WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Thursday, April 8, 2010

ZITTO KABWE:WANA SIASA WALAUMIWE KUUZWA KWA MITAMBO


MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, amesema wanasiasa nchini ndio wanaopaswa kulaumiwa kwa hatua ya kuuzwa nje, mitambo ya kufulia umeme wa gesi ya Dowans Tanzania.

Kauli ya Zitto imekuja baada ya serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kushindwa kununua mitambo hiyo baada ya maombi yao kupingwa na wanasiasa.

Zitto alitoa shutuma hizo juzi jijini Dar es Salaam katika ofisi ndogo za Bunge, alipokuwa akizungumza kikao cha kujadili ripoti ya hesabu za Tanesco za mwaka 2008.

Ripoti hiyo ilikuwa imewasilishwa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu ya Mashirika ya Umma(POAC).

Taarifa ya kuuzwa kwa Dowans ilibainishwa na Zitto katika kikao hicho.Hata hivyo Zitto hakutaja kampuni iliyonunua mitambo hiyo, wala nchi ilipouzwa, au gharama zake.

"Tayari mitambo ya Dowans imekwishauzwa nje ya nchi. Katika hili wanaotakiwa kulaumiwa ni sisi wanasiasa na si vinginevyo kwa kuwa walipinga Tanesco kununua mitambo hii," alisema Zitto

Hata hivyo mwanasheria wa Tanesco, Subira Wandiba alisema mitambo ya Dowans ya megawati 112 imezwa kwa Tanesco kupitia mahakama, kufuatia kesi iliyofunguliwa na kampuni hiyo iliyorithi mkataba tata wa Richmond Dvelopment LLC.

Alisema hatua hiyo imefanyika kwa matarajio kuwa kama itashinda kesi hiyo, mitambo hiyo itatumika kama fidia.

Februari 21, 2009 Tanesco iliwasilisha dhamira yake ya kutaka kununua mitambo ya Dowans na ilitoa sababu za kiuchumi na kimahitaji za kutetea uamuzi wake huo.

Hatua ya ilikuja takriban miezi miwili tangu uamuzi wake huo ukataliwe katakata na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini Desemba mwaka 2008.

Pamoja na mambo mengine, Tanesco chini ya aliyekuwa Mkurugenzi wake, Dk Idris Rashidi, ilitahadharisha kamati hiyo kwamba utafiti uliofanywa na wataalamu umegundua kwamba kama hatua za haraka hazitachukuliwa , taifa litakabiliwa na tatizo la mgawo wa umeme.

Tanesco pia iliitahadharisha serikali kutafakari uwezekano wa kampuni binafsi kujitokeza na kununua mitambo hiyo na kisha kuliuzia shirika hilo umeme.

Desemba 15 mwaka 2008, Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini ya Bunge ilikataa kuunga mkono uamuzi wa Tanesco kununua mitambo ya Dowans ikisema kuuridhia ilikuwa ni kukiuka utekelezaji wa maazimio yaliyopitishwa na Bunge Februari mwaka 2007 kuhusu kampuni za Richmond na Dowans.

Pia kamati hiyo ilikataa kujihusisha na jambo hilo ikijua kuwa kufanya hivyo ni kuvunja Kanuni ya 53 (8) na 54 (4) za Kanuni za Kudumu za Bunge (toleo la 2007), ambazo zote zinakataza kurudiwa kwa mjadala wa jambo ambalo tayari lilishatolewa uamuzi na Bunge.

Siku moja tu baada ya Kamati hiyo iliyochini ya mbunge wa Jimbo la Bumbulu William Shellukindo kutoa tamko hilo, Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alitangaza uamuzi wa serikali kukubaliana na hatua ya kusitisha nia yake ya kutaka kununua mitambo hiyo ya Dowans.

MAALIM SEIF SHARIF AANDIKA HISTORIA MPYA ZANZIBAR


MILANGO ya mwafaka inazidi kufunguka visiwani Zanzibar, baada ya Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad kwa mara ya kwanza tangu afukuzwe CCM, kuingia makao makuu ya chama hicho Kisiwandui kulikofanyika dua ya kumwombea rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume.

