WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Tuesday, May 18, 2010

ATUPWA JELA MAISHA YAKE YOTE BAADA KUMPASUA TUMBO MWANAMKE MWEZIE KWA LENGO LA KUCHUKUA KICHANGA


Mwanamke wa nchini Marekani ambaye alimlaghai mwanamke mjamzito na kumpeleka nyumbani kwake kabla ya kulipasua tumbo lake kwa kisu kwa nia ya kuiba kichanga chake, amehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Mwanamke wa nchini Marekani ambaye alikuwa na shauku ya muda mrefu ya kuwa na mtoto, amehukumiwa kwenda jela maisha baada ya kuiba kichanga toka kwenye tumbo la mwanamke mjamzito.

Andrea Curry-Demus, 40, alipatikana na hatia ya kumuua mwanamke mjamzito Kia Johnson, 18 baada ya kulipasua tumbo lake na kisha kuiba kichanga kilichokuwa tumboni mwake na kujifanya yeye ndiye aliyejifungua kichanga hicho.

Curry-Demus akisomewa hukumu yake aliigeukia familia ya Kia na kuwaambia "Naomba mnisamehe".

"Naiomba radhi familia yake", alisema Curry-Demus kabla ya kumgeukia jaji na kusema "Nimekosa".

Mama yake Kia, Darlene Lee, aliridhishwa na hukumu iliyotolewa ya kifungo cha maisha jela akisema kuwa hakutaka Curry-Demus ahukumiwe adhabu ya kifo kwakuwa anataka ateseke kwa uovu alioufanya.

"Nataka ateseke na aione sura ya mwanangu kila siku anapoamka, afikirie kitendo alichofanya".

Hili si tukio la kwanza la Curry-Demus kujaribu kuiba kichanga toka kwenye tumbo la mwanamke mjamzito, miaka 20 iliyopita, Curry-Demus alihukumiwa kwenda jela miaka 10 baada ya kumchoma na kisu tumboni mwanamke mjamzito akiwa
na nia ya kulipasua tumbo lake na kuiba kichanga chake.

Katika tukio la hivi karibuni Curry-Demus aliiongopea familia yake kuwa yeye ni mjamzito baada ya kumlaghai Kia na kujifanya rafiki yake.

Alikuwa akitamba kwa marafiki zake kuwa yeye ni mjamzito akiwaonyesha picha ya Ultrasound aliyoiiba toka kwa Kia na kisha kuibandika jina lake.

Baada ya kutimiza azma yake ya kuiba kichanga cha Kia, aliiambia familia yake kuwa amejifungua mtoto kabla ya muda wake ingawa vipimo vya hospitali havikuonyesha kama aliwahi kuwa mjamzito.

Alitiwa mbaroni baada ya maiti ya Kia kugundulika nyumbani kwake baada ya majirani kulalamikia harufu kali toka nyumbani kwake.

Kichanga alichokiiba kilinusurika maisha yake na kiliwahishwa hospitali kwa matibabu zaidi.

VIDEO YA BIBI KIZEE ALIYE MALIZA ELIMU YAKE AKIWA NA MIAKA 94


Elimu haina mwisho wala umri, hivyo ndivyo alivyothibitisha bibi wa Marekani mwenye umri wa miaka 94 mwenye wajukuu na vitukuu 41 ambaye mwishoni mwa wiki alisherehekea kumaliza elimu ya shahada ya kwanza na kuwa kikongwe wa pili duniani kumaliza elimu ya juu.
Bibi Hazel Soares, mwenye umri wa miaka 94 wa Oakland, Marekani alikuwa miongoni mwa wanafunzi 500 waliotunukiwa shahada mbalimbali za chuo kikuu.

"Imenichukua muda mrefu sana kumaliza digrii kwakuwa nilikuwa bize sana kwenye maisha yangu",alisema Soares ambaye sasa anamiliki digrii ya Art history.

Soares, ana watoto sita na wajukuu na vitukuu wapatao 40, anashika nafasi ya pili duniani kwa kumaliza digrii akiwa na umri mkubwa sana.

Nola Ochs wa Kansas ndiye anayeshikilia rekodi ya kumaliza digrii akiwa na umri mkubwa kuliko watu wote duniani. Alitunukiwa digrii miaka mitatu iliyopita baada ya kumaliza masomo yake kwenye chuo kikuu cha Fort Hays State University wakati huo akiwa na umri wa miaka 95.

Chini ni VIDEO ya bibi Hazel siku alipomaliza masomo yake.

ASKARI POLISI 5 WA KITUO CHA OYSTERBAY MBARONI KWA KUUA


ASKARI polisi watano wa Kituo cha Oysterbay cha jijini Dar es Salaam, wametiwa mbaroni kwa kuhusishwa na kifo cha Octavian Kashita (38) kilichotokea Jumapili wiki iiyopita aliyedaiwa kuhusika katika tukio la utekaji
Askari hao wamekamatwa na jeshi la polisi nchini wakituhumiwa kusababisha kifo cha raia huyo katika mapambano dhidi yao.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema kuwa, tukio hilo la mauaji lilitokea juzi katika eneo la Victoria katika nyumba za serikali.

