WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Wednesday, March 31, 2010

TWO FOREIGN TOURISTS ROBBED AT GUN POINT IN ARUSHA NATIONAL PARK


Two foreign tourists have been robbed of various items worth several million dollars at gunpoint in Arusha National Park, raising serious doubts about the security situation in the game sanctuary.

In the rare episode, three heavily armed gangsters posing as game wardens reportedly ambushed the tourists in the park located nearly 35kms north-east of the northern safari capital of Arusha.

The thugs managed to put the tourists under siege and ransacked them before walking away with hard cash, tourist bags, digital cameras and other valuable items.

Arusha regional police commander Basilio Matei confirmed the incident.

“My men, in collaboration with Tanzania National Parks Authority game wardens, are currently working extra time hunting for the armed hooligans,” Matei said.

Jeremiah Maka, a professional tour guide with Big Expeditions who was escorting the tourists, said the incident took place at Ngurdoto crater within the national park late last week.

Maka named the victims as Christina Lazano from Spain and Paulina Elago from Namibia.

According to him, the two tourists were resolved to visit the nearest park in Arusha after taking time off from participating in an international conference.

“This is a strange incident to happen within the maximum security national park. It is unbelievable indeed, no one can buy the tale,” Maka explained.

For his part, Big Expeditions executive director Nicholaus Minja made a passionate call to the police and TANAPA to apprehend the culprits behind the shameful incident.

"The latest robbery incident will tarnish the good image of the country, but I hope the police, in collaboration with TANAPA, will do something about this,” Minja stressed.

SERIKALI YAMNG'ANG'ANIA LIYUMBA



UPANDE wa jamhuri katika kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 221 inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu, Amatus Liyumba umeiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imuone mshitakiwa ana kesi ya kujibu.

Ombi hilo liliwasilishwa mahakamani hapo jana saa tisa alasiri kwa njia ya maandishi yaliyochukua kurasa 29 na Mkuu wa Kitengo cha Sheria cha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Ben Lincoln na wakili wa serikali Prosper Mwangamila.

Kuwasilishwa kwa ombi hilo kulitokana na amri iliyotolewa Machi 15, mwaka huu, na kiongozi wa jopo la mahakimu wakazi wanaosikiliza kesi hiyo, Edson Mkasimongwa ambaye alizitaka pande zote kuwasilisha maombi kwa njia ya maandishi.

Kwa mujibu wa nakala ya ombi hilo ambalo gazeti hili lina nakala yake, upande wa jamhuri umedai kwa mujibu wa vielelezo 12 walivyotoa mahakamani na mashahidi wanane waliowaleta, wameweza kutoa ushahidi thabiti dhidi ya mshitakiwa ambao utaishawishi mahakama hiyo imuone ana kesi ya kujibu na kuongeza kuwa wanaiomba mahakama hiyo itupilie mbali ombi la utetezi lililotaka mahakama imuone mshitakiwa huyo hana kesi ya kujibu kwa sababu halina msingi.

Wakichambua shitaka la matumuzi mabaya ya ofisi ya umma kinyume na kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, jamhuri imejigamba kuwa imeweza kuthibitsha shitaka hilo kwa sababu mshitakiwa huyo ni kweli alikuwa mtumishi wa serikali toka mwaka 1971-2007 na kwamba alikuwa na cheo wakati wa mradi wa 10 Milambo Office Extention na alikuwa na jukumu la kuusimamia na kwamba kwa mujibu wa shahidi 1, 2, 3, 5, 6 na 8 waliithibitishia mahakama kuwa mradi huo ulikuwa ukiratibiwa na ofisi aliyokuwa akiongoza Liyumba ya Utumishi na Utawala.

Wakichambua shitaka la pili la kuisababishia serikali hasara, upande wa jamhuri umejigamba kuwa umeweza kuthibitisha shitaka hilo kwa madai kuwa hoja iliyodaiwa na upande wa utetezi kuwa haiwezekani kutambua hasara iliyopatikana bila ripoti ya mwisho ya mradi kukamilika si ya msingi kwani hata ikitolewa haiwezi kubadili makadirio ya gharama za mradi.

Kuhusu hoja ya upande wa utetezi iliyodai upande wa mashitaka umeshindwa kuthibisha kwamba mshitakiwa huyo alitenda makosa hayo akiwa na nia ovu, umedai kuwa katika kesi za jinai hoja hiyo haina msingi.

Machi 22 mwaka huu, mawakili wa utetezi Majura Magafu, Onesmo Kyauke, Hudson Ndusyepo na Jaji Mstaafu Hillary Mkate waliwasilisha hoja zao wakitaka mahakama hiyo imuachilie huru mshitakiwa huyo kwa sababu upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha kesi yao.

Kwa sababu tayari pande zote mbili katika kesi hiyo zimekwisha wasilisha hoja zao, kiongozi wa jopo la mahakimu wakazi, Mkasimongwa, Lameck Mlacha na Benedict Mwingwa, Aprili 9 mwaka huu, wanatarajiwa kutoa uamuzi wao kuhusiana na hoja hizo.

MAJAMBAZI 37 YAKAMATWA DAR



JESHI la polisi nchini lemefanikiwea kukamatwa majambazi 37 sugu katika operesheni inayoendelea nchi nzima.

Majambazi hayo yamekamatwa katika siku tofauti tofauti katika msako mkali wa jeshi hilo kuweasaka majambazi hayo yanayofanya uhalifu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleimani Kova amesema wamefanikiwa kuwakamata watu hao kwa mitego ambayo ilitegwa na jeshi hilo katika maeneo tofauti tofauti.

Amesema majambazi hayo kati yao 15 yalikamatwa yakiwa yamevaa mabaibui na madira ili kufanikisha uhalifu wao katika maeneo tofauti ya jiji.

Amesema pia waliweza kukamata bunduki aina ya SMG mopja, Short gun moja, bastola tatu pamoja na risasi kadha walizokutwa nazo wahalifu hao.

MAMA SALMA KIWEKE ANUSURIKA AJALI MBAYA




MKE wa Rais Mama Salma Kikwete anusurika kifo kwa ajali mbaya baada ya msafara wake kuingia doa kwa kuvamiwa na lori na kugonga magari matatu ya msafara huo.

Ajali hiyo ilitokea jana wilayani Rorya mkoani Mara wakati Mama Salma akiwa ziarani mkoani humo.

Kamdanda wea Polisi Tarime, Bw. Constantine Masawe alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na alisema lori hilo lilisimamishwa na askari wa barabarani lisimame ili kupisha msafara huo na kukaidi na kuingia barabarani na kusababisha ajali hiyo.

Amesema kuwa lori hilo liligonga magari matatu ya nyuma ya msafara huo na kusababisha ajali ambayo haikuwa ya lazima wka muda huo.

Amesema lori hilo lilikuwa linaokea nchini Kenya ambapo ilidaiwa pia lori hilo lilikuwa limebeba mali za magendo.

Hivyo imedaiwa dereva huyo ameshikiliwa na jeshi hilo ili kujibu tuhuma hizo.

Hata hivyo hakuna aliyeweza kupoteza masiha kaika ajali hiyo.

