WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Friday, June 18, 2010

Hakuna mgombea binafsi- Mahakama


MAHAKAMA YA RUFAA ya Tanzania jana ilitengeua na kuondoa suala la mgombea binafsi na haitatumika katika uchaguzi tarajio kwa kuwa suala hilo limeonekana kuwa ni la kisiasa zaidi na si la kisheria.
Uamuzi huo uliotolewa jana na jopo la majaji saba na kusomwa na Jaji Mkuu, Agustino Ramadhani, na kusema mgombea binafsi hataruhusiwa katika uchaguzi ujao wa Oktoba mwaka huu.

Akisoma hukumu hiyo, katika ukumbi wa mahakama kuu, Jaji Ramadhani alisema baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili zilizowasilishwa mahakamani, mahakama imegundua kuwa suala la mgombea binafsi ni la kisiasa, hivyo mahakama haina mamlaka ya kulitolea uamuzi.

Alisema uamuzi wa kuwa na mgombea binafsi ni suala la kisiasa linapaswa kuzingatia historia na matakwa ya nchi husika, hivyo mahakama imependekeza suala hilo lirudishwe bungeni ili lijadiliwe kwa kina zaidi na kutolewa uamuzi huko kwa kuwa bunge ndicho chombo kitachokuwa na mamlaka ya kufanya mabadiriko ya katiba za nchi

“Kwa mujibu wa ibara ya 98 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bunge ndilo lenye jukumu la kufanya marekebisho ya vipengele vya katiba au sheria yeyote”

Mara baada ya hukumu hiyo kutolewa mahakamani hapo mmoja wa wadai wa ugombea binafsi, Mchungaji Chisptopher Mtikila alipohojiwa na vyombo vya habari kuhusiana na hukumu hiyo alisema, hakustushwa sana na maamuzi ya jopo hilo la majaji kwa kuwa tayari alikwishaanza kuona dalili ya mahakama kumpendelea Rais Jakaya Kikwete ili arudi madarakani.

Alisema ka kuwa hakuridhika na maamuzi hayo, anakusudia kuwasilisha rufaa mbele ya Mahakama ya Rufaa ya Afrika Mashariki ili litolewe uamuzi ambao anaamini utakuwa wa haki.

Kwa upande wa baadhi ya wananchi waliohudhuria hukumu hiyo wanasheria na wanaharakati mbalimbali walionekana dhahiri kusikitishwa na maamuzi hayo na kusema kuwa mahakama hiyo haijali maslahi ya wananchi na wanyonge wan chi hii.

Walisema maamuzi hayo wamepokea kwa masikitiko makubwa za kusitisha mgombea binafsi na kusema kuwa mahakama imeshindwa kushughulikia mambo ya msingi yalnayohitaji majibu kutoka kwenye chombo hicho na wameona maamuzi hayo ni kama kutowatendea haki wananchi.

Ili Kupinga Obama Kuwa Rais, Alichoma Moto Kanisa la Watu Weusi


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani anakabiliwa na kifungo cha miezi 108 jela baada ya kukiri kulichoma moto kanisa la watu weusi ili kupinga Barack Obama kuwa rais mweusi wa Marekani.
Benjamin Haskell, 23, wa Massachusetts nchini Marekani amekiri kosa lake la kulichoma moto kanisa la Wamarekani weusi ili kupinga kuchaguliwa kwa Barack Obama kuwa rais wa kwanza mweusi wa Marekani.

Benjamin alikiri jana kulichoma moto kanisa la Macedonia Church of God in Christ mnamo novemba 5 mwaka 2008, ikiwa ni ndani ya masaa machache baada ya Obama kuchaguliwa kuwa rais.

Benjamin alilimwagia petroli kanisa hilo kabla ya kulipiga kiberiti na kuliteketeza.

"Leo tunatoa ujumbe kuwa watu wanaofanya uhalifu kwa sababu za chuki, watachunguzwa na baadae ya kushtakiwa", alisema Carmen Ortiz mwanasheria mkuu wa Massachusetts.

Benjamin huenda akahukumiwa kwenda jela miezi 108 (miaka 9) baada ya kukiri kosa lake la kuhatarisha maisha ya waumini 300 wa kanisa hilo na kuliharibu jengo la kidini kwasababu ya chuki zake ubaguzi wa rangi.

Mke Amuua Mume Kwasababu ya Kombe la Dunia


Kombe la dunia linaloendelea nchini Afrika Kusini limekuwa sababu ya kifo cha mwanaume mmoja nchini humo ambaye alifariki baada ya kupigwa na mkewe na watoto wake wakati alipolazimisha kuangalia mechi kwenye TV wakati mkewe na watoto wake walitaka kuangalia nyimbo za dini.
David Makoeya mwenye umri wa miaka 61 hakutaka kuikosa mechi ya jumapili iliyopita kati ya Ujerumani na Australia.

Mke wake na watoto wake wao walitaka kuangalia programu ya nyimbo za dini za kikristo kwenye luninga.

Polisi wanasema kuwa Makoeya alikuwa akigombania remote control na familia yake ili aweze kuangalia mechi ya kombe la dunia.

Familia yake walikataa kubadilisha channel ya mambo ya dini waliyokuwa wakiiangalia na hapo ndipo mzozo ulipoanzia.

"Alisema, Hapana nataka kuangalia mpira", msemaji wa polisi Mothemane Malefo alisema.

Huku akiwa na hasira, Makoeya alinyanyuka na kuelekea kwenye TV ili aweze kubadilisha channel lakini hakufika mbali kwani mkewe na watoto wake walianza kumshushia kipigo.

Mke wa Makoeya mwenye umri wa miaka 68, Francina, akishirikiana na mtoto wake wa kiume Collin mwenye umri wa miaka 36 na binti yake Lebogang mwenye umri wa miaka 23 walimshushia kipigo cha nguvu baba yao.

"Inaonekana walikipigiza kichwa chake kwenye ukuta, walipiga simu polisi baada ya kumjeruhi vibaya sana... wakati polisi wanafika eneo la tukio, Makoeya alikuwa ameishafariki", alisema Malefo.

Mke wa Makoeya na wanae ambao wanaishi kwenye kijiji cha Makweya, walitiwa mbaroni jumapili usiku.

Binti yake aliachiwa kwa dhamana ya dola 200 wakati mkewe na mtoto wake wa kiume wanaendelea kunyea debe rumande.

Ndugu wa familia hiyo wamesikitishwa na kifo cha Makoeya wakisema kuwa Makoeya hakuwa mtu mwenye vurugu alikuwa mtulivu na mwenye furaha kwa familia yake.

VIDEO - Wivu Wapelekea Amchome Moto Mpenzi Wake


Kutokana na wivu mwanamke mmoja nchini Marekani alimchoma moto mpenzi wake na kisha kujichoma moto na yeye mwenyewe na kutokana na moto huo nyumba ilishika moto na kupelekea vifo vya watu wengine watatu.
Agnes Bermudez, 50, anatuhumiwa kumuua mpenzi wake William Salazar, 32, katika tukio la kutisha lililotokea siku ya akina baba duniani mwaka 2008.

Agnes ambaye hivi sasa kesi yake inaendelea mahakamani, alimchoma moto mpenzi wake huyo na kisha yeye mwenyewe alijipiga kibiriti.

Agnes hakufariki kutokana na moto aliouanzisha lakini aliungua vibaya sura yake kiasi cha kumfanya asitambulike.

Sababu ya Agnes kumchoma moto mpenzi wake ni wivu wa kimapenzi. Agnes alimshutumu Salazar kuwa anatembea na mwanamke mwingine nje.

Video ya tukio hilo imetolewa mahakamani kama ushahidi wa tukio hilo la kusikitisha.

Video inamuonyesha Agnes na Salazar wakitoka nje ya nyumba yao wakikimbilia kwenye duka lililopo chini ya jengo lao.

Salazar anaonekana akikimbia kuingia ndani ya duka akitafuta maji wakati Agnes alilala chini mbele ya duka hilo huku akiungua na moto.

Wasamaria wema walifanikiwa kuwamwagia maji na kuokoa maisha yao hata hivyo Salazar alifariki siku nne baadae hospitalini.

Moto ulioanzishwa na Agnes ulishika pia nyumba zingine zilizopo kwenye jengo hilo na kupelekea vifo vya watu watatu.

Chini ni VIDEO ya tukio hilo iliyoonyeshwa mahakamani.

Tuesday, June 1, 2010

Wahindi Walalamikia Ukubwa wa Kondomu


Utafiti uliofanyika nchini India umeonyesha kuwa wanaume wengi nchini India hawafurahishwi na ukubwa wa kondomu unaotambulika duniani kwakuwa kondomu hizo ni kubwa sana kulinganisha na ukubwa wa nyeti zao.
Utafiti huo uliowashirikisha wanaume 1,000 wa nchini India ulionyesha kuwa kondomu zenye ukubwa unaotambulika kimataifa huwapwaya wanaume wengi wa nchini India.

Utafiti huo uliweka wazi kuwa zaidi ya nusu ya wanaume walioshiriki utafiti huo walikuwa na uume ambao ulikuwa ni mfupi kulinganisha na ukubwa wa kondomu.

Utafiti huo uliofanyika kwa miaka miwili uliweka wazi kuwa asilimia 60 ya wanaume nchini India wana uume wenye urefu kati ya sentimeta tatu hadi tano pungufu ya ukubwa wa kondomu unaotambulika duniani.

Matokeo ya utafiti huu yamepelekea makampuni ya kutengeneza kondomu nchini India yatakiwe kutengeneza kondomu zenye ukubwa tofauti tofauti.

Matokeo ya utafiti huu yametiliwa mkazo kwakuwa India ndiyo nchini inayoongoza duniani kwa idadi kubwa ya watu walioathirika na virusi vya Ukimwi.

KIJANA AGONGWA NA TRENI JIJINI DAR


Mtu mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja amegongwa na treni katika eneo la Keko darajani jijini Dar es Salaam.
Mtu mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja amegongwa na treni katika eneo la Keko darajani jijini Dar es Salaam, kijana huyo inasadikika alikuwa akiishi chini ya daraja hilo ambapo kuna njia ya reli .

Kwa kuwa reli hiyo ilikuwa haitumiki kwa muda mwingi kijana huyo aliamua kufanya sehemu ya kulala leo serikali ya Tanzania ilitangaza kuwa safari ya treni ya kuelekea Kigoma , mwanza, mpanda itaanza baada ya matengenezo ya daraja lililokuwa limeharibika kutengenezwa,

Bila kujua kama kuna mtu tayari kichwa cha treni kilipita katika njia yake huku jamaa akiwa amepitiwa na usingizi katika reli na kukanyagwa hadi kufa.

Hadi tunakwenda mitaamboni hakuna taarifa za uhakika za kijana huyo ambaye amegongwa majira ya asubuhi leo.

Watanzania Kuzilipa Gharama za Kuwaleta Wabrazili


Washabiki wa soka Tanzania ndio wataolazimika kujipinda ili kuzilipa dola milioni 2.5 ambazo Brazili imelipwa ili kuileta timu yake Tanzania.
Shirikisho la soka Tanzania, TFF limepanga viingilio vikubwa kwenye mechi kati ya Brazili na Tanzania itakayofanyika jumatatu ijayo jijini Dar es Salaam.

Viingilio vimekuwa vikubwa kuliko kawaida ili kulipia gharama za kuwaleta mastaa wa Brazili Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vingi vya habari, Tanzania imewalipa Brazili dola milioni 2.5 ingawa TFF imekataa kusema imewalipa Brazili dola milioni ngapi.

TFF ilisema kuwa kuwaleta Brazili nchini Tanzania ni gharama sana hivyo Watanzania wajiandae kukaza mikanda kulipa gharama hizo.

TFF inaamini kuwa mapato ya magetini yatatosha kuzilipa gharama za kuwaleta Brazili Tanzania.

Viingilio katika mechi hiyo itakayochezwa juni 7 vimepangwa kuanzia Tsh. 30,000 hadi Tsh. 200,000.

Majukwaa ya VIP tiketi zinaanzia laki moja hadi laki mbili ambapo taarifa za TFF zinasema kuwa tiketi za laki mbili zimeishanunuliwa zote.

Majukwaa yaliyobakia tiketi zinaanzia Tsh. 30,000 hadi Tsh. 80,000.

BAJETI YA TANZANIA MWAKA UJAO NI TRILIONI 11


SERIKALI ya Tanzania imepanga kutumia Shilingi trilioni 11.1 katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2010/11.
Bajeti hiyo imeongezeka shilingi trillion 1.6 ukilinganisha na ya mwaka jana wa fedha.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Fedha na Uchumi , Mustapha Mkulo, alisema kati ya fedha hizo, zinazotarajiwa kukusanywa ni Sh trilioni 6 ambazo ni za mapato ya ndani na Sh trilioni 2.8 misaada na mikopo kutoka kwa wahisani mbalimbali.

Alisema pia kati ya fedha hizo, Sh trilioni 1.1 ni mikopo ya ndani, Sh bilioni 983.7 mikopo ya masharti ya kibiashara na Sh bilioni 30 ni mapato kutokana na ubinafsishaji.

Mkulo alisema katika bajeti hiyo, kilimo, huduma za jamii kama elimu, afya na maji, ardhi na umwagiliaji, miundombinu ambayo ni reli, bandari, viwanja vya ndege na nishati ndio vitapewa vipaumbele.

Bajeti hiyo inatarajiwa kutumia Sh trilioni 7.8 kwa matumizi ya kawaida na Sh trilioni 3.2 kwa matumizi ya maendeleo.

Hata hivyo, alisema Serikali itaendelea kutumia mikopo nafuu na kuanzia mwaka ujao itatumia mikopo ya kibiashara kwa ajili ya kugharimia bajeti yake.

Aidha, alisema kwa mwaka wa fedha 2010/11 Serikali inatarajia kukusanya mapato ya ndani yasiyopungua Sh trilioni sita, sawa na asilimia 17.3 ya pato la Taifa ikilinganishwa na mapato ya asilimia 16.4 ya pato la Taifa ya mwaka jana.

Pia alisema Serikali inatarajia kukusanya Sh bilioni 1.7 kutoka kwenye vyanzo vya halmashauri ambapo pia imelenga kuendeleza mfumo wa makusanyo ya mapato ya ndani, kuimarisha usimamizi na udhibiti wa makusanyo, kuchukua hatua za kupunguza misamaha ya kodi, kutenga fedha kwa ajili utekelezaji wa kaulimbiu ya Kilimo Kwanza.

AMPENDA DADA YAKE, AKAAMUA KUMUONA

Mwanaume mmoja nchini Ireland amejikuta akimzalisha dada yake bila kutarajia baada ya kuangukia kwenye mapenzi bila kujua kuwa mwanamke huyo ni dada yake. Ameamua kufunga naye ndoa ili waweze kumtunza mtoto aliyezaa naye.
Mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la Mark wa nchini Ireland alijikuta akizaa na dada yake wa baba mmoja mama tofauti, baada ya kuanza naye uhusiano bila kufahamu kuwa ni dada yake.

Wazazi wa Mark waliachana wakati Mark akiwa mdogo sana ambapo kwa jinsi ndoa hiyo ilivyovunjika kwa mgogoro mkubwa mahakamani, Mark alipewa jina tofauti la baba na mahakama iliamuru mtoto huyo asiambiwe baba yake anaitwa nani.

Kasheshe liliibuka baada ya Mark kukutana na mwanamke disco katika mji tofauti na anaoishi. Mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Maura naye alienda kwenye disco hilo akitoka kwenye mji mwingine tofauti.

Mark alianza uhusiano wa kimapenzi na Maura wakati huo. Miaka miwili baadae Maura alipopata ujauzito ndipo wawili hao walipoamua kuishi pamoja.

Baada ya Maura kujifungua, Mark aliamua kumtambulisha Maura kwa mama yake na ndipo ukweli ulipofichuka.

Mama yake Mark alimuuliza Maura baba yake anaitwa nani, alipolitaja jina lake ndipo mama huyo alipomwambia Mark "Mwanangu huyo ni dada yako".

Matokeo ya vipimo vya DNA yaliyotolewa mwezi uliopita yalithibitisha kuwa Mark na Maura ni mtu na dada yake.

Hata baada kugundua kuwa uhusiano wao ni haramu, wawili hao wameamua kuuendeleza na wamepanga kuzaa watoto wengi zaidi.

"Najua watu watatufikiria vibaya, kama tusingekuwa na mtoto tungeweza kufikiria kusitisha uhusiano wetu lakini kwakuwa tuna mtoto mmoja, tutafunga ndoa tuzae watoto wengi zaidi", alisema Mark.

Mark na Maura wanatoa lawama zao kwa mfumo wa sheria ambao ulizuia Mark kumjua baba yake.

Wamepanga kumfungulia kesi ya fidia jaji aliyeamuru Mark asijulishwe baba yake.