WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, May 10, 2010

WATU WATANO WAFARIKI BAADA YA LORI KUTEKETEA KWA MOTO



WATU watano wamefariki dunia baada ya malori mawili yaliyokuwa yamebeba mafuta na betri kulipuka baada ya kugongana huko eneo la Vigwaza Kibaoni mkoni Pwani.
Ajali hiyo mbaya iliyosabaabisha mafgari matatu kuwaka moto na kutekekteza watu hao ilitokea jana katika barabara ya Morogoro, majira ya saa 8 usiku.

Katika eneo la tukio ilidaiwa lori la mafuta lililigonga kwa nyuma gari jingine lililokuwa limeegeshwa pembeni ya barabara kwa ajili ya matengenezo na kusababisha moto mkubwa kuwaka hapo.

Kamanda wa polisi mkoani Pwani, Absaloom Mwakyoma alisema ajali hiyo ilihusisha malori mawili aina ya Scania, moja ambalo lilikuwa na trela na ambalo lilibeba mafuta liligonga kwa nyuma lori ambalo lilikuwa limesheheni mzigo wa betri za redio mali ya Said Daniel, mfanyabishara wa Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Alisema wakati moto huo unalipuka chini ya lori alikuwepo utingo wa gari ambalo lilikuwa katika matengenezo Omary Mumbi, mkazi wa Buguruni, alikuwepo dereva wa gari hilo Adam Amulike[ 35], mkazi wa Temeke na dereva mwingine aliyefika kusaidia kutengeneza gari hilo na wote hao waliteketea kwa moto huo

Pia katika ajali hiyo ulimuunguza dereva na utingo wa lori lililosababisha ajali, ambao majina yao hayakuweza kupatikana wote waliteketea kabisa wakiwa ndani ya gari lao.

Alisema wakati moto huo unaendelea kuwaka magari yalisimama na kutoendela na safari lakini lori jingine aina ya Scania lililokuwa na trela lenye tanki ambalo halikuwa na mafuta lilifanya ubinshi kujaribu kupita eneo hilo na baadae kushindwa kuendela na safari baada ya moto kushika kwenye gari hilo na matairi matano ya upande wa kulia kuungua.

MWANAMKE ALIYE WAUA WATOTO WAKE AFIKISHWA MAHAKAMANI

MWANAMKE Benedicto Thadei [44] anayedaiwa kuwaua watoto wake watatu kwa kutumia shoka jana alifikishwa katika mahakama ya mjini Moshi kujibu mashitaka matatu ya mauaji ya kukusudia.
Mwanamke huyo alifikishwa katika mahakama hiyo akiwa chini ya ulinzi polisi na kusomewa mashitaka yake mbele ya hakimu Mfawidhi Simon Kobero wa Mkoa wa Kilimanjaro.


Kwa upande wa mashitaka uliongozwa na Wakili wa serikali, Abdalah Chavulla,alidai kuwa Aprili 29 mwaka huu, majira ya saa 1:30 asubuhi, mshitakiwa aliwaua watoto wake Rose Thadei [12] Noel Thadei[5] na Anthony Thadei mwenye umri wa miaka miwili na nusu na .


Alisai kosa hilo ni kinyumecha sheria cha kifungu namba 196 cha kanuni ya adhabu ambacho kinataja adhabu ni kunyongwa hadi kufa iwapo mshtakiwa atapatikana na hatia.



Hata hivyo mshitakiwa huyo hakutakiwa kujibu chochote mahakamani hapo kama ni kweli alihusika ama la, kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza mashitaka ya mauaji na kutakiwa kwenda kujibu mashitaka hayo Mahakama Kuu pindi utaratibu wa kimahakama utakapokamilika.


Ilidaiwa na Chavula kuwa wakati mama huyo anafikishwa mahakmani hapo mtoto wake aliyemjeruhi Paschal Thadei[ 9], ambaye ni mwanafunzi wa darasa la pili alikuwa amelazwa chumba cha wagonjwa mahuti katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC na tayari madaktari wea hopspitali hiyo walilazika kumfanyia upasuaji wa kichwa kutokana na majeraha mabaya aliyoyapata wakati wa tukio.

Kesi hiyo imepangwa tena kurudishwa mahakamani hapo Mei 19, mwaka huu, kwa kutajwa.

VIDEO YA GAIDI WA NIGERIA FAROUK ABDULMUTALLAN AKIFANYA MAZOEZI YATOLEWA


Video imetolewa ikimuonyesha mwanafunzi wa Nigeria anayetuhumiwa kujaribu kuilipua ndege ya Marekani siku ya krismasi, akifanya mazoezi na wenzake kwenye kambi ya Al-Qaeda nchini Yemen.
Video hiyo inamuonyesha Umar Farouk Abdulmutallab na wanaume wengine wakifanya mazoezi ya kulenga shabaha kwenye kambi ya kundi la Al-Qaeda nchini Yemen linalojulikana kama "Agap".

Umar anakabiliwa na mashtaka ya kujaribu kuiangusha ndege ya Marekani kwa kutumia mabomu aliyoyaficha kwenye chupi yake.

Jaribio lake lilifeli na Umar alibaki na majeraha ya kuungua na moto kwenye sehemu zake za siri.

Alikanusha madai ya kesi zote alizofunguliwa lakini shirika la ujasusi la Marekani limesema kuwa anaonyesha ushirikiano kwa maafisa wa upelelezi.

Umar mwenye umri wa miaka 23 aliwaambia wapelelezi wa Marekani kuwa alipewa mafunzo nchini Yemen. Alipewa vifaa vyenye uwezo wa kusababisha mlipuko mkubwa na kuambiwa nini anatakiwa afanye.

Umar aliwaonya Wamarekani kuwa mamia ya vijana kama yeye wapo wengi nchini Yemen wakipatiwa mafunzo na wako tayari kufanya mashambulizi wakati wowote.

Katika video iliyotolewa, Umar anaonekana akiwa ameshika bunduki na mwishoni mwa video anaonekana akitoa ujumbe katika lugha ya kiarabu.

Haijajulikana ni lini video hii ilitengenezwa na kama ni feki au la.

Chini VIDEO hiyo.

AMJERUHI MMEWE KISA HARIDHISHWI NA HUDUMA KITANDANI


Mwanamke wa nchini Marekani ambaye hakuridhishwa na pafomansi ya mumewe kitandani anashikiliwa na polisi kwa kumjeruhi mumewe kwa mkasi.
Michelle Thomas, 26, alikamatwa jumanne wiki iliyopita baada ya polisi kuitwa kwenye nyumba yao kwenye majira ya saa saba usiku.

Tukio hilo lilitokea Texas, Marekani wakati Michelle alipokasirishwa na uwezo mdogo ulioonyeshwa na mumewe kitandani siku hiyo.

Mume wa Michelle aliwaambia polisi kuwa Michelle alipatwa na hasira baada ya gemu la malavidavi kuisha bila ya Michelle kuridhishwa kimapenzi.

Alisema kuwa Michelle alichukua mkasi na kuutumia kumkatakata kwenye sehemu mbalimbali za mwili wake.

Polisi walimkuta mume wa Michelle akiwa na majeraha makubwa kifuani, mkononi na miguuni.

Michelle amefunguliwa mashtaka ya kudhuru mwili kwa kutumia silaha hatari ingawa mumewe hakutaka kufungua kesi dhidi yake, liliripoti gazeti la Lufkin Daily News.

Michelle huenda akatupwa jela miaka 20 iwapo atapatikana na hatia.