Monday, March 29, 2010

WORK FOR WATER IN PORTLAND OREGON WITH ERICK MWARABU


THE AMBASSADOR TO THE US HON.OMBENI SEFUE





Walk for Water-Down town Portland, was an event to drawing attention to the plight of millions of people whose access to safe drinking water is severely limited, Walk for Water raised funds to benefit Water For All, a non-profit organization dedicated to bringing clean water to families in sub-Saharan Africa. Walker registration fees, combined with local sponsor donations, went toward the goal of raising funds needed to build a series of water pumps in Tanzania. Ambassador Ombeni Sefue was the Key-note Speaker.
Eric Cliff Mwarabu
(Project Management/Marketing)
PORTLAND ROASTING.
503-236-7378 Main
800-949-3898 Free
503-841-3176 Mobile
503-231-2901 Fax

DINNER BANQUE IN LAS VEGAS


THE HONOR OF YOUR PRESENCE IS REQUESTED AT A DINNER BANQUET
WHICH WILL BE HELD ON SATURDAY 05.29TH.2010 AT 3525 E FLAMINGO RD LAS VEGAS NV 80121
R.S.VP NO LATER THAN MAY 8TH BY TELEPHONE OR EMAIL.
JACQUELINE KADIRI AT 707-290-4301 OR tonopa32@hotmail.com or
DOMICIAN MBEIKYA @ 707-290-2407 OR domcdavidy@yahoo.com
REGISTRATION WILL BEGIN AT 4:30PM AND DINNER WILL BE SERVED AT 5:30
REGISTRATION FEES OS $25 PER HEAD AND GROUP RATES FOR HOTELS ARE AVAILABLE .

MTOTO MWENYE VIDOLE 31 TOKA CHINA



Mtoto huyu wa nchini hana idadi ya vidole vya miguu na mikono kama watu wengine, amechukua rekodi ya dunia kwa kuwa na jumla ya vidole 31.
Mtoto mwenye umri wa miaka sita wa nchini China analazimika kufanyiwa operesheni ili kupunguza idadi ya vidole vyake vya mikono na miguu.

Mtoto huyo wa mji wa Shenyang katika jimbo la Liaoning kaskazini mwa China ana jumla ya vidole 16 vya miguu na vidole 15 vya mikono.

Vidole vyake vitatu katika kila mkono wake vimeungana pamoja.

Idadi ya vidole vyake inavunja rekodi ya dunia ya vidole 25 iliyokuwa ikishikiliwa na watoto wawili wa India Pranamya Menaria na Devendra Harne, ambao kila mmoja wao ana vidole 12 vya mikono na vidole 13 vya miguu.

Hata hivyo mtoto huyo wa nchini China atafanyiwa operesheni ya kupunguza idadi ya vidole vyake wiki hii.

MWANAME MWENYE MATITI MAKUBWA DUNIANI TOKA CHINA



Guo Feng mwanaume mwenye matiti makubwa Monday, March 29, 2010 4:58 AM
Madaktari nchini China wanadai kumgundua mwanaume mwenye matiti makubwa kuliko wote duniani.
Madaktari nchini China wanadai kumgundua mwanaume mwenye matiti makubwa kuliko wote duniani baada ya mwanaume huyo kujitokeza kwenye kliniki moja mjini Beijing.

Daktari wa hospitali ya Jinan Chest Hospital, Dokta Zhang Lilan alisema "Huyu ni mwanaume kamili isipokuwa ana matiti kama mwanamke".

"Yeye ni mkulima na anasema kuwa anasumbuliwa na ukubwa wa matiti yake wakati anapofanya kazi zake za kilimo".

"Anasema pia matiti yake yamekuwa gumzo kijijini kwake ambapo watu wengi wamekuwa wakimtafuta ili kumuona na imekuwa kero kubwa sana kwake kiasi cha kumfanya awe anavaa makoti makubwa hata wakati wa joto kali ili kuyaficha matiti yake", alisema dokta Lilan.

Mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la Guo Feng mwenye umri wa miaka 53, alisema "Miaka 10 iliyopita matiti yangu yalianza kuwa makubwa lakini nilikuwa nikifikiria unene wangu ndio sababu .. lakini miaka michache iliyopita nimekuwa nikizunguka hospitali moja baada ya nyingine kutafuta tiba lakini hakuna mtu anayetaka kunisaidia".

"Nimetumia pesa nyingi sana kwenye vipimo hospitalini lakini hakuna jibu lolote la maana huku matiti yangu yakiendelea kuwa makubwa", alisema Guo Feng.

"Wakati mwingine huwa nafikiria madaktari hawataki kunisaidia", alilamika Guo Feng.

Dokta Lilan alisema kuwa Guo Feng ametishia kuyakata matiti yake yeye mwenyewe iwapo hakuna daktari atakayejitokeza kumpatia tiba.

Hata hivyo madaktari wamekataa kuchukua hatua yoyote mpaka watakapogundua sababu ya matiti yake kuwa na ukubwa huo usio wa kawaida.

"Katika miaka yangu 30 ya kufanya kazi ya udaktari sijawahi kukumbana na kitu kama hichi", alisema Dokta Lilan.

"Awali tulidhania amekula kitu chenye sumu lakini vipimo vya damu yake havijaonyesha kitu chochote. Tumemfanyia X-ray hana dalili ya kansa", aliongeza mmiliki wa hospitali hiyo.

DARAU ZA RAISI WA ZAMAMNI WA MAREKANI GEORGE BUSH




Bush akiufuta mkono wake kwa kutumia shati la Bush Monday, March 29, 2010 5:45 AM
Rais wa zamani wa Marekani, George Bush ameingia katika zengwe kubwa sana baada ya kudaiwa kuonyesha dharau kwa kuufuta mkono wake kwa kutumia shati la rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton baada ya kupeana mkono na mhanga wa tetemeko la Haiti.
George W Bush ameingia kwenye zengwe kubwa sana baada ya kudaiwa kuufuta mkono wake baada ya kupeana mkono na raia wa Haiti aliyenusurika kwenye tetemeko kubwa la ardhi lililoikumba nchi hiyo na kuua maelfu ya watu.

Rais huyo wa zamani wa Marekani alinaswa live katika video akisalimiana kwa kupeana mkono na mkimbizi wa Haiti halafu alifuta mkono wake kwa kutumia shati la rais mwenzake mstaafu, Bill Clinton.

Tukio hilo limetokea wiki iliyopita wakati Bush na Clinton walipotembelea kambi ya wahanga wa tetemeko la ardhi mjini Port-au-Prince baada ya kuombwa na rais Barack Obama wafanye hivyo ili kutunisha mfuko wa kusaidia wahanga wa Haiti.

Bush anaonekana wazi akipeana mkono na mwanaume raia wa Haiti na kisha kuuzungusha mkono wake hewani akiangalia wapi ausafishe mkono wake kabla ya kuamua kutumia shati jeupe la Bill Clinton aliyekuwa amesimama pembeni yake kujifutia katika staili ambayo hata Clinton mwenyewe hakushtukia.

Video ya tukio hilo imewekwa kwenye YouTube na kuzua maoni mbali mbali mengi yao yakipigia kelele kitendo hicho.

Angalia VIDEO ya tukio hilo chini.

MADEREVA WA DALADALA DAR WATANGAZA MGOMO


MADEREVA na makondakta wa daladala wa jijini Dar es Salaam wametangaza mgomo wa kuacha huduma hiyo ambayo walidai utaanza leo.
Mgomo huo tarajio ulisambazwa kwa njia ya vipeperushi na baadhi ya madereva wa jijini humo na mgomo huo utahusisha njia zote za mkoa wa Dar es Salaam.

