Ajali ya kuvunjika kwa miguu yake imetokea ikiwa ni miezi michache baada ya kuvunjika kwa enka za miguu yake yote miwili baada ya kuteleza na kuanguka chini alipokanyaga kiazi mviringo.

Miongoni mwa ajali mbaya zilizowahi kumkumba Mick ni kupasuka kwa fuvu la kichwa chake kwenye sakafu alipopigwa mweleka na paka.

Mick pia ameishawahi kuvunjika mbavu, shingo na mikono katika mfululizo wa ajali mbaya zinazoendelea kumkumba ambazo zimeifanya sura yake ikose tabasamu wakati wote.

AZINDUKA TOKA KWENYE KOMA NA KUANZA KUZUNGUMZA KIJERUMANI


Msichana mmoja wa nchini Croatia amewashangaza watu wengi baada ya kuzinduka toka kwenye koma baada ya kupoteza fahamu kwa masaa kadhaa akiwa ameisahau kabisa lugha yake halisi na kuanza kubonga kijerumani kama vile alizaliwa nacho.
Msichana huyo ambaye alipoteza fahamu kwa masaa 24 wiki mbili zilizopita, amewaacha madaktari wakiumiza vichwa kutokana na hali aliyo nayo.

Msichana huyo alizinduka akiwa ameisahau kabisa lugha yake ya Croatia na kuanza kuzungumza kijerumani fasaha kama vile alizaliwa nacho.

Wazazi wake walisema kuwa msichana huyo alikuwa akijifunza kijerumani shuleni na pia akiangalia shoo za kijerumani kwenye luninga lakini kijerumani kilikuwa hakipandi kabisa akishindwa hata kuziunga sentesi kifasaha.

"Huwezi kujua ukizinduka toka kwenye koma ubongo utakuwa katika hali gani", alinukuliwa mkurugenzi wa hospitali ya KB Hospital ambayo msichana huyo alikuwa amelazwa.

Madaktari kadhaa wamejaribu kumfanyia uchunguzi msichana huyo lakini wameshindwa kujua chanzo cha hali iliyomtokea.

Monday, April 12, 2010

NAKAYA SUMARI AJIUNGA NA CHADEMA


MSANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Nakaaya Sumari jana alitangaza rasmi kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akiwa na nia ya kuwahamasisha vijana kujitambua zaidi na kutetea haki zao za msingi na demokrasia kwa ujumla.

Mwanamuziki huyo wa kike, aliyewashangaza watu wengi mkoani hapa kwa kuwa wa kwanza kujiingiza katika masuala ya kisiasa, bila kuhofia ama kuogopa kazi zake zinaweza kushuka kiwango, alisema, ataweza kuendesha shughuli zake za muziki na siasa pia.

Nakaaya alijiunga mapema jana mkoani hapa, mbele ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali na kusema kuwa kwa muda mrefu alikuwa na kiu kubwa ya kujiunga katika chama cha siasa chenye mwelekeo, dira na nia nzuri ya kusaidia wananchi wake, ambapo aliona CHADEMA ndicho chama pekee ambacho kinaweza kutimiza ndoto zake za kujiingiza katika masuala ya siasa.

“Kwa kipindi cha muda mrefu nimekuwa na kiu ya kujiingiza katika siasa, ili kuweza kuwahamasisha vijana wa Kitanzania kujitambua na kutetea haki zao za msingi, hasa kwa demokrasia bila kununuliwa ama kushurutishwa na vyama, ambavyo havina msaada wowote katika maisha yao,” alisema Sumari.

Alisema, kutokana na Tanzania kuwa na vivutio vya kutosha, kuwawezesha wananchi wake wote kuondokana na umaskini, lakini hadi hivi sasa, anashangazwa na chama kilichopo madarakani kushindwa kutatua shida na adha kubwa ya umaskini zinazowakumba Watanzania, ambao wengi wao ni maskini.

“Nchi yetu ina rasilimali za kutosha kabisa, hasa kwa upande wa madini ya Tanzanite ambayo yatosha kuwawezesha wananchi wote kuwa katika kiwango bora na kinachostahili kimaisha, mbali na vivutio vingine vya kitalii vilivyopo, lakini cha kushangaza mpaka hivi sasa, wapo Watanzania ambao wanaishi katika hali duni kimaisha na chini ya dola moja kwa siku,” alisema.

Alisema, amejiunga na chama hicho hivi sasa na si mwaka jana ama mwaka juzi, kutokana na kuona hivi sasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu nchini Tanzania, jamii itamhitaji zaidi katika kuwahamasisha juu ya kujitambua katika haki zao za msingi, hasa katika masuala ya kisiasa.

Vyombo vya habari vilimhoji mwanadada huyo kwa nini katika hatua za kwanza kwa lengo lake la kuamua kuingia katika siasa, ameamua kujiunga na chama hicho badala ya kuingia Chama tawala (CCM), au Chama cha Jamii (CCJ), alijibu kwa mshangao kuwa hajaona kama ni vyama ambavyo vipo kwa ajili ya kusaidia watu, bali ni kwa maslahi yao binafsi.

Nao viongozi wa chama hicho mkoa, waliupongeza uamuzi wa msanii huyo kwa uthubutu wake wa kujiunga katika masula ya siasa bila woga wa aina yoyote ile, huku wakimuahidi kumruhusu kugombea nafasi yoyote ile ya uongozi, pindi atakapotimiza masharti na taratibu zote ndani ya chama.

Viongozi hao walimkabidhi kadi ya uanachama na kumtaka kuwa makini sana, hasa katika kuhamasisha vijana wenzake, huku akiwashawishi wasanii wengine kuingia katika siasa na kuongea yale yote yanayostahili kwa haki kwa manufaa ya nchi yao.

"Ukiwa kama kijana mdogo sana na msanii ambaye ni kioo cha jamii, tunataka tuone bidii yako ya kuweza kufichua na kukemea maovu yote, utakayoyaona ndani ya vuguvugu la kisiasa ndani ya nchi yetu, ili jamii nayo iwe na imani na wanasiasa wake," alisema mmoja wa viongozi hao wa CHADEMA.

Aidha, waliwataka wasanii wote nchini ambao wana uchungu wa kweli katika nchi yao, kujiunga kwa wingi katika chama hicho, ili kuweza kufikia na kutimiza lengo la kuwakomboa wananchi walio wengi masikini na sauti za wanyonge kusikika, hasa katika suala zima la kutatua matatizo yao ikiwa ni pamoja na umaskini.

KIKWETE KUFUNGUA SEMINA YA UKIMWI KWA WANAJESHI



RAIS Jakaya Kikwete kesho anatarajia kufungua kongamano la kimataifa kuhusu tatizo la ugonjwa ukimwi katika majeshi litakalofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha AICC mjini hapa.

Kongamano hilo, linatarajia kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 260 kutoka nchi 70 ambapo hadi sasa nchi 60 zimethibitisha kushiriki kongamano hilo ambalo linaelezwa kuwa la kwanza kufanya nchini.

Msemaji wa jeshi hilo, Luteni Kanali Kapambala Mgawe, alisema kongamano hilo litahudhuriwa na makamanda kutoka nchi za bara la Afrika, Asia, Amerika, Carribean, Ulaya na Marekani.

Luteni Kanali Mgawe, alisema mbali na makamanda wa jeshi pia taasisi za kimataifa zinazojihusisha na mapambano dhidi ya ugonjwa huo zitahudhuria.

Kongamano linafanyika kwa ushirikiano kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kushirikiana na jeshi la Marekani kuhusu masuala ya ukimwi kutokana na askari wengi kufariki kwa ugonjwa huo.

Alisema pia Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Tanzania, Jenerali Aden Mwamunyange, pamoja na makamanda wa ngazi ya juu kutoka JWTZ watahudhuria.

Alisema kongamano hilo linafanyika kwa ushirikiano wa pamoja kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Wizara ya Ulinzi ya Marekani kwa lengo la kukabiliana na tatizo la ugonjwa ukimwi ndani majeshi.

POMBE YA KIENYEJI YAUA WATU 7 NA WENGINE 10 WAISHIA KUPOFUKA


Mmoja wa watu waliopoteza macho yao baada ya kunywa Chang'aa akiwa amelazwa hospitali.