Dua hiyo ilifanyika jana katika Ofisi Kuu ya CCM, Kisiwandui, mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi wa Serikali ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano, mabalozi, viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali.

Hii ni mara ya kwanza katika kipindi cha zaidi ya miaka 20 kwa Maalim Seif kuingia kwenye jengo hilo la CCM tangu afukuzwe uanachama wa chama hicho mwaka 1988.

Akizungumza na waandishi wa habari, muda mfupi baada ya dua hiyo, Seif alisema uamuzi wake wa kushiriki ibada hiyo umelenga kuonyesha kuwa uhasama wa CUF na CCM uliodumu kwa muda mrefu, umemalizika.

Alisema CUF wanautambua mchango mkubwa uliotolewa na mwasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 katika kuijenga Zanzibar imara na yenye umoja.

“Mzee Karume ndiye aliyeuanzisha msingi wa umoja Zanzibar. Na sisi sasa tunafuata nyayo zake katika kuimarisha umoja, maelewano na mshikamano kwa Wazanzibari wote,� alisema Maalim Seif.

Maalim Seif alisema ushiriki wa CUF katika sherehe hizo ni muelekeo mpya wa kuijenga Zanzibar ambapo sasa tafauti za kisiasa zinabakia kwenye sera na itikadi za vyama.

"Uhasama sasa uko kwenye sera na itikadi, lakini, linapokuja suala la kitaifa kama hilo, sote tunabakia kuwa Wazanzibari kwanza, vyama vyetu baadaye,�alisema.

Akizungumza katika dua hiyo, kwa niaba ya Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Mufti Mussa Salim, aliisifu picha iliyojitokeza hapo ya umoja na mshikamano wa Wazanzibari na akaomba iendelee kudumishwa.

“Marehemu Mzee Karume alisimamia umoja wa Wazanzibari. Na mtoto wake (Rais Amani Karume) leo hii anavaa viatu vya baba yake kwa kuwaunganisha Wazanzibari. Tunamuona Maalim Seif kaja hapa kuunganika na ndugu yake katika kukumbuka kifo cha mzee wao. Huu ndio umoja unaotakiwa,� alisema Sheikh Salim.

Askofu Mkuu wa Kanisa la Katoliki, Jimbo la Zanzibar Augustine Shao, alisema kwamba historia ya Zanzibar haiwezi kuzungumzia maendeleo ya visiwa hivi bila kumtaja na kumtukuza Marehemu Mzee Karume, kwani ni kutokana na busara, ubunifu na kipaji alichojaliwa kiongozi huyo na Mwenyezi Mungu, ndio maana Zanzibar imefika ilipofika.

Tokea kufikiwa kwa maridhiano baina ya vyama vya CCM na CUF hapo Novemba 5, 2009, kumekuwa na matukio kadhaa ambapo Maalim Seif na Rais Karume wamekuwa wakikutana katika shughuli za kijamii na kimaendeleo, jambo ambalo hapo nyuma halikuwa likifanyika kutokana na mivutano ya kisiasa.

Juzi Rais Karume alijumuika na waalikwa wengine katika hafla ya harusi ya binti wa Maalim Seif huko Bwawani, mjini Zanzibar, tukio ambalo limezidisha mahusiano ya karibu ya viongozi hao na wafuasi wao.

Baada ya kisomo hicho cha hitima ambacho hufanyika kila Aprili 7, viongozi hao na wananchi walimwombea dua, marehemu Abeid Karume katika kaburi lake lililopo pembezoni mwa afisi hiyo ya CCM Kisiwandui iliyoongozwa na viongozi wa dini mbalimbali kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

Aidha, mjane wa Mzee Karume, Mama Fatma Karume, alishiriki katika hitima hiyo akiongozana na mke wa Rais wa Zanzibar Mama Shadya Karume na mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete na viongozi wengine wanawake wa kitaifa wakiwemo Mawaziri, wabunge, wawakilishini na wananchi kutoka sehemu mbalimbali ya Zanzibar na Tanzania Bara.

Aprili 7, 1972 ndiyo siku aliyouawa Rais wa Kwanza wa Zanzibar marehemu Mzee Abeid Amani Karume na wapinga maendeleo nchini.