Sababu ya kuanzisha mgomo huo ulidaiwa na maderava hao kuwa ni maslahi duni kwa siku, na kubwa ni kero za barabarani zinazosababishwa na Kampuni ya Majembe na askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani (Trafiki) ambao wamekuwa wakiwasumbua kila siku kwa sababu ambazo hazina msingi.

Madai mengine ni kutaka kuwekewa mazingira bora ya kazi ikiwemo mishahara, na makato ya mishahara hiyo ipelekwe Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa lengo ya kuboresha kazi hiyo kama wafanyakazi wengine nchini.

ACTIVE FINANCE AND ACTIVE TOURS






Kevin William Mbogo
Chief Executive Officer
...............................
ACTIVE FINANCE AND ACTIVE TOURS
P.O.BOX 3176
Dar es salaam
Tanzania
Tel: +255 22 2134700
Fax:+255 22 2134700
Hotline: +255 787 888 884
+255 777 028 570
Email:info@activetz.com
Web:www.activetz.com

Sunday, March 28, 2010

INDIGENATION


FROM ARUSHA TO WASHINGTON DC
For all of you who resides in DC Metro Area, come join your country men in a Roots Reggae Jam Session and a debut show for Indigenation, a new Reggae Group lead by GMtui.

Thursday April 8th @ 9:30pm
Cover: Free
Location: O'Shaughnessy's Pub. 1324 King Street. Alexandria, VA 22314.

See Ad on Facebook (Indigenation Roots Reggae), CityPaper, www.tanzamerica.blogspot.com and more

Come one, Come all, Support the local.

iNdiGeNation
From Arusha to DC as it was from Hebron To Babylon.

SIMBA KUVUNJA REKODI YA MWAKA 1993



Wachezaji wa Simba wakishangilia ushindi katika mojawapo ya mechi za ligi kuu ya Bara Saturday, March 27, 2010 3:51 AM
MABINGWA wa Bara, timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam wamepania kuvunja rekodi yao ya mwaka 1993 ya kufika fainali ya Kombe la CAF, ambapo sasa wanataka kutwaa taji la Shirikisho hilo la Afrika. Simba mwaka 1993 ilitolewa katika fainali za CAF baada ya kufungwa 2-1 na timu ya Stella Abdjan katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa (sasa Uhuru).

Katika mchezo wao wa kwanza, timu hizo zilitoka suluhu na hivyo Simba ilihitaji ushindi wa angalau bao 1-0 ili kutwaa taji hilo.

Meneja wa timu hiyo, Innocent Njovu alisema jijini kuwa wana uhakika wa kutwaa taji hilo kutokana na kuwa na kikosi bora kama cha mwaka 1993.

Njovu alisema mbali na kikosi hicho kuwa bora pia wachezaji wao wamekuwa na ari ya ushindi baada ya kutwaa ubingwa wa bara mapema kabla ya ligi kumalizika, wakiwa wamesaliwa na mechi mbili kibindoni.

"Sisi tuna uhakika wa kufika kwenye fainali kwani kwa sasa kikosi ni bora, na wana ari ya kushinda katika kila mechi wanayocheza, hivyo kutokana na dhamira hiyo tuna uhakika wa kufikia hatua ya juu zaidi yaani ya fainali," alisema Njovu.

Alisema baada ya kuwapa mapumziko mafupi wachezaji wao, watapiga kambi huko Zanzibar kujiandaa na mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Lenghten ya Zimbabwe.

Katika mchezo wa awali uliofanyika Zimbabwe Ijumaa iliyopita, ambao Simba iliyofuzu hatua ya pili moja kwa moja, waliwashinda wapinzani wao kwao kwa magoli 3-0, ushindi ambao ni mnono kwa klabu hiyo.

Hata hivyo, Njovu alisema wapinzani wao sio wa kubeza kutokana na kandanda safi waliyoionyesha na wanaamini mchezo wa marudiano utakaofanyika Jumapili ijayo jijini Dar es Salaam, utakuwa wa ushindani mkubwa.

KAPUYA AWEKA UWAZIRI PEMBENI NA KUANZA KUPEKECHA



Katika hali isiyo ya kawaida kwa viongozi wa juu nchini kuonekana katika kumbi za starehe tena katika sare sambamba na waimbaji wa bendi, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya aliingia ukumbini na kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya wana wa Akudo. Huku akiwa amevalia sare sawa na waimbaji wa bendi ya Akudo, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya alijitosa ukumbini na kuanza kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya bendi ya Akudo Impact iliyokuwa ikitoa burudani kwenye ukumbi wa Msasani Beach.

Kapuya ambaye ndiye mmliki wa bendi hiyo alijimwaga stejini na kusakata muziki kwa nguvu zote huku jasho likimtoka akiwa pamoja na mpambe wake ambaye jina lake halikufahamika.

Kapuya anakuwa kiongozi wa pili wa juu serikalini kumiliki bendi wa kwanza alikuwa Waziri Mdhihiri Mdhihiri ambaye aliwahi kumiliki bendi ya Mchinga Sound ambayo baadaye ilivunjika.

Kutokana na jinsi anavyoithamini bendi yake, waziri Kapuya amefanikiwa kuifanya bendi ya Akudo iwe miongoni mwa bendi zinazopendwa sana nchini kiasi cha kuleta ushindani mkubwa katika medani ya muziki wa dansi hapa nchini.

BABU WA MIAKA 96 AMUOA MWANAMKE WA MIAKA 30



Babu mwenye umri wa miaka 96 wa nchini Taiwan amekuwa gumzo nchini humo baada ya kufunga ndoa na mwanamke aliyemzidi miaka 66. Babu Lin Chung ameweka rekodi ya kuwa bwana harusi mwenye umri mkubwa kuliko wote nchini Taiwan baada ya kufunga ndoa na mwanamke mwenye umri wa miaka 30.

Chung amekuwa gumzo kwenye kitongoji cha Tainan baada ya kumuoa mwanamke huyo anayetoka maeneo ya ukanda wa kati nchini China katika jimbo la Hunan.

Chung ambaye hakuwahi kuoa katika ujana wake, ana watoto wawili aliojitolea kuwalea tangia walipokuwa wadogo ambao hivi sasa mmoja kati ya watoto hao ana umri wa miaka 68.

Chung anadai kwamba miaka mitatu iliyopita, alipewa maelezo na Mungu aende kwenye jimbo la Hunan nchini China ili kumtafuta mwanamke anayekuja kuwa mke wake.

Chung alifunga ndoa na mwanamke huyo hivi karibuni pamoja na upinzani mkali toka kwa mwanae huyo wa kujitolea ambaye alikuwa akimuona babu huyo kama amelaghaiwa.

"Inanibidi niwe na mwenza katika uzee wangu... sikuwahi kuwa na mke, kwanini hivi sasa hataki mimi nioe", alisema Mzee Chung.

Chung hivi sasa anashughulikia taratibu za kisheria kumwezesha mkewe ahamie Taiwan toka China ili waishi pamoja.

Saturday, March 27, 2010

"FROM ARUSHA TO DC AS ITS WAS FROM HEBRON TO BABILON



CAME ON PEOPLE LETS SHOW SOME LOVE TO OUR FOX FROM HOME.
DC ARE YOU READY???????????????????
ITS GOING DOWN FOX!!!!!!!!!!ITS REALLY GOING DOWN .LETS GIVE IT UP FOR OUR BROTHERS.
DON'T MISS IT DC ITS GOING DOWN.