Pombe ya kienyeji maarufu nchini Kenya kama Chang'aa imesababisha vifo vya zaidi ya watu 7 na kupofuka macho kwa watu wengine 10.
Zaidi ya watu saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 10 wamebaki vipofu baada ya kunywa pombe maarufu nchini Kenya kwa jina la Chang'aa.

Wakazi wengi wa kitongoji cha Shauri Moyo jijini Nairobi nchini Kenya walikimbizwa hospitali wakiwa hawajiwezi baada ya kunywa Chang'aa (Gongo).

Katika tukio hilo lililotokea jana ijumaa, watu watatu walifariki kwenye eneo la tukio wakati watu watano walipofuka macho hapohapo ya kubwia kilevi hicho cha kienyeji ambacho ni kinyume cha sheria kukutwa nacho.

Mkuu wa kituo cha polisi cha Buruburu alisema kuwa watu wengi zaidi waliwahishwa kwenye hospitali ya Kenyatta baada ya kunywa pombe hiyo.

Baada ya kunywa pombe hiyo, watu walianza kutoa mapovu mdomoni huku wakilalamika maumivu makali ya tumbo.

Hadi kufikia leo watu waliopoteza macho yao wamefikia 10 huku jumla ya watu 7 tayari wameishapoteza maisha yao.

Sunday, April 11, 2010

ONLINE CHATING YASABABISHA AMUUE MKEWE


Mwanaume mmoja nchini Jordan anashikiliwa na polisi baada ya kumuua mkewe miezi sita baaa ya ndoa yao akidai kuwa alimfumania akichat online na mwanaume mwingine.
Mtuhumiwa alimkaba koo mkewe mwenye umri wa miaka 37 kabla ya kukipasua kwa nyundo kichwa chake na kisha kujaribu kuutupa mwili wake”, alisema msemaji wa polisi.

“Alijaribu kuuchoma moto mwili wake lakini alishindwa. Alidai kuwa mkewe alikuwa na tabia mbaya ya kuchat na mwanaume kwenye internet”, aliendelea kusema msemaji huyo wa polisi.

Mtuhumiwa huyo ambaye ana umri wa miaka 30 anashikiliwa na polisi na anakabiliwa na adhabu ya kifo.

”Baada ya mauaji alitoa taarifa kwa wakwe zake kuwa mkewe amepotea na hajui alipo wakati huo huo watu wengine wawili walienda kutoa taarifa polisi”, alisema msemaji wa polisi.

Lakini hata hivyo kutokana na taarifa zake za utatanishi polisi walimhisi yeye ndiye aliyefanya mauaji ya mkewe.

Baada ya kubanwa sana na polisi mwanaume huyo aliamua kukiri kumuua mkewe akisema kuwa alikuwa hapendi tabia ya mkewe kuchat na mwanaume kwenye internet.

AJALI YA NDEGE YAUA WENGI PAMOJA RAIS WA POLAND



VIDEO - Ndege Yadondoka Rais Wa Poland Afariki
Ndege aliyokuwemo rais wa Poland na mkewe pamoja na maafisa wa serikali yake.

Rais wa Poland, Lech Kaczynski pamoja na mkewe na maafisa wa jeshi na serikali wamefariki dunia baada ya ndege iliyokuwa imebeba abiria 132 kuanguka karibu na uwanja wa ndege nchini Urusi.
Rais Lech Kaczynski wa Poland amefariki dunia kufuatia ajali mbaya ya ndege iliyotokea leo baada ya ndege yake kuanguka kwenye miti karibu na uwanja wa ndege wa Smolensk nchini Urusi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, abiria waote 132 waliokuwemo kwenye ndege hiyo wamefariki dunia.

Miongoni mwa wwaliofariki katika ajali hiyo ni mke wa rais huyo, Maria, Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Andrzej Kremer, Mkuu wa majeshi ya Poland, Franciszek Gagor, na Gavana wa Benki Kuu ya nchi hiyo, Slawomir Skrzypek.

Pia katika orodha ya watu waliofariki kutokana na ajali hiyo ya ndege ni wabunge wa Poland na wanahistoria kadhaa.

Rais huyo wa Poland pamoja na ujumbe wake walikuwa wakielekea katika mji wa Katyn karibu na Smolensk kuhudhuria kumbukumbu ya mauaji ya wafungwa wa vita wa Urusi na Poland waliouawa wakati wa utawala wa kisovieti.