Wakati huo huo, Rais Kikwete amekata mzizi wa fitina na kutoa msimamo wa CCM juu ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa visiwani Zanzibar.

Kauli ya Rais Kikwete imekuja siku chache baada ya baadhi ya wana CCM kupita matawini na kueneza uvumi kwamba msimamo wa chama chao juu ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa haujatolewa rasmi.

Mbali ya wana-CCM kupita katika matawi pia wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa upande wa CCM katika kikao kilichomalizika wiki hii waligomea kuuchangia mswaada wa kura ya maoni juu ya uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa wakidai kwamba hawajasikia msimamo wa chama juu ya suala hilo.

Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya kifo cha marehemu Mzee Karume yaliofanyika viwanja vya Maisara Mjini Unguja Rais Kikwete alisema msimamo wa chama ni kuunga mkono uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa.

Hata hivyo, aliwataka vijana kujitokeza kwa wingi katika kupiga kura ya maoni juu ya uundwaji wa serikali hiyo kwani faida zake ni nyingi kuliko hasara.

Alisema serikali ya umoja wa kitaifa ndio yenye maslahi kwa wananchi wa Zanzibar ambayo itavunja mambo yanayojitokeza kila wakati wa uchaguzi pamoja na kuondoa chuki na uhasama miongoni mwa Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla.

Alisema uamuzi huo umepitishwa na CCM hivyo hauna matatizo wala shaka yoyote na azimio hilo lilitokana na kikao kilichofanyika Butiama.

Aidha, Rais Kikwete alisema anajua kwamba kuna hisia na mitazamo tofauti juu ya suala hilo na baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha ukweli juu ya dhana nzima ya kuwepo kwa serikali ya umoja wa kitaifa, lakini msimamo wa chama ni kwamba umefika wakati suala hilo lazima lifanyike kwa kuwa litasaidia kwa kiasi kikubwa kujenga jamii bora.

Alisema uamuzi kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa haukuwa uamuzi rahisi kufikiwa kwa upande wa CCM hata kwa CUF, lakini alitumia msemo wa Kiswahili usemao ‘lisilobudi hutendwa’.

THE PRESIDENT KIKWETE TO MEET THE GERMANY FOREIGN MINISTER


PRESIDENT Jakaya Kikwete is expected to meet the Germany Foreign Minister, Mr Guido Westerwelle, in Dar es Salaam today to discuss issues of development cooperation.

Mr Westerwelle, who is accompanied by his Minister for Development Cooperation, Dirk Niebel, was expected to jet in Dar es Salaam yesterday evening. This will be Westerwelle's first trip to Africa since he became the Deputy Chancellor after his party, FDP, formed a coalition partnership with CDU/CSU parties of Chancellor Angela Merkel last October.

According to the itinerary released by German Embassy Deputy Head of Mission, Political Officer, Mr Clemens Hach, the duo are expected also to meet the Finance and Economic Affairs Minister, Mustafa Mkulo.

Mr Hach said Mr Westerwelle and Niebel will also meet with the President of the International Criminal Tribunal for Rwanda, Judge Dennis Byron. They will launch a project with the aim of sensitizing East African youth on the history of Rwandan Genocide and the importance of international criminal prosecution.

He said the guests will participate in official inauguration of the premises of the German cultural institute, the Goethe-Institute, visit the Ocean Road Hospital and meet representatives of Tanzania Albino Society.

Later in the afternoon, Mr Westerwelle and Tanzanian Foreign Minister Mr Bernard Membe would hold a press conference followed by another one by Niebel and Mkulo.

Mr Hach said the minister had chosen Tanzania as his first destination in his first trip to Africa in recognition of the excellent and long standing bilateral relations between the two countries. "As well as in recognition of Tanzania being Germany's most important development partner in Africa," Mr Hach told the 'Daily News' today.

He said Tanzania was also important because it hosts the East African Community Secretariat and it is also currently holding the chair of the EAC Council.

They are expecting to leave today evening for South Africa (Pretoria and Cape Town, including Robben Island) and proceed to Djibouti, he said.

