WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Sunday, March 28, 2010

INDIGENATION


FROM ARUSHA TO WASHINGTON DC
For all of you who resides in DC Metro Area, come join your country men in a Roots Reggae Jam Session and a debut show for Indigenation, a new Reggae Group lead by GMtui.

Thursday April 8th @ 9:30pm
Cover: Free
Location: O'Shaughnessy's Pub. 1324 King Street. Alexandria, VA 22314.

See Ad on Facebook (Indigenation Roots Reggae), CityPaper, www.tanzamerica.blogspot.com and more

Come one, Come all, Support the local.

iNdiGeNation
From Arusha to DC as it was from Hebron To Babylon.

SIMBA KUVUNJA REKODI YA MWAKA 1993



Wachezaji wa Simba wakishangilia ushindi katika mojawapo ya mechi za ligi kuu ya Bara Saturday, March 27, 2010 3:51 AM
MABINGWA wa Bara, timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam wamepania kuvunja rekodi yao ya mwaka 1993 ya kufika fainali ya Kombe la CAF, ambapo sasa wanataka kutwaa taji la Shirikisho hilo la Afrika. Simba mwaka 1993 ilitolewa katika fainali za CAF baada ya kufungwa 2-1 na timu ya Stella Abdjan katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa (sasa Uhuru).

Katika mchezo wao wa kwanza, timu hizo zilitoka suluhu na hivyo Simba ilihitaji ushindi wa angalau bao 1-0 ili kutwaa taji hilo.

Meneja wa timu hiyo, Innocent Njovu alisema jijini kuwa wana uhakika wa kutwaa taji hilo kutokana na kuwa na kikosi bora kama cha mwaka 1993.

Njovu alisema mbali na kikosi hicho kuwa bora pia wachezaji wao wamekuwa na ari ya ushindi baada ya kutwaa ubingwa wa bara mapema kabla ya ligi kumalizika, wakiwa wamesaliwa na mechi mbili kibindoni.

"Sisi tuna uhakika wa kufika kwenye fainali kwani kwa sasa kikosi ni bora, na wana ari ya kushinda katika kila mechi wanayocheza, hivyo kutokana na dhamira hiyo tuna uhakika wa kufikia hatua ya juu zaidi yaani ya fainali," alisema Njovu.

Alisema baada ya kuwapa mapumziko mafupi wachezaji wao, watapiga kambi huko Zanzibar kujiandaa na mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Lenghten ya Zimbabwe.

Katika mchezo wa awali uliofanyika Zimbabwe Ijumaa iliyopita, ambao Simba iliyofuzu hatua ya pili moja kwa moja, waliwashinda wapinzani wao kwao kwa magoli 3-0, ushindi ambao ni mnono kwa klabu hiyo.

Hata hivyo, Njovu alisema wapinzani wao sio wa kubeza kutokana na kandanda safi waliyoionyesha na wanaamini mchezo wa marudiano utakaofanyika Jumapili ijayo jijini Dar es Salaam, utakuwa wa ushindani mkubwa.

KAPUYA AWEKA UWAZIRI PEMBENI NA KUANZA KUPEKECHA



Katika hali isiyo ya kawaida kwa viongozi wa juu nchini kuonekana katika kumbi za starehe tena katika sare sambamba na waimbaji wa bendi, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya aliingia ukumbini na kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya wana wa Akudo. Huku akiwa amevalia sare sawa na waimbaji wa bendi ya Akudo, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya alijitosa ukumbini na kuanza kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya bendi ya Akudo Impact iliyokuwa ikitoa burudani kwenye ukumbi wa Msasani Beach.

Kapuya ambaye ndiye mmliki wa bendi hiyo alijimwaga stejini na kusakata muziki kwa nguvu zote huku jasho likimtoka akiwa pamoja na mpambe wake ambaye jina lake halikufahamika.

Kapuya anakuwa kiongozi wa pili wa juu serikalini kumiliki bendi wa kwanza alikuwa Waziri Mdhihiri Mdhihiri ambaye aliwahi kumiliki bendi ya Mchinga Sound ambayo baadaye ilivunjika.

Kutokana na jinsi anavyoithamini bendi yake, waziri Kapuya amefanikiwa kuifanya bendi ya Akudo iwe miongoni mwa bendi zinazopendwa sana nchini kiasi cha kuleta ushindani mkubwa katika medani ya muziki wa dansi hapa nchini.

BABU WA MIAKA 96 AMUOA MWANAMKE WA MIAKA 30



Babu mwenye umri wa miaka 96 wa nchini Taiwan amekuwa gumzo nchini humo baada ya kufunga ndoa na mwanamke aliyemzidi miaka 66. Babu Lin Chung ameweka rekodi ya kuwa bwana harusi mwenye umri mkubwa kuliko wote nchini Taiwan baada ya kufunga ndoa na mwanamke mwenye umri wa miaka 30.

Chung amekuwa gumzo kwenye kitongoji cha Tainan baada ya kumuoa mwanamke huyo anayetoka maeneo ya ukanda wa kati nchini China katika jimbo la Hunan.

Chung ambaye hakuwahi kuoa katika ujana wake, ana watoto wawili aliojitolea kuwalea tangia walipokuwa wadogo ambao hivi sasa mmoja kati ya watoto hao ana umri wa miaka 68.

Chung anadai kwamba miaka mitatu iliyopita, alipewa maelezo na Mungu aende kwenye jimbo la Hunan nchini China ili kumtafuta mwanamke anayekuja kuwa mke wake.

Chung alifunga ndoa na mwanamke huyo hivi karibuni pamoja na upinzani mkali toka kwa mwanae huyo wa kujitolea ambaye alikuwa akimuona babu huyo kama amelaghaiwa.

"Inanibidi niwe na mwenza katika uzee wangu... sikuwahi kuwa na mke, kwanini hivi sasa hataki mimi nioe", alisema Mzee Chung.

Chung hivi sasa anashughulikia taratibu za kisheria kumwezesha mkewe ahamie Taiwan toka China ili waishi pamoja.