Kufuatia kifo hicho, Spika wa bunge la Poland, Bronislaw Komorowski, anachukua madaraka ya nchi hiyo.

Rais Kaczynsk na mkewe ambao wote wamefariki katika ajali hiyo wameacha mtoto mmoja wa kike, Marta.

Thursday, April 8, 2010

ZITTO KABWE:WANA SIASA WALAUMIWE KUUZWA KWA MITAMBO


MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, amesema wanasiasa nchini ndio wanaopaswa kulaumiwa kwa hatua ya kuuzwa nje, mitambo ya kufulia umeme wa gesi ya Dowans Tanzania.

Kauli ya Zitto imekuja baada ya serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kushindwa kununua mitambo hiyo baada ya maombi yao kupingwa na wanasiasa.

Zitto alitoa shutuma hizo juzi jijini Dar es Salaam katika ofisi ndogo za Bunge, alipokuwa akizungumza kikao cha kujadili ripoti ya hesabu za Tanesco za mwaka 2008.

Ripoti hiyo ilikuwa imewasilishwa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu ya Mashirika ya Umma(POAC).

Taarifa ya kuuzwa kwa Dowans ilibainishwa na Zitto katika kikao hicho.Hata hivyo Zitto hakutaja kampuni iliyonunua mitambo hiyo, wala nchi ilipouzwa, au gharama zake.

"Tayari mitambo ya Dowans imekwishauzwa nje ya nchi. Katika hili wanaotakiwa kulaumiwa ni sisi wanasiasa na si vinginevyo kwa kuwa walipinga Tanesco kununua mitambo hii," alisema Zitto

Hata hivyo mwanasheria wa Tanesco, Subira Wandiba alisema mitambo ya Dowans ya megawati 112 imezwa kwa Tanesco kupitia mahakama, kufuatia kesi iliyofunguliwa na kampuni hiyo iliyorithi mkataba tata wa Richmond Dvelopment LLC.

Alisema hatua hiyo imefanyika kwa matarajio kuwa kama itashinda kesi hiyo, mitambo hiyo itatumika kama fidia.

Februari 21, 2009 Tanesco iliwasilisha dhamira yake ya kutaka kununua mitambo ya Dowans na ilitoa sababu za kiuchumi na kimahitaji za kutetea uamuzi wake huo.

Hatua ya ilikuja takriban miezi miwili tangu uamuzi wake huo ukataliwe katakata na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini Desemba mwaka 2008.

Pamoja na mambo mengine, Tanesco chini ya aliyekuwa Mkurugenzi wake, Dk Idris Rashidi, ilitahadharisha kamati hiyo kwamba utafiti uliofanywa na wataalamu umegundua kwamba kama hatua za haraka hazitachukuliwa , taifa litakabiliwa na tatizo la mgawo wa umeme.

Tanesco pia iliitahadharisha serikali kutafakari uwezekano wa kampuni binafsi kujitokeza na kununua mitambo hiyo na kisha kuliuzia shirika hilo umeme.

Desemba 15 mwaka 2008, Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini ya Bunge ilikataa kuunga mkono uamuzi wa Tanesco kununua mitambo ya Dowans ikisema kuuridhia ilikuwa ni kukiuka utekelezaji wa maazimio yaliyopitishwa na Bunge Februari mwaka 2007 kuhusu kampuni za Richmond na Dowans.

Pia kamati hiyo ilikataa kujihusisha na jambo hilo ikijua kuwa kufanya hivyo ni kuvunja Kanuni ya 53 (8) na 54 (4) za Kanuni za Kudumu za Bunge (toleo la 2007), ambazo zote zinakataza kurudiwa kwa mjadala wa jambo ambalo tayari lilishatolewa uamuzi na Bunge.

Siku moja tu baada ya Kamati hiyo iliyochini ya mbunge wa Jimbo la Bumbulu William Shellukindo kutoa tamko hilo, Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alitangaza uamuzi wa serikali kukubaliana na hatua ya kusitisha nia yake ya kutaka kununua mitambo hiyo ya Dowans.

