WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, April 12, 2010

NAKAYA SUMARI AJIUNGA NA CHADEMA


MSANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Nakaaya Sumari jana alitangaza rasmi kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akiwa na nia ya kuwahamasisha vijana kujitambua zaidi na kutetea haki zao za msingi na demokrasia kwa ujumla.

Mwanamuziki huyo wa kike, aliyewashangaza watu wengi mkoani hapa kwa kuwa wa kwanza kujiingiza katika masuala ya kisiasa, bila kuhofia ama kuogopa kazi zake zinaweza kushuka kiwango, alisema, ataweza kuendesha shughuli zake za muziki na siasa pia.

Nakaaya alijiunga mapema jana mkoani hapa, mbele ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali na kusema kuwa kwa muda mrefu alikuwa na kiu kubwa ya kujiunga katika chama cha siasa chenye mwelekeo, dira na nia nzuri ya kusaidia wananchi wake, ambapo aliona CHADEMA ndicho chama pekee ambacho kinaweza kutimiza ndoto zake za kujiingiza katika masuala ya siasa.

“Kwa kipindi cha muda mrefu nimekuwa na kiu ya kujiingiza katika siasa, ili kuweza kuwahamasisha vijana wa Kitanzania kujitambua na kutetea haki zao za msingi, hasa kwa demokrasia bila kununuliwa ama kushurutishwa na vyama, ambavyo havina msaada wowote katika maisha yao,” alisema Sumari.

Alisema, kutokana na Tanzania kuwa na vivutio vya kutosha, kuwawezesha wananchi wake wote kuondokana na umaskini, lakini hadi hivi sasa, anashangazwa na chama kilichopo madarakani kushindwa kutatua shida na adha kubwa ya umaskini zinazowakumba Watanzania, ambao wengi wao ni maskini.

“Nchi yetu ina rasilimali za kutosha kabisa, hasa kwa upande wa madini ya Tanzanite ambayo yatosha kuwawezesha wananchi wote kuwa katika kiwango bora na kinachostahili kimaisha, mbali na vivutio vingine vya kitalii vilivyopo, lakini cha kushangaza mpaka hivi sasa, wapo Watanzania ambao wanaishi katika hali duni kimaisha na chini ya dola moja kwa siku,” alisema.

Alisema, amejiunga na chama hicho hivi sasa na si mwaka jana ama mwaka juzi, kutokana na kuona hivi sasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu nchini Tanzania, jamii itamhitaji zaidi katika kuwahamasisha juu ya kujitambua katika haki zao za msingi, hasa katika masuala ya kisiasa.

Vyombo vya habari vilimhoji mwanadada huyo kwa nini katika hatua za kwanza kwa lengo lake la kuamua kuingia katika siasa, ameamua kujiunga na chama hicho badala ya kuingia Chama tawala (CCM), au Chama cha Jamii (CCJ), alijibu kwa mshangao kuwa hajaona kama ni vyama ambavyo vipo kwa ajili ya kusaidia watu, bali ni kwa maslahi yao binafsi.

Nao viongozi wa chama hicho mkoa, waliupongeza uamuzi wa msanii huyo kwa uthubutu wake wa kujiunga katika masula ya siasa bila woga wa aina yoyote ile, huku wakimuahidi kumruhusu kugombea nafasi yoyote ile ya uongozi, pindi atakapotimiza masharti na taratibu zote ndani ya chama.

Viongozi hao walimkabidhi kadi ya uanachama na kumtaka kuwa makini sana, hasa katika kuhamasisha vijana wenzake, huku akiwashawishi wasanii wengine kuingia katika siasa na kuongea yale yote yanayostahili kwa haki kwa manufaa ya nchi yao.

"Ukiwa kama kijana mdogo sana na msanii ambaye ni kioo cha jamii, tunataka tuone bidii yako ya kuweza kufichua na kukemea maovu yote, utakayoyaona ndani ya vuguvugu la kisiasa ndani ya nchi yetu, ili jamii nayo iwe na imani na wanasiasa wake," alisema mmoja wa viongozi hao wa CHADEMA.

Aidha, waliwataka wasanii wote nchini ambao wana uchungu wa kweli katika nchi yao, kujiunga kwa wingi katika chama hicho, ili kuweza kufikia na kutimiza lengo la kuwakomboa wananchi walio wengi masikini na sauti za wanyonge kusikika, hasa katika suala zima la kutatua matatizo yao ikiwa ni pamoja na umaskini.

KIKWETE KUFUNGUA SEMINA YA UKIMWI KWA WANAJESHI



RAIS Jakaya Kikwete kesho anatarajia kufungua kongamano la kimataifa kuhusu tatizo la ugonjwa ukimwi katika majeshi litakalofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha AICC mjini hapa.

Kongamano hilo, linatarajia kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 260 kutoka nchi 70 ambapo hadi sasa nchi 60 zimethibitisha kushiriki kongamano hilo ambalo linaelezwa kuwa la kwanza kufanya nchini.

Msemaji wa jeshi hilo, Luteni Kanali Kapambala Mgawe, alisema kongamano hilo litahudhuriwa na makamanda kutoka nchi za bara la Afrika, Asia, Amerika, Carribean, Ulaya na Marekani.

Luteni Kanali Mgawe, alisema mbali na makamanda wa jeshi pia taasisi za kimataifa zinazojihusisha na mapambano dhidi ya ugonjwa huo zitahudhuria.

Kongamano linafanyika kwa ushirikiano kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kushirikiana na jeshi la Marekani kuhusu masuala ya ukimwi kutokana na askari wengi kufariki kwa ugonjwa huo.

Alisema pia Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Tanzania, Jenerali Aden Mwamunyange, pamoja na makamanda wa ngazi ya juu kutoka JWTZ watahudhuria.

Alisema kongamano hilo linafanyika kwa ushirikiano wa pamoja kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Wizara ya Ulinzi ya Marekani kwa lengo la kukabiliana na tatizo la ugonjwa ukimwi ndani majeshi.

POMBE YA KIENYEJI YAUA WATU 7 NA WENGINE 10 WAISHIA KUPOFUKA


Mmoja wa watu waliopoteza macho yao baada ya kunywa Chang'aa akiwa amelazwa hospitali.

Pombe ya kienyeji maarufu nchini Kenya kama Chang'aa imesababisha vifo vya zaidi ya watu 7 na kupofuka macho kwa watu wengine 10.
Zaidi ya watu saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 10 wamebaki vipofu baada ya kunywa pombe maarufu nchini Kenya kwa jina la Chang'aa.

Wakazi wengi wa kitongoji cha Shauri Moyo jijini Nairobi nchini Kenya walikimbizwa hospitali wakiwa hawajiwezi baada ya kunywa Chang'aa (Gongo).

Katika tukio hilo lililotokea jana ijumaa, watu watatu walifariki kwenye eneo la tukio wakati watu watano walipofuka macho hapohapo ya kubwia kilevi hicho cha kienyeji ambacho ni kinyume cha sheria kukutwa nacho.

Mkuu wa kituo cha polisi cha Buruburu alisema kuwa watu wengi zaidi waliwahishwa kwenye hospitali ya Kenyatta baada ya kunywa pombe hiyo.

Baada ya kunywa pombe hiyo, watu walianza kutoa mapovu mdomoni huku wakilalamika maumivu makali ya tumbo.

Hadi kufikia leo watu waliopoteza macho yao wamefikia 10 huku jumla ya watu 7 tayari wameishapoteza maisha yao.