MAYALA WEBTECH SOLUTIONS




Hallow fellow Tanzanians; this is Isack Mayala presenting MAYALA WEBTECH SOLUTIONS (M.W.S). This is a global full service firm that offers web designing from scratch, re-designing old websites, logo designing, flash designing, business card design, online website solution e.g. e-commerce and database management.

Our product/service is purchased by corporations, universities, and organizations around the world. Below is a list of just a few of our clients that we have provided our services for over the years.

http://www.angellalubala.com

http://www.holifrench.org

http://www.themissionband.org

http://www.christianmissionschurch.org

We are here to create, implement and provide the most needed web services and educate consumers to use those products as an integrated part of their business. We are currently based in United States of America; soon we will be opening our offices in Dar Es Salaam, Tanzania. Please visit our website http://www.mayalawebtech.com for more information. Send us an email at info@mayalawebtech.com if you have any question.

Thanks in advance for your business

Friday, March 26, 2010

APOTEZA MAISHA KWA MOTO KISA KUKATALIWA


Mwanaume mmoja wa nchini Uingereza ambaye alitoswa na mkewe wa ndoa ya miaka 14 ambaye alipata mwanaume mwingine nje, amefariki dunia kutokana na moto aliouanzisha ili kuichoma moto nyumba yake ili mkewe asiambulie kitu watakapoachana. Wakati Timothy Flood alipoimiminia petroli nyumba yake ili ndoa yake na mkewe itakapovunjika, mkewe asiambulie kitu, hakungundua kuwa kuna kiasi kidogo cha petroli kilimwagikia kwenye nguo zake.

Na wakati alipoipiga kiberiti nyumba yake alishangaa kujikuta na yeye mwenyewe akiwaka moto.

Timothy ambaye ni baba wa watoto watatu alijaribu kuuzima moto uliokuwa ukimteketeza kwa kutumia maji ya mvua lakini hadi wakati anaokolewa alikuwa ameishangua asilimia 90 ya mwili wake na alifariki dunia siku mbili baadae hospitalini.

Timothy mwenye umri wa miaka 42, aliamua kuichoma moto nyumba yake baada ya mkewe kuamua kuivunja ndoa yao alipoanza uhusiano na mwanaume aliyesoma naye shule.

Ingawa Timothy na mkewe, Catherine, 39, walikuwa wakiendelea kuishi kwenye nyumba moja walikuwa hawazungumzi wala kujuliana hali.

Mgogoro mkubwa ulikuwa kwenye nyumba yao ambapo Catherine alimtaka Timothy aondoke amuachie yeye nyumba hiyo.

Timothy kwa kuhofia kuwa watakapoachana rasmi kisheria kutokana na sheria mkewe anaweza akapewa nyumba kwa sababu ya watoto wao,
aliamua kuichoma moto ili wakose wote.

Mahakama katika mji wa Newport, kusini mwa Wales iliambiwa kuwa Timothy ili kuichoma moto nyumba hiyo alinunua lita 51 za petroli na viberiti kadhaa ili kuhakikisha kuwa hakitoki kitu.

Siku ya tukio, alimpeleka mkewe kwa wazazi wake na ndipo aliporudi na kuipiga moto nyumba hiyo baada ya kumtumia meseji mkewe akimwambia "Nimeishapata suluhisho la kuishi bila wewe".

Moto mkubwa ulizuka ambao uliiteketeza sehemu kubwa ya nyumba hiyo.

Majirani wanasema kuwa Timothy alisikika akipiga kelele za kuomba msaada wakati moto aliouanzisha akitegemea kuiteketeza nyumba yake ulipokuwa ukimchoma yeye mwenyewe.

Timothy alifariki siku mbili baadae hospitalini baada ya ndugu zake kukubali kuzizima mashine zilizokuwa zikimsaidia aendelee kuishi.

DR,SLAA AMFURISHA KIKWETE

BAADA ya Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa kuibana serikali kuhusu vipengele vilivyoongezwa kinyemela katika muswada uliosaniwa na Rais Jakaya Kikwete kwa mbwembwe wiki iliyopita, taarifa mpya zinasema Rais amefura, akitaka maelezo ya kina ya walioingiza vipengele hivyo.

Tanzania Daima lilipozungumza na mmoja wa wasaidizi wa Rais Kikwete kuhusu sakata hilo jana, alidokeza kwa maneno machache, na kwa msisitizo, akisema: “Rais amefura.”

Msaidizi huyo wa rais alisema kutokana na kasoro hiyo ya kwanza ya aina yake kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii, Rais Kikwete ametaka maelezo ya kina ili kubaini waliohusika kuchomeka vipengele hivyo.

Naye Dk Slaa, ambeye ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amezidi kuibana serikali akiitaka irejeshe bungeni Muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi ili kifungu kilichochomekwa kinyemela kiondolewe.

Alisema hilo ni hitaji la lazima la kisheria; na kwamba serikali isipofanya hivyo katika mkutano ujao wa 19 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, itachukuliwa hatua za kisheria. Alitaka waliohusika wawajibishwe.

Dk. Slaa, mmoja wa wabunge wanaosoma sana na wenye upeo mkubwa bungeni, ndiye aliyeibua sakata la kasoro hiyo wiki hii.

Jana alisema: “Naomba serikali ichukue hatua kuwasilisha Miscellaneous Amendment katika mkutano wa 19, yaani Bunge la Aprili, ili kifungu hiki ambacho ni kinyume na demokrasia kiondolewe kwenye Sheria ambayo rais ameisaini, vinginevyo tutachukua hatua za kisheria.

“Kama ilivyoripotiwa na gazeti la Tanzania Daima, Mhe. Spika jana wakati anajibu kwenye taarifa ya saa mbili usiku ya TBC1 ni dhahiri alionyesha kuwa hajasoma na hakuwa ameelewa vizuri kinacholalamikiwa.

“(Kama) Angekuwa amesoma, Spika angekuwa mwangalifu kutamka aliyoyatamka. Mheshimiwa Spika anakiri kulikuwa na mjadala, lakini hakutamka mjadala ulihusu nini na wala hakumnukuu Mwenyekiti wa siku hiyo ambayo alikuwa Mhe. Naibu Spika alitoa maagizo gani.

“Ni hatari kwa viongozi wetu kutoa matamko kwa mambo mazito bila kufanya utafiti angalau mdogo. Mhe. Spika atakubali kuwa kwenye Hansard, hakuna popote ambapo imejadiliwa achilia mbali kukubaliwa kuwa ‘Timu ya Kampeni itathibitishwa na Msajili (kwa
mgombea urais) au Katibu Tawala (kwa mgombea ubunge) au na Mtendaji wa Kata kwa (mgombea udiwani).’ Hii ni dhana mpya kabisa, siyo tu haijajadiliwa wala haikufikiriwa kama Hansard inavyoonyesha.”

Dk. Slaa alitoa kauli hii ya jana wakati akijibu kauli ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye juzi alizungumza kupitia kituo cha Televisheni cha TBCI, akitetea udhaifu huo wa kuchomeka kipengele hicho kiholela.

Dk. Slaa alifafanua kuwa kilichojadiliwa ambacho yeye alishiriki ni hoja aliyoleta Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge kutaka kufanyia mabadiliko pendekezo la serikali kwa kifungu cha 7(2).

Alisema katika kifungu hicho, Chenge alitaka makundi ya sanaa yaingizwe baada ya neno voters.

