WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Sunday, April 25, 2010

MAITI ZA WATU KUUZWA KWENYE SUPERMAKET UJERUMANI



Yule daktari bingwa wa mifupa wa Ujerumani ambaye mwaka jana aliandaa maonyesho ya maiti zikifanya mapenzi, ameamua kufungua supermarket ambapo atauza vipande vya miili ya watu.
Baada ya kuandaa maonyesho mwaka jana akizionyesha maiti katika hali mbalimbali za kujamiiana, Dr. Gunther von Hagens wa nchini Ujerumani ameamua kuwauzia watu maiti za watu alizo nazo.

Hagens anafungua supermarket ya maiti za binadamu mjini Guben, Brandenburg, ambayo imepangwa kufunguliwa rasmi mei 28 mwaka huu.

Fuvu la binadamu likiwa limening'inizwa kwenye chuma litauzwa euro 1,200.

Hagens pia ana mpango wa kufungua tovuti ya duka hilo ili aweze pia kufanya mauzo online.

Hagens ambaye anajulikana zaidi kama "Dr Death" (Dokta Kifo), ni mtaalamu maarufu wa elimu ya mwili na viungo vya binadamu na wanyama (Anatomy).

Hagens anatumia njia aliyoigundua yeye mwenyewe inayojulikana kitaalamu kama "plastination" ambapo maiti hutolewa ngozi yote na kisha majimaji yote kwenye maiti kukaushwa.

Hagens hutumia plastiki zilizotengenezwa kwa madini ya silicon kuziweka maiti hizo katika maumbile mbali mbali kuonyesha maisha ya kila siku ya mwanadamu.

Hagens alisema kuwa maiti anazozitumia kwenye kazi zake ni za watu waliojitolea miili yao kwake kabla hawajafariki. Hagens aliongeza zaidi kuwa yeye mwenyewe ameishajitolea maiti yake itumike namna hiyo akishafariki.

Mwaka jana Hagens aliingia kwenye mzozo mkubwa wakati alipofungua maonyesho mjini Berlin akiyaweka maumbile ya maiti katika staili mbalimbali za kujamiiana.

Miaka miwili iliyopita Hagens alijaribu kufungua duka la kuuza vipande vya miili ya watu lakini alilazimika kuahirisha mpango wake kutokana na upinzani mkubwa toka kwa makanisa na watu mbalimbali.

Safari hii Hagens amesema ameweka nia ya kweli ya kufungua supermarket hiyo ya maiti za binadamu na amesema hatauahirisha mpango wake kwa sababu yoyote ile.

RAIS WA AFRIKA KUSINI JACOB ZUMA APIMA UKIMWI NA KUWEKA MAJIBU WAPI


Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ambaye mwaka 2006 alifanya mapenzi na mwanamke mwenye ukimwi bila ya kutumia kinga na kuzusha uvumi kuwa na yeye ni muathirika, amepima ukimwi na kuweka majibu yake hadharani.
Rais Zuma amewathibitishia watu kuwe yupo fiti na wala hajaathirika kutokana na vipimo vya HIV alivyofanya mwezi huu ambavyo majibu yake yamewekwa hadharani wananchi wayaone.

"Baada ya kuliangalia suala hili kwa umakini nimeamua kuweka wazi majibu yangu ya vipimo vya HIV .. ili kusisitiza uwazi miongoni mwa watu", alisema Zuma.

Rais Zuma alipima 'Ngoma' aprili nne mwaka huu na majibu yalikuwa ni NEGATIVE. Alisema kuwa kabla ya hapo alishafanya vipimo mara tatu na majibu yalikuwa pia NEGATIVE.

Rais Zuma alifanya vipimo hivyo katika kuiunga mkono kampeni ya kuwahimiza watu wapime ukimwi na wazitambulishe hali zao kama wameathirika.

Kampeni hiyo ina malengo ya kuwapima 'ngoma' jumla ya watu milioni 15 ifikapo mwishoni mwa mwezi juni mwakani.

Mwaka 2006, Rais Zuma alifikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumbaka mwanamke mwenye ukimwi.

Hata hivyo rais Zuma alikanusha kumbaka mwanamke huyo na kusema kuwa alifanya mapenzi na mwanamke huyo kwa hiari yake mwenyewe.

Rais Zuma alikiri pia wakati huo kuwa alifanya mapenzi na mwanamke huyo bila kutumia kinga ingawa alikuwa akijua fika kuwa mwanamke huyo ni muathirika.

Rais Zuma alisema kuwa siku zote hutumia kondomu lakini siku hiyo alikuwa hana kondomu na mwanamke huyo ndiye aliyeanza uchokozi uliopandisha mashetani yake ya ngono.

Kipindi hicho, Rais Zuma aliamsha hasira za wanaharakati wa kupambana na maambukizi ya ukimwi alipoiambia mahakama kuwa alienda kuoga punde baada ya kumaliza kufanya mapenzi na mwanamke aliyeathirika ili kujiepusha na maambukizi ya gonjwa hilo.