Alisema, polisi hao walikwenda eneo la tukio majira ya saa 1:00 jioni baada ya kupata taarifa kutoka kwa dada wa Bariki aitwae Sia Minja za kutekwa nyara kwa mtu aliyetajwa kwa jina la Bariki Minja.

Kova alieleza kuwa walipofika eneo hilo la tukio walipoelekezwa na huyo dada, waliliona gari aina ya Toyota Prado lenye namba za usajili T 864 BHC ambalo ndilo lililodaiwa kutumiwa na watekaji nyara hao na lkufanikiwa kuwakamata vijana wannne waliosadikiwea kuhusika na tukio hilo.

Alisema walipofanikiwa kuwakamata vijana hao walianza kuwahoji na katika gari hilo walimkuta mateka akiwa ndani ya gari hilo akiwa na watuhumiwa.

Alisema katika mahojiano hayo kulizuka vurugu kubwa kati ya polisi na watuhumiwa hao, na kutokana na vurugu hizo polisi mmoja alifyatua risasi na kumpata mtuhumiwa Octavian na kupoteza maisha papo hapo.

Kamanda Kova alieleza kuwa, katika uchunguzi wa awali uliofanywa na jeshi hilo ulibaini kuwa chanzo cha tukio hilo la utekaji nyara ni ugomvi wa muda mrefu wa kifamilia kati ya familia ya Bariki na familia ya Martha Makishe ambaye ni mzazi mwenzake ambapo walizaa mtoto mmoja.

Uchunguzi huo ulibaini mzozo huo wa kifamilia umefikia kufunguliwa kwa kesi ya madai namba 31 ya mwaka huu, katika Mahakama ya Kinondoni ambapo shauri hilo linahusisha ugomvi kati yao wawili kumtunza mtoto wao aitwaje Kinsley Bariki.

Hata hivyo Kamanda Kova alipotakiwa kutaja majina ya watuhumiwa hao wengine alisema majina hayo hayatwekwa wazi sasa kwa sababu za kipolisi na inaweza ikavuruga upelelezi.

Hata hivyo ilidaiwa katika watuhumiwa hao wanne yumo mwanafamilia ambaye inadaiwa ni mtoto wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Celina Kombani lakini Kamanda Kova hakuthibitisha hilo na kusema ni mwanafamilia tu kutoka katika familia hiyo ya waziri.

AMUUA MKEWE KISHA KUILA NYAMA YAKE



Mwanaume mmoja wa nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela miaka 15 baada ya kumuua mkewe kwa kumchoma choma na kisu mara 250 na kisha kula nyama za mapafu yake kabla ya kunywa damu yake mbele ya mtoto wake wa miaka minne.
Mohammad Solaiman alihukumiwa kwenda jela kati ya miaka 15 na kifungo cha maisha kwa kumuua kikatili mkewe Shahida Sultanna ndani ya nyumba yao mjini New York katika tukio lililotokea mwaka 2007.

Binti yao mwenye umri wa miaka minne alikuwa chumba cha pili wakati baba yake alipokuwa akimuua mama yake na alishuhudia kitendo cha baba yake akinywa damu ya mama yake.

"Alichukua maini na mapafu yake na kuyatafuna", alisema dada wa marehemu na kuongeza "Alikunywa damu yake, binti yake ameniambia".

Wakili wa Solaiman, John Scarpa alikanusha madai ya Solaiman kumgeuza asusa mkewe ingawa alikubali kumuua mkewe.

Wakili huyo aliendelea kusema kuwa Solaiman alikuwa akipigwa na kunyanywaswa sana na mkewe na hiyo ndio sababu iliyompelekea kufanya mauaji.

Akitoa hukumu ya kesi hiyo, jaji Richard Buchter alisema kuwa faili la mshtakiwa halikusema chochote kama alikuwa akinyanywaswa na mkewe.

"Tunachojua ni kwamba, mshtakiwa alimchoma na kisu mkewe usoni, shingoni, tumboni, mgomgoni na kwenye maeneo yake ya siri", jaji Buchter alisema.

"Kuthibitisha kitendo chake cha kikatili alimuonyesha binti yake wa miaka minne mabaki ya mwili wa mama yake", aliongeza jaji Buchter.

Solaiman alihukumiwa kwenda jela kati ya kifungo cha miaka 15 na kifungo cha maisha baada ya kukiri kufanya mauaji hayo.

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUIONA MAITI YA AJALI YA NDEGE LIBYA



Afisa mmoja wa Libya amefariki baada ya kuona maiti za ajali ya ndege wakati alipokimbilia kwenye eneo la tukio kutoa msaada.
Afisa huyo ambaye ni mlinzi kwenye uwanja wa ndege alifariki baada ya kuona maiti za watu 102 waliokuwemo kwenye ndege ya Libya ambayo ililipuka wakati wa kutua kwenye uwanja wa ndege wa Tripoli.