MAALIM SEIF SHARIF AANDIKA HISTORIA MPYA ZANZIBAR


MILANGO ya mwafaka inazidi kufunguka visiwani Zanzibar, baada ya Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad kwa mara ya kwanza tangu afukuzwe CCM, kuingia makao makuu ya chama hicho Kisiwandui kulikofanyika dua ya kumwombea rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume.

Dua hiyo ilifanyika jana katika Ofisi Kuu ya CCM, Kisiwandui, mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi wa Serikali ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano, mabalozi, viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali.

Hii ni mara ya kwanza katika kipindi cha zaidi ya miaka 20 kwa Maalim Seif kuingia kwenye jengo hilo la CCM tangu afukuzwe uanachama wa chama hicho mwaka 1988.

Akizungumza na waandishi wa habari, muda mfupi baada ya dua hiyo, Seif alisema uamuzi wake wa kushiriki ibada hiyo umelenga kuonyesha kuwa uhasama wa CUF na CCM uliodumu kwa muda mrefu, umemalizika.

Alisema CUF wanautambua mchango mkubwa uliotolewa na mwasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 katika kuijenga Zanzibar imara na yenye umoja.

â€Å“Mzee Karume ndiye aliyeuanzisha msingi wa umoja Zanzibar. Na sisi sasa tunafuata nyayo zake katika kuimarisha umoja, maelewano na mshikamano kwa Wazanzibari wote,â€� alisema Maalim Seif.

Maalim Seif alisema ushiriki wa CUF katika sherehe hizo ni muelekeo mpya wa kuijenga Zanzibar ambapo sasa tafauti za kisiasa zinabakia kwenye sera na itikadi za vyama.

"Uhasama sasa uko kwenye sera na itikadi, lakini, linapokuja suala la kitaifa kama hilo, sote tunabakia kuwa Wazanzibari kwanza, vyama vyetu baadaye,�alisema.

Akizungumza katika dua hiyo, kwa niaba ya Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Mufti Mussa Salim, aliisifu picha iliyojitokeza hapo ya umoja na mshikamano wa Wazanzibari na akaomba iendelee kudumishwa.

â€Å“Marehemu Mzee Karume alisimamia umoja wa Wazanzibari. Na mtoto wake (Rais Amani Karume) leo hii anavaa viatu vya baba yake kwa kuwaunganisha Wazanzibari. Tunamuona Maalim Seif kaja hapa kuunganika na ndugu yake katika kukumbuka kifo cha mzee wao. Huu ndio umoja unaotakiwa,â€� alisema Sheikh Salim.

Askofu Mkuu wa Kanisa la Katoliki, Jimbo la Zanzibar Augustine Shao, alisema kwamba historia ya Zanzibar haiwezi kuzungumzia maendeleo ya visiwa hivi bila kumtaja na kumtukuza Marehemu Mzee Karume, kwani ni kutokana na busara, ubunifu na kipaji alichojaliwa kiongozi huyo na Mwenyezi Mungu, ndio maana Zanzibar imefika ilipofika.

Tokea kufikiwa kwa maridhiano baina ya vyama vya CCM na CUF hapo Novemba 5, 2009, kumekuwa na matukio kadhaa ambapo Maalim Seif na Rais Karume wamekuwa wakikutana katika shughuli za kijamii na kimaendeleo, jambo ambalo hapo nyuma halikuwa likifanyika kutokana na mivutano ya kisiasa.

Juzi Rais Karume alijumuika na waalikwa wengine katika hafla ya harusi ya binti wa Maalim Seif huko Bwawani, mjini Zanzibar, tukio ambalo limezidisha mahusiano ya karibu ya viongozi hao na wafuasi wao.

Baada ya kisomo hicho cha hitima ambacho hufanyika kila Aprili 7, viongozi hao na wananchi walimwombea dua, marehemu Abeid Karume katika kaburi lake lililopo pembezoni mwa afisi hiyo ya CCM Kisiwandui iliyoongozwa na viongozi wa dini mbalimbali kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

Aidha, mjane wa Mzee Karume, Mama Fatma Karume, alishiriki katika hitima hiyo akiongozana na mke wa Rais wa Zanzibar Mama Shadya Karume na mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete na viongozi wengine wanawake wa kitaifa wakiwemo Mawaziri, wabunge, wawakilishini na wananchi kutoka sehemu mbalimbali ya Zanzibar na Tanzania Bara.

