WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Sunday, May 23, 2010

VIDEO - Wanaume Waliooana Malawi Watupwa Jela Miaka 14


Wanaume wawili wa nchini Malawi ambao waliiga tamaduni za watu wa magharibi na kuamua kuoana na kufanya sherehe kubwa, wamehukumiwa kwenda jela miaka 14 pamoja na kufanyishwa kazi ngumu.
Akitoa hukumu jaji wa mahakama ya Blantyre, Nyakwawa Usiwa-Usiwa alisema kuwa anatoa hukumu kali ili kuwalinda wananchi na watu wenye tabia kama ya wanaume hao waliooana.

Steven Monjeza, 26, na Tiwonge Chimbalanga, 20, walitupwa jela tangia walipotiwa mbaroni mwezi disemba mwaka jana wakati walipofanya sherehe ya harusi yao.

Kukamatwa kwa Monjeza na “mkewe” Tiwonge Chimbalanga kulisababisha Malawi iingie kwenye mgogoro mkubwa na mataifa ya magharibi ambayo yanatoa msaada kwa Malawi. Uingereza ambayo ndiyo mfadhili mkubwa wa Malawi iliweka wazi kukasirishwa kwake na kesi hiyo lakini haikusitisha misaada yake.

Mahakama ilijaa mamia ya watu na wengine walijaa nje ili kujua hukumu ya Monjeza na mwenzake. Walipotolewa mahakamani kupelekwa jela kuanza kutumikia vifungo vyao, baadhi ya watu walipiga kelele na kuwatupia maneno ya kejeli.

“Mmepata mlichostahili”, “Miaka 14 haitoshi ilibidi mfungwe jela miaka 50”.
Akiongea wakati wa kutoa hukumu, Jaji Usiwa-Usiwa alisema “Nitawapa hukumu ya kutisha ili kuilinda jamii na watu kama nyinyi na iwe mfano kwa wengine”.

Wakili wa washtakiwa aliitaka mahakama itoe adhabu ndogo kwakuwa vitendo vya Monjeza na mwenzake havimdhuru mtu mwingine yeyote.

“Ni watu wawili watu wazima ambao wanafanya mambo yao kwa siri. Hakuna mtu atakayedhurika iwapo wataruhusiwa kurudi kwenye jamii”, alisema wakili huyo.

Nayo taasisi ya kutetea haki za binadamu ya Cedep ya nchini Malawi, ilisema kuwa leo ni siku mbaya sana kwa Malawi.

“Inakuwaje wafungwe miaka 14 eti kwakuwa wanapendana? Hata kama wakifungwa jela miaka 20 jinsia zao haziwezi kubadilika”, mwanaharakati wa taasisi hiyo.

Jaji Usiwa-Usiwa alisema kuwa wanaume hao hawakuonyesha dalili yoyote ya kujutia tabia yao mbaya ya Sodoma na Gomora.

Wakati huo huo Marekani imelaani hukumu iliyotolewa na imesema kuwa hukumu hiyo ni hatua moja nyuma katika kulinda haki za binadamu.

Chini ni VIDEO ya Monjeza na mkewe mahakamani jana.


VIDEO - Wanaume Waliooana Malawi Watupwa Jela Miaka 14

Ajisalimisha polisi baada ya kutupa mtoto

JESHI la Polisi Mkoani Pwani, linamshikilia Eliza Mwalongo [20] aliyetupa kichanga mwenye umri wa siku tano mwishoni mwa wiki iliyopita huko Kibaha Kwa Mfipa.
Msichana huyo alitupa kichanga hicho njiani Mei 14 , mwaka huu, majira ya saa 12 asubuhi, na kumfunika kwa majani na miba na kilionekena na wapita njia waliopita katika njia hiyo na kutoa taarifa kituo cha polisi.

Baada ya kupatikana kwa taarifa hiyo kituo cha polisi msichana huyo aliamua kujisalimisha mwenyewe katika ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Kwa Mfipa na baadae kupelekwa kituoni kwa mahojiano zaidi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani, Bw. Absaloom Mwakyoma amesema msichana huyo anahojiwa na baadaye atapelekwa kwa daktari ili akapimwe akili zake kama ziko sawasawa na mara baada ya uchunguzi msichana huyo atafikishwa mahakamani.

Msichana huyo alikuwa ni msichana wa kazi za ndani kwa Meja Mstaafu Lekule ambaye alikuwa akimfanyia kazi za mstaafu huyo lakini alikuwa akiishi kwake.