Taarifa zinasema kuwa mlinzi huyo alikimbilia kwenye eneo la ajali kwa nia ya kutoa msaada lakini alipofika na kuziona maiti zikiwa zimezagaa kila kona ugonjwa wake wa kisukari ulimzidia na hapo hapo aliiaga dunia.

Taarifa zaidi kuhusiana na kifo chake hazikutolewa ingawa taarifa zilisema kuwa mlinzi huyo alikuwa ni mzee.

Wakati huo huo mtu pekee aliyenusurika kwenye ajali hiyo mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka tisa, Ruben, amesafirishwa leo kurudishwa kwao Uholanzi.

Ruben alikuwa na baba yake, mama yake pamoja na kaka yake mwenye umri wa miaka 11 kwenye ndege hiyo lakini wote walifariki kwenye ajali hiyo.

Ruben na wazazi wake pamoja na kaka yake walikuwa likizo nchini Afrika Kusini kusherehekea ndoa ya wazazi wake kutimiza mwaka mmoja.

Shangazi na mjomba wake toka Uholanzi walikimbilia mjini Tripoli kuwa karibu na mtoto huyo ambaye alikuwa akipatiwa matibabu kutokana na majeraha kadhaa kwenye miguu yake.

Mtoto huyo ameishaambiwa na shangazi yake kuwa wazazi wake na kaka yake wamefariki kwenye ajali hiyo mbaya ya ndege.

AITELEKEZA FAMILIA YAKE BAADA YA KUFANYIWA LIMBWATA NA MTOTO WA KITANGA

MWANAUME mmoja [40] [jina kapuni] mkazi wa Mabibo Jeshini ,amekiri kuwa amefanyiwa mambo anayohisi ni ya kumpumbaza akili na kujikuta akikimbia familia yake na kuhamia kwa msichana mwenye asili ya kitanga bila kujitambua.
Akiongea na mwandishi wa habari hii kwenye mazungumzo ya urafiki, amekiri kuwa inawezekana amefanyiwa kitu mbaya na msichana ambaye hakumtaja jina na kumsahau mke wake na watoto na kwenda kuhamia kwa dada huyo.

Alidai kuwa alipoanza urafiki na dada huyo miezi minane nyuma alikuwa yupo katika hali ya kawaida, lakini ipipotimia kiezi mitano ya urafiki wao alijikuta akiingia katika penzi zito na dada huyo hali ambayo ilimfanya aanze kusahau kidogokidogo familia yake bila kujitambua.

Alidai kuwa alikuwa akienda kwa dada huyo na kuchelewa kurudi nyumbani kwake, mara alijikuta akishindwa kurudi kabisa nyumbani kwake na kulala hukohuko na kumpigia mke wake simu kuwa alikuwa yuko bize kazini na kurudi kesho yake.

Alisema mbaya zaidi alijiona kama yuko tofauti na kuanza kumuona mke wake kama mtu wa kawaida na kumuona dada huyo kama ni mke wake na kuona kamda kitu cha kawaida.

Kutokana na hali hiyo ya kuzidi kusahau familia yake alidai mke wake alikwenda kuripoti kwa ndugu zake yeye na kuulizwa na kukana kuwa si kweli.

Hivyo kadri siku zilivyozidi kwenda hali ndiyo ilizidi kuongezeka ya kusahau familia yake na mke wake kuwataka baadhi ya ya shemeji zake wafike nyumbani kwake walale ili wathibitishe maneno ambayo alikuwa akiwaambia ya kuwa mume wake alikuwa harudi nyumbani.

Shemeji zake hao walithibitisha tukio hilo na kuanza kulifanyia kazi susala hilo na kumfatilia ndugu yao huyo na kugundua kuwa alikuwa akizuzuliwa na mwanamke huyo.

KWa kuwa alikuwa hajitambui ilibidi ndugu hao wamkanye na kumtaka aachane na mwanamke huyo nay eye kukiri ni kweli alikuwa na mahusiano na huyo dada na kuwambia alikuwa anatamani aondokane na hali hiyo lakini alikuwa anashindwa kujinasua kuachana na huyo dada.

“yaani rafiki yangu inawezekana nimeshalishwa limbwata na yule dada kama watu wanavyosema, yaani nimefikia hatua sirudi nyumbani kwangu hii kali? Alisema kaka huyo kwenye mazungumzo na mwandishi wa habari hii

“Na sitamani kumuacha, nimewaambia ndugu zangu mwenye kujua dawa ya kunifanya nirudi nyumbani kwangu anitafutie anipe ili nisisahau kurudi nyumbani kwangu nikienda kwa yule dada, nampenda mkewangu ila ndio hali imenikuta hii” alidai