DIEGO MARADONA ANGATWA USONI NA MBWA WAKE


Diego Maradona aliwahishwa hospitali na kufanyiwa operesheni ya dharura kurekebisha sura yake baada ya kung'atwa vibaya na mbwa wake alipojaribu kumbusu.
Madaktari nchini Argentina walilazimika kumfanyia operesheni ya dharura gwiji wa soka duniani, Diego Maradona ambaye alijeruhiwa vibaya na mmoja wa mbwa wake.

Maradona alishonwa nyuzi 10 kwenye mdomo wake wa juu baada ya kung'atwa na mbwa wake mwenye sura ya kutisha anayeitwa Bela ambaye ni jamii ya mbwa wa kichina wanaoitwa Shar-Pei.

Inadaiwa kuwa Maradona alijaribu kumbusu ili kumliwaza mbwa wake huyo aliyekuwa akisumbuliwa na maumivu ya tumbo ndipo mbwa huyo kwa hasira alipomshambulia mdomoni.

Maradona alipata majeraha makubwa kwenye mdomo wake wa juu na alikimbizwa hospitali huku akivuja damu nyingi.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari, Maradona atalazimika kupumzika kwa siku tatu baada ya kutumia masaa 15 hospitalini.

Maradona hakuzungumza na waandishi wa habari lakini Fernando Molina, mpenzi wa dada yake Maradona, Dalma, aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa Maradona anaendelea vizuri na amepumzika nyumbani kwake.

Maradona aliwahi kulazwa kwenye hospitali hiyo hiyo mwaka 2007 kutokana na maradhi aliyopata kutokana na unywaji pombe uliokithiri.

Maradona mwenye umri wa miaka 49 ndiye anayetarajiwa na Waargentina kuiongoza timu ya taifa ya Argentina kulinyakua kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

Maradona alichaguliwa kuwa kocha wa Argentina mwaka 2008 baada ya kujiuzulu kwa kocha Alfio Basile.

Pamoja na Argentina kutoonyesha uwezo mkubwa katika mechi za hatua ya awali ya kufuzu fainali ya kombe hilo, hatimaye ilifanikiwa kupata tiketi ya kuja Afrika baadae mwaka huu.

Argentina ipo kundi moja na Nigeria pamoja Ugiriki na Korea Kusi

WIVU WA MAPENZI WAPELEKEA AHUKUMIWE KIFO



Mwanamke wa nchini Kuwait ambaye alianzisha moto kwenye harusi kupinga mumewe kuoa mke mwingine na kupelekea vifo vya watu 57 amehukumiwa adhabu ya kifo.
Akitoa hukumu dhidi ya Nasra Yussef Mohammed al-Enezi, 23, jaji Adel al-Sager aliamuru Nasra auliwe kwa kitendo chake cha kuanzisha moto kwenye hema wakati wa sherehe za harusi na kupelekea vifo vya watu 57.

Nasra alipatikana na hatia ya kulichoma moto hema ambalo wanawake na watoto walikuwa wamekaa wakati wa harusi ya mumewe akiongeza mkewe mwingine.

Moto katika tukio hilo la mwezi wa nane mwaka jana, uliwateketeza wanawake na watoto ndani ya dakika 10 tu na ulisababisha majeruhi kadhaa.

Nasra alianzisha moto huo ili kupinga mumewe kuongeza mke mwingine.

Nasra alikamatwa siku moja baada ya wanawake 41 na watoto kufariki kwenye moto uliozuka kwenye hema katika mji wa Jahra uliopo magharibi mwa Kuwait. Idadi ya vifo iliongezeka baadae na kufikia 57.

Awali ilidaiwa kuwa alikuwa amepewa talaka na mumewe lakini wakili wa utetezi walisema kuwa alikuwa bado ni mke wa bwana harusi huyo na alikuwa na mimba ya miezi miwili ambayo mawakili wake wanadai ilitolewa alipokuwa jela.

Nasra na mumewe walikuwa na watoto wawili ambao wote walikuwa na matatizo ya akili.

Mawakili wa Nasra wamesema watakata rufaa ya hukumu hiyo mahakama kuu.