Aprili 7, 1972 ndiyo siku aliyouawa Rais wa Kwanza wa Zanzibar marehemu Mzee Abeid Amani Karume na wapinga maendeleo nchini.

Wakati huo huo, Rais Kikwete amekata mzizi wa fitina na kutoa msimamo wa CCM juu ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa visiwani Zanzibar.

Kauli ya Rais Kikwete imekuja siku chache baada ya baadhi ya wana CCM kupita matawini na kueneza uvumi kwamba msimamo wa chama chao juu ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa haujatolewa rasmi.

Mbali ya wana-CCM kupita katika matawi pia wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa upande wa CCM katika kikao kilichomalizika wiki hii waligomea kuuchangia mswaada wa kura ya maoni juu ya uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa wakidai kwamba hawajasikia msimamo wa chama juu ya suala hilo.

Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya kifo cha marehemu Mzee Karume yaliofanyika viwanja vya Maisara Mjini Unguja Rais Kikwete alisema msimamo wa chama ni kuunga mkono uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa.

Hata hivyo, aliwataka vijana kujitokeza kwa wingi katika kupiga kura ya maoni juu ya uundwaji wa serikali hiyo kwani faida zake ni nyingi kuliko hasara.

Alisema serikali ya umoja wa kitaifa ndio yenye maslahi kwa wananchi wa Zanzibar ambayo itavunja mambo yanayojitokeza kila wakati wa uchaguzi pamoja na kuondoa chuki na uhasama miongoni mwa Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla.

Alisema uamuzi huo umepitishwa na CCM hivyo hauna matatizo wala shaka yoyote na azimio hilo lilitokana na kikao kilichofanyika Butiama.

Aidha, Rais Kikwete alisema anajua kwamba kuna hisia na mitazamo tofauti juu ya suala hilo na baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha ukweli juu ya dhana nzima ya kuwepo kwa serikali ya umoja wa kitaifa, lakini msimamo wa chama ni kwamba umefika wakati suala hilo lazima lifanyike kwa kuwa litasaidia kwa kiasi kikubwa kujenga jamii bora.

Alisema uamuzi kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa haukuwa uamuzi rahisi kufikiwa kwa upande wa CCM hata kwa CUF, lakini alitumia msemo wa Kiswahili usemao ‘lisilobudi hutendwa’.

THE PRESIDENT KIKWETE TO MEET THE GERMANY FOREIGN MINISTER


PRESIDENT Jakaya Kikwete is expected to meet the Germany Foreign Minister, Mr Guido Westerwelle, in Dar es Salaam today to discuss issues of development cooperation.

Mr Westerwelle, who is accompanied by his Minister for Development Cooperation, Dirk Niebel, was expected to jet in Dar es Salaam yesterday evening. This will be Westerwelle's first trip to Africa since he became the Deputy Chancellor after his party, FDP, formed a coalition partnership with CDU/CSU parties of Chancellor Angela Merkel last October.

According to the itinerary released by German Embassy Deputy Head of Mission, Political Officer, Mr Clemens Hach, the duo are expected also to meet the Finance and Economic Affairs Minister, Mustafa Mkulo.

Mr Hach said Mr Westerwelle and Niebel will also meet with the President of the International Criminal Tribunal for Rwanda, Judge Dennis Byron. They will launch a project with the aim of sensitizing East African youth on the history of Rwandan Genocide and the importance of international criminal prosecution.

He said the guests will participate in official inauguration of the premises of the German cultural institute, the Goethe-Institute, visit the Ocean Road Hospital and meet representatives of Tanzania Albino Society.

Later in the afternoon, Mr Westerwelle and Tanzanian Foreign Minister Mr Bernard Membe would hold a press conference followed by another one by Niebel and Mkulo.

Mr Hach said the minister had chosen Tanzania as his first destination in his first trip to Africa in recognition of the excellent and long standing bilateral relations between the two countries. "As well as in recognition of Tanzania being Germany's most important development partner in Africa," Mr Hach told the 'Daily News' today.

He said Tanzania was also important because it hosts the East African Community Secretariat and it is also currently holding the chair of the EAC Council.