“Hivyo ni vyema naye Spika akiri tu kuwa utaratibu wa kutunga sheria umekiukwa. Haifai kubishana kwa sababu ya kubishana wakati Hansard ndiyo ushahidi wa wazi wa jambo hilo.

“Mimi ndiye namwomba Mwanasheria Mkuu, rafiki na ndugu yangu, aisome vizuri kwa kuwa yeye ndiye hajasoma. Amesema vizuri kututaja ambao tulikuwa na mjadala ukumbini, sasa anionyeshe mahali popote katika mjadala huo ni wapi approving authority ilijadiliwa, na kuwa hiyo approving authority iwe Msajili, DAS na WEO.

“Hivyo, ni ustaarabu tu kukiri kuwa kifungu hiki kimechomekwa na kuwa akubali,” alisema Dk. Slaa.

Hata hivyo, tayari Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema juzi aliliambia gazeti hili kwamba iwapo itabainika kuwa kauli ya Dk. Slaa ni ya kweli, serikali itaomba radhi na kupeleka muswada bungeni kwa ajili ya masahihisho hayo.

Dk. Slaa alidai Rais Kikwete amepotoshwa katika baadhi ya vipengele, kikiwamo kipengele kinachohusu uthitibishwaji wa wajumbe wanaounda timu za kampeni kwa ajili ya wagombea urais, wabunge na udiwani.

Alisema Bunge halikukubaliana kuhusu kipengele hicho, wala hakimo katika kumbukumbu za Bunge; na kwamba kiliongezwa baadaye, kabla ya Rais Kikwete kusaini muswada huo kuwa sheria.

Kifungu kinachodaiwa kuchomekwa ni cha 7 (3), ambacho hakikuwepo kabisa kwenye muswada uliojadiliwa na kupitishwa bungeni.

Kwa mujibu wa sheria hiyo, kifungu kidogo cha pili, kinaeleza maana ya timu ya kampeni kuwa ni kundi la watu lililoundwa na mgombea wakati wa zoezi la uteuzi lenye madhumuni ya kumwakilisha au kumsaidia mgombea kwenye kampeni za uchaguzi ambaye amepitishwa kuwania.

“(a) Kwa kesi ya urais watathibitishwa na Msajili, (b) Kwa kesi ya Mbunge watathibishwa na Katibu Tawala wa Wilaya na (c) Kwa kesi ya Diwani watathibitishwa na Katibu Tarafa...,” ilieleza sehemu ya sheria hiyo iliyosainiwa na Rais Kikwete ambayo nakala yake tunayo.

Muswada huo wa sheria ulioasisiwa na Rais Kikwete mwenyewe, ulipitishwa kwa mbinde Februari 12 mjini Dodoma huku ukiibua malumbano makubwa baina ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Werema, na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, pamoja na wabunge wengine kuhusu vipengele mbalimbali vya muswada huo.

MREMA AFUNGUA KESI MAHAKAMANI,ADAI BIL 1/-

HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema amefungua kesi ya madai ya sh bilioni moja dhidi ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Kesi hiyo ya madai namba 32/10 imefunguliwa na mwenyekiti huyo anayeongoza chama chenye wafuasi wasiozidi 500,000 nchini kote kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya chama hicho Magomeni, Dar es Salaam jana, Mrema alieleza dhamira yake ni kutaka kupata uthibitisho kutoka kwa spika huyo wa Bunge kama amefilisika na kwa sasa anahongwa na makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kadhalika, Mrema anadai kwamba kitendo cha Sitta kuieleza jamii kupitia gazeti kwamba amechanganyikiwa na amepewa fedha kwa ajili ya kuipigia debe CCM kina lengo la kumdhoofisha katika kampeni zake za kuwania ubunge wa Vunjo kwa tiketi ya TLP.

“Katika barua niliyopeleka kwa Spika nilitaka aniombe radhi kwa uzito ule ule katika kipindi cha siku saba na kunilipa fidia, lakini akawa kimya kwa muda wote huo,” alisema Mrema na kuongeza kwamba washitakiwa wengine katika kesi hiyo ambayo haijapangiwa jaji ni gazeti lililochapisha habari hiyo na mhariri wake akiamini kuwa ndiyo chombo kilichotumika kumchafua na kumpotezea hadhi aliyojijengea.

“Hivi kweli mimi nimechanganyikiwa? Kwanini anivunjie hadhi yangu?… Nimekuwa Naibu Waziri Mkuu wa nchi hii, nimefanya mengi sana nilipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, kwa miaka 30 nimeitumikia Tanzania,” alisema Mrema.

NYUKI WENYE HASIRA WAUA MIFUGO NA KUJERUHI WATU 40


Nyuki wenye hasira walikitesa kijiji kizima nchini Niger kwa masaa kadhaa na kuua mifugo kadhaa pamoja na kuwafanya watu zaidi ya 40 wakimbizwe hospitali wakiwa majeruhi. Kundi la nyuki waliokuwa na hasira baada ya mzinga wao kwenye mti kung'olewa, walikitesa kijiji kimoja kusini mwa nchi ya Niger kwa kuwashambulia watu na mifugo kwa masaa kadhaa.

Watu zaidi ya 40 wakiwemo watoto 14 waliwahishwa hospitali baada ya kushambuliwa na nyuki wakati mzinga wa nyuki uliokuwa kwenye mti mkubwa kwa zaidi ya miaka 50 ulipodondoshwa chini kutokana na upepo mkali.

Punda mmoja na farasi mmoja walifariki dunia huku ng'ombe na mbuzi 95 wakiachwa wakiwa wamepooza miili yao baada ya kudungwa sindano za nyuki hao wenye hasira.

Kwa mujibu wa radio Anfani ya nchini Niger, nyuki walikivamia kijiji cha Dake-Garka katika mji wa Birni-N'Konni baada ya tawi la mti lililokuwa na mzinga wao, lilipoangushwa chini na upepo mkali.

Iliripotiwa kuwa masaa kadhaa baada ya uvamizi wa nyuki hao, wanakijiji walikuwa bado wanahofia kurudi kwenye majumba yao kwa kuhofia mashambulizi ya nyuki.

CALIFORNIA NEW LAW WONT HURT ECONOMY

SAN FRANCISCO

California's economy will not be damaged by the state's 2006 climate change law, a state agency said in a report yesterday that counters the business community's arguments that the economically troubled state will lose more jobs and businesses.

The analysis by the state Air Resources Board, the chief regulator of the law, forecast higher energy prices from new regulations and a cap-and-trade system for greenhouse gases, but said greater energy efficiency would keep costs manageable in the trend-setting environmental state.

It concluded that the measure will yield modest job gains statewide, will have a negligible effect on the state's overall economy -- the eighth largest in the world -- and could benefit some sectors like alternative energy businesses.

In sharp contrast to a 2008 report that was panned as shallow and full of faulty assumptions, the Wednesday analysis was received with cautious approval from academics at Stanford and other universities who consulted on the process.

Business groups however said the state was still making rosy assumptions.

In 2006, California's Legislature passed and Republican Governor Arnold Schwarzenegger signed a law committing the state to developing regulations to reduce greenhouse gas emissions -- blamed for global climate change -- to 1990 levels by 2020.

"These policies can shift the driver of economic growth from polluting energy sources to clean energy and efficient technologies, with little or no economic penalty," the report said.

Thousands of manufacturing, mining and utilities industry jobs will be lost, but service, finance, and other sectors will gain similar numbers, leaving the most populous US state about the same in terms of total jobs, income and growth, the report said. Five scenarios found a maximum effect of tens of billions of dollars on state output of $2.5 trillion in 2020.

Much will depend on what happens outside California, including whether California is at the leading edge of a move away from fossil fuels.

"It might hasten the arrival of regional, national or other international policies, and I think that is what California is betting on," said Stanford economist Larry Goulder, one of the academics on the panel advising state researchers.

California aims to reduce greenhouse gas emissions through a variety of steps such as tighter standards on car fuel efficiency, standards on energy efficiency in buildings, and a "cap and trade" market for pollution credits.

Under cap-and-trade, carbon dioxide and other greenhouse gas emissions would be capped. Companies would need permits for the pollution they send into the atmosphere and those permits could be traded on a regulated market.

Three US senators -- Democrat John Kerry, Republican Senator Lindsey Graham and independent Senator Joseph Lieberman -- are working to resuscitate climate change legislation in the US Senate after the House of Representatives passed its version of the measure last year.

A parallel study by consultancy Charles River Associates, which worked at the request of the Air Resources Board, put the cost of the climate law at a few hundred dollars per person in 2020 and said success would depend on the state giving itself room to respond to issues, such as high gasoline prices.

"It is clear that flexibility matters," said Charles River consultant Paul Bernstein.

Many businesses still fear tens or hundreds of thousands of jobs could be lost, spurred by higher energy prices from the law, known locally as AB32.

"Their conclusion is that AB32, the most far-reaching regulation in history, won't impact jobs in California," Shelly Sullivan, spokeswoman for the AB 32 Implementation Group, which includes several chambers of commerce, said skeptically.

Goulder and the other economists called the new report "valuable information" and said it addressed key concerns by creating a better scenario if the law did not take effect and scenarios if parts of the law did not work as planned.

Mary Nichols, chair of the Air Resources Board, told reporters that the new analysis was better than 2008.

"We made all the changes and found that the results were pretty much the same as they had been the first time around, which is very modest, almost undetectable overall effect on gross state product by 2020 but some modest improvement in areas of job growth and personal income," she said.

AJALI MBAYA DAR, HIACE YAKANDAMIZWA NA LORI




ZAIDI ya watu nane wamepoteza maisha papohapo kwa ajali mbaya iliyotokea huko maeneo ya Kibamba Darajani nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Ajali hiyo ilitokea jana, majira ya saa 11 alfajiri ambapo ilihusisha gari aina ya lori lililokuwa na namba za usajili T 189 na basi dogo la abiria aina Toyota Hiace lililokuwa na namba za usajili T 616 AJW.


Ajali hiyo imetokea baada ya lori hilo lililokuwa likitoka Dar es Salaam kuelekea Pwani kupoteza mwelekeo na kuingia kulia zaidi na kuivaa basi hilo uso kwa uso lililokuwa na abiria na kulilalia na kupoteza maisha ya watu hao.

Hiace hiyo ilikuwa inatoka Lugoba mkoani Pwani ilikuwa inaelekea Dar es Salaam na ndipo ilipovamiwa na lori hilo na abiria wote waliokuwemo humo kufariki dunia papohapo na kati yao kulikuwa na mamda mjamzito.


Hata hivyo ilidaiwa kuwa lori hilo lilikuwa imeshindwa kuhimili breki na kudaiwa halikuwa na breki na ndicho chanzo kikuu cha ajali hiyo mbaya.

Hata hivyo mara baada ya kutokea kwa ajali hiyo dereva wa lori na utingo wake wlikimbia na kuacha lori hilo papohapo na hawakujulikana mara moja walikimbilia wapi kwa muda huo.

Katika hali ya kushangaza wananchi bado hawajifunzi na baadhi ya maelfu waliokimbilia katika ajali hiyo kuonekana kuzoa mafuta ya taa yaliyomwagika barabarani na kusahau kuwa siku za karibuni watu walipoteza maisha kutokana na matukio kama hayo walikuw wnazoa mafuta na ghafla lori kulipuka na kupoteza maisha na wengine walipata vilema vya maisha kutokana na

MAHABUSU WAJIPAKA KINYESI MAHAKAMANI DAR.

MAHABUSU watano jana walitoa kioja cha mwaka katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni walijipaka kinyesi kwa kugoma kurudi mahabusu. Washitakiwa hao wanaokabiliwa na kesi ya wizi wa kutumia silaha wote kwa pamoja walichukua uamuzi huo baada ya kugoma kurudi mahabusu kwa kutaka wafutiwe mashitaka yao ambayo yamedumu wka muda mrefu.


Hivyo washitakiwa hao walipotakiwa na askari magereza kutoka mahabusu na kuelekea mahakamani walichukua vinyesi na kujipaka mwilini.


Hali ilikuwa tata walipofika mahakamani hapo hali iliyoradhimu hakimu kushindwa kuendelea kusikiliza shauri hilo kwa siku hiyo.


Mahabusu hao walionekana kugoma kupanda basi maalum linalowarudisha rumande kwa madai ya kutaka kufutiwa shauri hilo hali iliyofanya wapakiwe kwenye gari dogo na kupelekwa kituo cha polisi Magomeni.

EASTER SPECIAL AT MENAI BAY BEACH BUNGALOWS!!!


SUNSET VIEW AT MENAI BAY BEACH BUNGALOWS!!! IT'S LOVELY

YOU WILL GET A CHANCE TO RELAX AND ENJOY ON THE LOCALLY BEDS.

SINGLE ROOM AT MENAI FRESH WEATHER AND CLEAN!!!



DOUBLE ROOM

MENAI BUNGALOWS FROM OUTSIDE
NAI BAY BEACH BUNGALOWS

Menai Bay Beach Bungalows (Unguja Ukuu) Consisting of five beach bungalows set in a shady palm grove direct on the beach.

THE BEACH BUNGALOWS.
The hotel Menai consists of ten rooms in bungalows, built of local materials. The rooms are equipped with double or king size beds, mosquito nets, 4 rooms with fans & 6rooms with fan and Air Conditions.
The private verandah overlooks the lush tropical gardens and the Indian Ocean beyond. All rooms have their own bathroom with toilet, washing basin, shower and hair dryers.

THE BEACH RESTAURANT (NEW MASAI RESTAURANT)
Is situated direct on the beach under a huge baobab tree. Our specialty is all kind of fresh caught seafood, prepared in international or traditional local style.
Enjoy romantic sunsets over the bay while sipping a glass of wine.

We are proud of our lush tropical garden.
1000 years old Baobab trees, Mango and Almond trees, Bougainvilleas and Barbados Pride illuminate the hotel ground.

EASTER SPECIAL OFFER FOR TANZANIAN AND EST AFRICANS.
ROOMS WITH FANS
SINGLE ROOM ON BB Tshs. 25,000 per night
DOUBLE ROOM ON BB Tshs. 30,000 per night
TRIPLE ROOM ON BB Tshs. 50,000 per night
ROOMS WITH AC
SINGLE ROOM ON BB Tshs. 30,000 per night
DOULBE ROOM ON BB Tshs. 35,000 per night
TRIPLE ROOM ON BB Tshs. 55,000 per night
HB SUPPLEMENT
ADULT ON HB Tshs. 15,000 per person
CHILD ON HB Tshs. 10,000 per child
FB SUPPLEMENT
ADULT ON FB Tshs. 20,000 per person
CHILD ON FB Tshs. 15,000 per child
Includes 1 soda, a glass of juice or bottle of water
during the meal.
TWO NIGHTS STAY – you get free tour to Jozani Forest where you can see Red Colobus Monkeys and etc.

BEACH PARTY ON 3RD APRIL 2010
ENTRANCE FEE: TSHS 5,000 FOR MEN (includes 1 drink)
LADIES FREE.

Enjoy with us UNFORGETTABLE HOLIDAY in an untouched nature far off the beaten track.
Contact: +255 0 777 422008 / 0 715 422009 / 0 769 662662

Thursday, March 25, 2010

ON THE SPOT-CAROLA KINASHA(TANZANIAN DIVAS)


When you talk of Afro-fusion music in Tanzania and leave out Carola's name you will be doing a great injustice. The songstress is one of the great musicians around who maintain a low profile. She spoke to Erick Mchome about herself.
Where were you born? I am a Maasai born in I.ongido in Arusha.
Are you married? Yes, to a fellow Tanzanian and we have two kids.
Where exactly do you live? I am based at Kinondoni in Dar es Salaam.
How many countries have you visited so far? Music has taken me to more than 10 countries.
How do you manage to keep your voice? I do not really take care of it, as I smoke but it is natural and am proud of it.
Who would you like to feature in your music? I prefer those not yet recognized like Anania Ngoliga (Tanzania) while in South Africa, I would go for a woman called Letambulu.
What can't you live without? My children; they are so precious to me.

INVESTORS IN DAR TRANSPORT TO ENJOY TAX EXEMPTION


The Tanzania Investment Centre (TIC) has joined the drive to address public transport woes in Dar es Salaam and efforts being by made by the authorities to end the nagging problem of traffic congestion in the city.
The agency said it is now ready to offer fiscal incentives to enable local investors to import modern buses to create public transport fleets, which are a sure way of safe commuting in cities. The TIC incentives include tax exemptions to transporters who will import new big buses for providing commuter services in the city.
Its director of Investment Promotion Raymond Mbilinyi told BusinessWeek recently that the incentives aim at encouraging local investors to invest in modernizing public transport to overhaul the current wanting system and help to reduce traffic jams on Dar es Salaam roads.
He said investors interested to invest in commuter bus companies can approach the agency for assistance.  
"TIC can assist in providing incentives such as tax exemptions to local investors who form partnerships to acquire modern buses. The incentives will not only attract and retain the investors in the city transport sector, but also help to create formal jobs in the industry and the national economy at large," he said.
TIC has been reluctant in the past to give bus operators such incentives, they said, was important for the sector’s growth and development as well as a measure to increase the safety of passengers.
Owners of upcountry buses have for many years called on the agency to include passenger buses into the list of capital goods which would make them eligible for exemption of some taxes.
Last year, Mr Mohamed Abdullah, the chairperson of the Tanzania Bus Owners Association, told BusinessWeek that its members wanted the government to waive VAT on new buses. He said by doing so, would greatly help to address the problem of accidents on the country’s roads since transporters would be enabled to reasonably acquire news buses.
But with the tax on, he noted, acquisition of new buses is expensive, forcing many transporters to resort to old vehicles that jeopardize the safety of passengers.
It is expected that TIC’s fiscal incentives offer will also include buses plying upcountry routes. Currently, buses providing upcountry transport services, also include those with built on lorry chasses, which logistics management experts say is mechanically wrong.
TIC says tax waiver for public commuting buses will be given to transporters who partner to form companies or associations operating transport fleets. In Kenya, such services are provided by groups of operators who have joined forces to form saving and credit cooperative societies (saccos).
The Surface and Marine Transport Regulatory Authority (Sumatra), has already ordered Dar es Salaam commuter bus owners to form transport such organisations or risk being banned from doing business.
The authority argues that Dar es Salaam public transport currently dominated by individuals owning single buses, would improve if the owners operate as companies or cooperative societies. The present chaotic nature of the city’s transport is due to the fact that each owner tries to maximize revenue in a single day without regard to traffic rules or safety of commuters.
"Only operators who team up to form companies will be licensed and the rest will be banned,” Sumatra director-general Israel Sekirasa had told commuter bus owners at a recent meeting in Dar es Salaam.
He said the plan had many advantages including improving city transport and enabling bus companies to easily get loans from financial institutions. Mr Mbilinyi urged private operators to form partnerships to create medium and large commercial fleets that would facilitate profitable operations.
According to him, engaging the private sector in transport service delivery is important in improving services, adding that private companies or cooperatives can also easily attract local capital and/or foreign direct investment that are required to transform the sector.
The investment promotion expert said transport companies could raise money from banks to finance assets and vehicle acquisition through arrangements such as leasing finance and capital markets.
He urged commuter operators to form saccos as a way of raising long-term capital from various sources since such groupings appeal more to financiers than individuals. He said major benefits of commencing commuter city bus transport companies would include improvement of quality of service and enhancement of planning and management of operations.
Available statistics show that currently, Dar es Salaam has about 6,000 commuter buses that are owned by about 3,171 operators. These buses carry only 43 per cent of the city daily commuters. Most of the commuter buses have a capacity of less than 30 seats. This results into most people resorting into to owning vehicles.
Other benefits to be accrued from forming city bus transport cooperatives is the reduction in vehicle operating costs, improving efficiency and offer quality service to commuters. Logistics expert say such arrangements would also be an incentive for attracting investors to establish bus assembly plants in Tanzania.
Commuting fleets, they argue, would also promote use of compressed natural gas [CNG] or biodiesel for public transport, hence reducing fossil fuel imports. That would also boost possibility of undertaking of clean development mechanism [CDM] transport project, whose focus is reducing carbon emissions.
The CDM transport initiatives are being promoted worldwide to help attract financing of urban public transport using windows of carbon trading. Tanzania is also considering venturing into that area.
Mr Mbilinyi said limitations to efficient and safe public transport in the country include limited incentive packages, constrained financing as result of the global financial and economic crisis, infrastructure limitations and high fossil costs. According to him, investment in modern bus fleets is not only about getting money, but employment of contemporary business management practices.

AJIPIGA RISANI KICHWANI KWENYE HARUSI YA RAFIKI YAKE KISA MCHEZO WA RUSSIAN ROULETTE


Mwanaume mmoja nchini Urusi anashikiliwa na polisi baada ya kuanzisha mchezo wa kuchezea bunduki katikati ya sherehe za harusi na kupelekea mwanaume mmoja ajipige risasi ya kichwa. Huku bwana harusi na bi harusi wakiangalia kwa mshtuko mkubwa, mwanaume aliyepewa bunduki aigize anajipiga kichwani baada ya kuambiwa kuwa bunduki hiyo haina risasi, aliichukua bunduki na kuielekeza kichwani mwake.

Huku watu wengine wakimsihi asijaribu kufanya hivyo, mwanaume huyo aliielekeza bunduki kichwani na alipoifyatua risasi ilitoka kweli na kulifumua fuvu la kichwa chake.

Mwanaume huyo amelazwa hospitali akiwa amepooza mwili wake huku ubongo wake ukiwa umeharibiwa vibaya na risasi hiyo.

Kasheshe hilo lilianza kwa mwanaume mmoja ambaye ni rafiki wa bwana harusi alipotoa bunduki na kuwaalika watu waje kucheza mchezo unaoitwa "Russian Roulette".

Mwanaume huyo alijielekezea mwenyewe risasi na kuifyatua lakini risasi haikutoka. Ndipo alipomualika mtu mwingine naye aje ajaribu.

