WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, April 26, 2010

SHEREHE ZA MUUNGANO ZILIVYOKUWA SEATTLE WASHINGTON

WADAU WAKISEREBUKA KAMA KAWA NDANI ZA SEHEREHE ZA MUUNGANO SEATTLE.HAPA KWANZIA MAVAZI,LUGHA,CHAKULA STORI YAANI NI TANZANIA TUUUUUU














WAALIMU KUCHAPWA BAKORA NA SUNGUSUNGU KISA KUCHELEWA KWENYE KIKAO


Chama cha walimu Tanzania kimesema kitaishtaki serikali kufuatia tukio la walimu wanne kuchacharazwa bakora mbele ya hadhara na sungusungu kwa kosa la kuchelewa kwenye kikao.
Chama cha walimu Tanzania, kimesema kuwa kimesikitishwa na tukio la kuwadhalilisha walimu kwa kuwacharaza bakora mbele ya hadhara.

Tukio hilo limetokea mkoani Shinyanga ambapo sungusungu waliwacharaza bakora walimu wanne akiwemo mwalimu mmoja mwanamke ambaye alikuwa ni mjamzito.

Walimu hao walicharazwa bakora kwa kosa la kuchelewa kwenye kikao cha walimu na wazazi.

Afisa mmoja wa umoja wa walimu mkoani Shinyanga alisema kuwa wamechoshwa na tabia za mamlaka za dola kuwacharaza bakora walimu na wanatarajia wahusika watafikishwa mahakamani.

Mwaka jana mkuu wa wilaya ya Bukoba, Albert Mnali alisimamishwa kazi baada ya kuwaamuru polisi wawachape bakora walimu 32 kutokana na matokeo mabaya ya mitihani ya darasa la saba.

Mkuu huyo wa wilaya aliamuru polisi mmoja kuwachapa viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizo Bukoba, kutokana na wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba.