WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Thursday, April 22, 2010

DENI LA TANZANIA LAZIDI KUONGEZEKA


DENI la Taifa limeongezeka maradufu na kufikia shilingi trillion 7.6

Hayo yaliwekwa wazi na katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Ludovick Otouh, alipokuwa akiwajulisha waandishi wahabari.

Amesema deni la taifa limeongezeka kwa kasi kutoka kiasi cha sh trilioni 6.4 mwaka 2007/08 hadi kufikia shilingi trilioni 7.6 katikka mwaka wa fedha wa 2008/09
.
Amesema kuwa deni hilo limeongezeka kwa tofauti ya shilingi trillion 1.1 kutoka lile la mwaka wa fedha wa jana.

Amesema kutokana na hali hiyo, kuna umuhumu wa serikali kusimamia vizuri makusanyo na matumizi ya fedha zake.

Amesema deni hilo limeongezeka hivyo kutokana na serikali kujiingiza katika bajeti kubwa kuliko uwezo wenyewe.

Vilevile amesema serikali imeshindwa kudhibiti matumizi ya juu, kutokuwa makini na mikataba mbalimbali, pamoja na kuzamini mambo mbalimbali kinyume na uwezo halisi.


Hivyo amesema katika taarifa zilizowasilishwa na maofisa masuuli, zilieleza bayana kuwa wizara, idara, walaka na sekretarieti za mikoa hazikuzingatia kikamilifu sheria ya manunuzi ya umma namba 21 ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2005 ambapo jumla ya sh bilioni 12.8 zilionyesha kasoro mbalimbali za ukiukwaji wa taratibu za manunuzi.

Pia alisema katik ukusanyaji wa mapato matokeo ya ukaguzi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), unaonyesha kuwa misamaha mingi iliyotolewa kwa taasisi mbalimbali na watu binafsi yenye thamani ya sh bilioni 752.3 imerudisha nyuma mapato ya serikali.

MSICHANA ABAKWA NA BOSS WAKE

MSICHANA mmoja jina lake halitaweza kuchapishwa kwa leo amebakwa na mwajiri wake usiku wa kuamkia leo
Msichana huyo alifanyawa unyama huo usiku wa kuamikia leo, huko maeneo ya Mbezi anapofanyia kazi yake hiyo aliyodumu nayo kwa muda wa mwaka mmjoa na nusu sasa.

Msichana huyo alionekana akilia na mwandishi wa habari hii huko Kimara, majira ya saa kumi na mbili asubuhi, alipokuja kuomba ushauri kwa ndugu yake wa kutoka kijiji kimoja huko Iringa.

Ndugu yake huyo ambaye ni jirani na mwandishi wa habari hii alidai mdogo wake huyo aliweza kulazimishwa afanye mapenzi na bosi wake huyo ambaye ni mwajiriwa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania na alifanikiwa kumbaka pasipo hiari yake

Alidai msichana huyo kuwa mwajiri wake huyo alimwingilia chumbani majira ya sa saba usiku, na kumtaka afanye nae mapenzi na alishindwa kutoroka kwa kuwa alimzidi nguvu kwa hali ya kuwa yeye ni mwanaume.

Alidai aliweza kuingia katika chumba hicho kwa kuwa chumba hicho hakikumaliza mlango kwani walihamia hivi karibuni bila nyumba hiyo kumalizika ipasavyo.

Alidai mara baada ya kuingia chumbani humo alimuamsha msichana huyo na kushangaa kulikuwa na tatizo gani punde alimuamuru afanya matendo anayoyahitaji na kukataa huku akilia na baba huyo kumuahidi kuwa pindi atakapokubali atamsomesha na kumuhamisha hapo nyumbani.

Mbali na ahadi hiyo binti huyo aliendaelea kugoma huku akilia na kumkatalia ndipo baba huyo alimlazimisha na kumbaka.

Alidai kuwa baba huyo alifanikiwa kumbaka kwa kuwa mke wake alisafiri kwenda kwao mkoani Mbeya kwa mama yake alikwenda huko kwa kuwa alikwenda kujifungua kwao ili akapate uangalizi wa karibu.

Alidai mke wake alisafiri mwanzoni mwa mwezi huu na alimuacha mdogo wake wa waishi nae na kwa jana mdogo wake huyo hakurudi nyumbani na ndiyo baba huyo alitumia fursa hiyo kufanikisha adhama yake.

Hata hivyo kwa maelezo ya haraka haraka alimwambia dada yake huyo anaogopa kurudi tena na atarudi endapo bosi wake kike atakaporudi kwa kuwa aliihitaji kazi yake kwani ndiyo ilikuwa ikimsaidia kujikimu matatizo yake madogomadogo.

JESHI LA POLISI LACHAPISHA KITABU CHA MUONGONZO KWA WAPIGA KURA


JESHI la Polisi Nchini, limetoa kitabu maalum kinachofafanua na kumuongoza mwananchi mchakato mzima wa uchaguzi kwa lengo la kuwezesha uchaguzi, huo kufanyika kwa utulivu na amani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam , Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema alisema kitabu cha Haki na wajibu wa Mpigakura, kimebeba ujumbe mzito unaohusu kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.


Mwema alisema ni haki ya kila Mtanzania aliyetimiza vigezo wa kupiga kura kitabu hicho kitamuongoza katika kuhakikisha kuwa sheria za nchi hazikiukwi kabla na baada ya uchaguzi

Alisema kitabu hicho kinalenga kuufanya uchaguzi huo uwe wa haki katika kuchagua viongozi na kutekeleza wajibu wa usalama, amani na utulivu vinadumu katika jamii.

Alisema kitabu hicho kinaelezea umuhimu wa kujiandikisha kupiga kura, uteuzi wa wagombea katika vyama vya siasa, kampeni za wagombea na vyama vyao na matangazo yatakayowekwa na vyama vya siasa na wagombea.

Mambo mengine ni wajibu na umuhimu wa polisi katika mchakato wa uchaguzi, haki na wajibu wa mpigakura, siku ya uchaguzi, jinsi ya kupiga kura, kusubiri matokeo, kupokea matokeo na uvunjaji wa sheria wakati wa uchaguzi.


Pia alisema “askari polisi watakaovujisha siri za taarifa mbalimbali zinazohusu mitaa katika uchaguzi watachukuliwa hatua kali, pia na mwananchi yeyote atakayehatarisha hatari ama kugundulika kuvunja amani sheria itafata mkondo wake” alisema.