Kamanda alisema msichana huyo alitokea nyumbani kwao Iringa kuja kutafuta maisha ambapo tayari alishakuwa na mtoto mmoja ambaye alitengana na baba yake baada ya ugumu wa maisha ndipo alipokuja huku na kukutana na mwanaume aliyemzalisha na kuishi nae lakini alimkataa baada ya kuzaa mtoto huyo.
.
Kamanda Mwakyoma amesema kuwa, alipoulizwa ni kwa nini aliamua kufanya kitendo hicho alijitetea kuwa alifikia uamuzi huo kutokana na ugumu wa maisha unaomkabili kwa kuwa alikataliwa na mwanaume aliyemzalisha mtoto huyo.

Pia alisema asingeweza kumuhudumia mtoto huyo kwa kuwa tayari ana mtoto mwingine mdogo mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu na hakuwa na ndugu yoyote wa kumsaidia.

Kichanga hicho cha kiume kilizaliwa Mei 10, mwaka huu, na kimechukuliwa na hospitali ya Tumbi na kinaendelea vizuri.

MTOTO YATIMA AJARIBU KULIPUA UBALOZI WA MAREKANI DAR

MWANAFUNZI Nassib [16] anayekabiliwa na tuhuma za kutaka kujaribu kulipua ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam uchunguzi umebaini kuwa ni yatima anaishi na shangazi yake Kinondoni Moscow.
Habari hizo za uhakika kutoka ndani ya jeshi la polisi, zimebaini hilo na mwanafunzi huyo anaishi na shangazi yake aitwae Chiku Simba baada ya wazazi wake kufariki.

Imefahamika kuwa mtandao wa kigaidi wa Al Qaeda umekuwa ukitumia watoto yatima, watoto wa mitaani na wajane kuwatumia kufanya vitendo vya ugaidi.

Hata hivyo shangazi yake alishangaa kutokana na kitendo hicho na alisema ameshitushwa na taarifa alizozipata kutoka kwenye vyombo vya habari kwa kuwa mtoto wake huyo hakuwa na vitendo vya kihuni na vya ajabu na majirani walithibitisha kuwa mwanafunzi huyo alikuwa ni mkarimu na hakuwa mtu wa makundi na hana tabia ya kukaa vijiweni.

Hata hivyo kati ya wanafunzi nane waliokamatwa juzi na maafisa wa polisi waliounganishwa katika tuhuma hizo saba wameachiwa huru na mmoja ambaye ni Amani Thomas anaendelea kushikiliwa kwa kuwa yeye ndiye aliongozana na Nassib hadi katika jengo hilo la ubalozi .

ATAKA TAKA KISA ATAKA KUPIGWA NA MME WAKE


Mwanamke mmoja nchini Iran amemfikisha mumewe mahakamani akidai talaka kwakuwa mume wake hajawahi kumpiga hata siku moja.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 24 [jina kapuni] alifungua kesi katika mahakama ya masuala ya familia mjini Tehran akilalamika kuwa mumewe hampigi hivyo anataka apewe talaka.

Kwa mujibu wa gazeti moja la kila siku la nchini Iran, mwanamke huyo aliiambia mahakama "Mume wangu ananitumikia na kunitunza vizuri sana lakini mimi nataka awe ananipiga, kama hawezi basi naomba anipe talaka yangu".

Mume wake ambaye ana umri wa miaka 28 alijitetea mahakamani "Mke wangu nampenda sana, sioni sababu ya kumpiga au kutumia maguvu dhidi yake".

Kwakuwa mwanamke huyo alisisitiza kuwa anataka awe anapigwa na mumewe au la apewe talaka, mahakama ilimruhusu mumewe awe anamshushia kipigo mkewe siku moja moja ili kuilinda ndoa yake.

Mumewe kwa shingo upande alikubali na aliahidi kuwa atakuwa akimshushia kipigo mkewe ili kumridhisha.

VIDEO - Panya Ndani ya Ikulu ya Obama


Hotuba ya Rais Barack Obama wa Marekani iliingiliwa na kitu asichokitegemea baada ya panya kukatiza mbele yake wakati akitoa hotuba ndani ya ikulu ya Marekani.
Rais Barack Obama alikuwa akitoa hotuba kwenye bustani maarufu ya Rose Garden iliyopo mbele ya ikulu wakati panya alipojitokeza na kukatiza mbele yake toka upande mmoja kwenye upande mwingine.

Wapiga picha waliokuwepo eneo la tukio hawakupitwa na panya huyo na walifanikiwa kuchukua taswira wakati kiumbe hicho kilipokuwa kikipita mbele ya mkuu wa taifa kubwa duniani.

Haijajulikana kama rais Obama alimuona panya huyo au la kwani alielendelea na hotuba yake bila kutetereka.

Taarifa zinasema kwamba panya huyo alionekana pia akipiga misele kabla ya Obama hajaanza kutoa hotuba yake.

Chini ni VIDEO ya tukio hilo.


VIDEO - Panya Ndani ya Ikulu ya Obama