They are expecting to leave today evening for South Africa (Pretoria and Cape Town, including Robben Island) and proceed to Djibouti, he said.

DIEGO MARADONA ANGATWA USONI NA MBWA WAKE


Diego Maradona aliwahishwa hospitali na kufanyiwa operesheni ya dharura kurekebisha sura yake baada ya kung'atwa vibaya na mbwa wake alipojaribu kumbusu.
Madaktari nchini Argentina walilazimika kumfanyia operesheni ya dharura gwiji wa soka duniani, Diego Maradona ambaye alijeruhiwa vibaya na mmoja wa mbwa wake.

Maradona alishonwa nyuzi 10 kwenye mdomo wake wa juu baada ya kung'atwa na mbwa wake mwenye sura ya kutisha anayeitwa Bela ambaye ni jamii ya mbwa wa kichina wanaoitwa Shar-Pei.

Inadaiwa kuwa Maradona alijaribu kumbusu ili kumliwaza mbwa wake huyo aliyekuwa akisumbuliwa na maumivu ya tumbo ndipo mbwa huyo kwa hasira alipomshambulia mdomoni.

Maradona alipata majeraha makubwa kwenye mdomo wake wa juu na alikimbizwa hospitali huku akivuja damu nyingi.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari, Maradona atalazimika kupumzika kwa siku tatu baada ya kutumia masaa 15 hospitalini.

Maradona hakuzungumza na waandishi wa habari lakini Fernando Molina, mpenzi wa dada yake Maradona, Dalma, aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa Maradona anaendelea vizuri na amepumzika nyumbani kwake.

Maradona aliwahi kulazwa kwenye hospitali hiyo hiyo mwaka 2007 kutokana na maradhi aliyopata kutokana na unywaji pombe uliokithiri.

Maradona mwenye umri wa miaka 49 ndiye anayetarajiwa na Waargentina kuiongoza timu ya taifa ya Argentina kulinyakua kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

Maradona alichaguliwa kuwa kocha wa Argentina mwaka 2008 baada ya kujiuzulu kwa kocha Alfio Basile.

Pamoja na Argentina kutoonyesha uwezo mkubwa katika mechi za hatua ya awali ya kufuzu fainali ya kombe hilo, hatimaye ilifanikiwa kupata tiketi ya kuja Afrika baadae mwaka huu.

Argentina ipo kundi moja na Nigeria pamoja Ugiriki na Korea Kusi

WIVU WA MAPENZI WAPELEKEA AHUKUMIWE KIFO



Mwanamke wa nchini Kuwait ambaye alianzisha moto kwenye harusi kupinga mumewe kuoa mke mwingine na kupelekea vifo vya watu 57 amehukumiwa adhabu ya kifo.
Akitoa hukumu dhidi ya Nasra Yussef Mohammed al-Enezi, 23, jaji Adel al-Sager aliamuru Nasra auliwe kwa kitendo chake cha kuanzisha moto kwenye hema wakati wa sherehe za harusi na kupelekea vifo vya watu 57.

Nasra alipatikana na hatia ya kulichoma moto hema ambalo wanawake na watoto walikuwa wamekaa wakati wa harusi ya mumewe akiongeza mkewe mwingine.

Moto katika tukio hilo la mwezi wa nane mwaka jana, uliwateketeza wanawake na watoto ndani ya dakika 10 tu na ulisababisha majeruhi kadhaa.

Nasra alianzisha moto huo ili kupinga mumewe kuongeza mke mwingine.

Nasra alikamatwa siku moja baada ya wanawake 41 na watoto kufariki kwenye moto uliozuka kwenye hema katika mji wa Jahra uliopo magharibi mwa Kuwait. Idadi ya vifo iliongezeka baadae na kufikia 57.

Awali ilidaiwa kuwa alikuwa amepewa talaka na mumewe lakini wakili wa utetezi walisema kuwa alikuwa bado ni mke wa bwana harusi huyo na alikuwa na mimba ya miezi miwili ambayo mawakili wake wanadai ilitolewa alipokuwa jela.

Nasra na mumewe walikuwa na watoto wawili ambao wote walikuwa na matatizo ya akili.

Mawakili wa Nasra wamesema watakata rufaa ya hukumu hiyo mahakama kuu.