Video ya tukio hilo iliyowekwa kwenye tovuti ya YouTube inamuonyesha mwanaume huyo akiichukua bunduki na kuielekeza kichwani kwake kabla ya kuifyatua na yeye mwenyewe kuanguka chini na kuzua mshikeshike kwenye harusi hiyo.

Rafiki huyo wa bwana harusi anashikiliwa na polisi ingawa alijitetea kuwa alikuwa akijua kuwa bunduki yake ilikuwa tupu haina risasi.

Mchezo wa Russian Roulette ulikuwa ukifanyika kwenye jela za Urusi wakati wa miaka ya mapinduzi ya Urusi ambapo wafungwa walilazimishwa kuzichezea bunduki huku maafisa wa jela wakicheza kamari kujua mfungwa yupi atafariki kwanza.

Chini ni VIDEO ya tukio hilo la kwenye harusi.

MATATANI KWA KUMPIGA MGONJWA WA TB

MWANAMKE mmoja jana aliingia matatani baada ya kushindwa kuvumilia matusi aliyokuwa akitukanwa na mgonjwa wa kifua kikuu na kujikuta akimpiga ili aweze kumliza hasira zake. Tukio hilo lilitokea jana majira ya jioni, huko Mbagala Charambe baada ya mwanamke huyo [jina kapuni] kumpa kipigo mgonjwa huyo ambaye anaumwa kwa muda mrefu.

Ilidaiwa mwanamke huyo ambaye anaishi jirani na anakoishi mgonjwa huyo, alipatwa na jazba baada ya mgonjwa huyo kumtukana matusi na kushindwa kuvumilia na kumtia mikononi.

Ilidaiwa mgonjwa huyo alimtukana mama huyo matusi ya nguoni na ilidaiwa ni kawaida yake kumtuakana masma huyo na siku hiyo alishindwa kuvumilia na kumtiq mikononi.

Ilidaiwa ndugu wa mwanamke huyo walimsihi asimpige mgonjwa huyo japo kuwa anamatatizo mana alikuwa anatumia kigezo cha ugonjwa wake na kumsihi anaweza akapatwa na matatizo..

Bila kutambua alijikuta akimuingia mgonjwa huyo na ndugu wa mgonjwa huyo kuchachamaa na kwenda kuripoti kituo cha polisi.

Hata hivyo ilidaiwa kuwa mwanamke huyo alitakiwa kituo cha polisi akatoe maelezo machache kuhusiana na sakata hilo.

Kitakachoendelea kitawajia baada ya kupata tarifa kamili

MITI 6OOO YAKATWA KUZUIA WATU KUFANYA MAPENZI UKO UINGEREZA




Miti ipatayo 6,000 iliyopo pembeni mwa barabara moja kuu nchini Uingereza imekatwa ili kuwazuia watu kupeana huduma za chap chap. Miti zaidi ya 6,000 iliyopo pembeni barabara namba A666 katika mji wa Darwen kaskazini masharibi mwa Uingereza imeteketezwa ili kuwazuia watu kufanya mapenzi chini ya miti hiyo.

Miti hiyo iliyochukua eneo la hekta 12 ilikuwa ni maarufu kama kituo cha watu wanaopeana huduma za mapenzi za chap chap.

Miti hiyo iliyopandwa baada ya vita vya pili vya dunia, ilikatwa baada ya maafisa wa manispaa ya mji huo kudai kuwa miti hiyo imezeeka na inaweza ikayaangukia magari yanayopita kwenye barabara hiyo.

Lakini sajenti wa polisi Mark Wilson alisema kuwa miti hiyo ilikatwa kutokana na kuwa kero kwa wapitanjia kutokana na baadhi ya watu kupenda kufanya mapenzi kwenye maeneo ya miti hiyo huku wakionekana wazi.

"Lilikuwa ni tatizo la muda mrefu lililoleta kero kero kubwa sana kwa jamii", alisema sajenti Wilson.

Haijajulikana kama kukatwa kwa miti hiyo kutaleta ufumbuzi wa tatizo hilo la watu kujisevia pembeni mwa barabara hiyo.

CHINI YA ULINZI KISA UZURURAJI

WASICHANA wawili wamejikuta wakiwa katika wakati mgumu baada ya kuchaniwa nguo zao walizovaa kwa kuonekana walikuwa wabishi baada ya kukutwa na askari wa mtaani maarufu kama sungusungu.
Wasichana hao majina hayakuweza kupatikana mara moja walikutwa na dhahama hiyo, juzi majira ya usiku huko maeneo ya Mnazi Mmmoja jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa maelezo ya askari hao jamii wanaoshirikiana a askari wa jeshi la polisi walidai waliwakuta wasichana hao wamevaa nusu uchi na kuwasimamisha kwa kuwa wao walikuwa lindo kusaka waharifu wapitao majira hayo.


Walidai kuwa walipotakiwa kusimama walionekana kukaidi na kutaka kuondoka bila kutambua watu hao walikuwa katika lindo.


Hivyo walipoonekana kubisha zaidi wanalindo hao waliwabeba kwa nguvu na ndipo nguo zao zilipochanikia kwa kuwa walikuwa wakaidi kwenda kituoni cha polisi kwa mahojiano.

Mmoja wa askari hao aliokuwa eneo la tukio alidai wasichana hao baada ya kutakiwa kwenda kituo cha polisi walifungua mikoba yao na kutoa magauni marefu kutak kuvaa maarufu kama Madera na kuzuiliwa wafike hivyo hivyo kituoni.


JEshi la polisi wameunda vikosi maalum vya mitaani vya ulinzi vinavyojulikana polisi jamii ewanaoshirikana na askari kukamata waharifu mitaani.

ATUPWA JELA KWA KUFANYA MAPENZI NA MWANAFUNZI

MWANAMKE Sophia Philemon [44] ambaye ni mama wa watoto watatu, amehukumiwa kwenda kutumikia kifungo cha miaka saba jela baada ya kupatikana na hatia ya kufanya mapenzi na mwanafunzi chini ya miaka 18. Mwanamke huyo mkazi wa wilayani Moshi vijijini alifanya mapenzi na mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Langasani mwenye umri wa miaka 15 bila kutambua anatenda kosa kisheria.

Hukumu hiyo takatifu, ilitolewa jana na Kaimu Hakimu Mkazi Mfawidhi John Nkwabi wa Mahakama ya Mkoa Kilimanjaro, John Nkwabi baada ya kuridhika na ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa mashitaka.

Nkwabi alisema ameridhika na ushahidi uliotolewa akiwemo na mwanafunzi huyo umeithibitishia mahakama pasipo shaka yoyote na mahakama imeridhika na ushahidi huo.

Nkwabi alisema kitendo alichokifanya mwanamke huyo cha kumlazimisha kijana huyo kufanya nae tendo la ndoa ni kosa chini ya kifungu namba 138B (1) (d) cha kanuni ya adhabu kinachosimamia makosa ya kimapenzi kwa watoto baada ya sheria hiyo kufanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Awali hati ya mashitaka ilionyesha kuwa, Februari 28, mwaka jana, saa 1:00 usiku, huko katika kambi namba tisa katika nyumba za sukari wilayani Moshi vijijini, mshitakiwa alimlazimisha mwanafunzi huyo kufanya naye mapenzi katika chumba anachoishi na mumewe.

Ilidaiwa kuwa muda huo mwanafunzi huyo alikuwa ametoka dukani alikokuwa ametumwa na wazazi wake na mwanamke huyo alimwita na kumshawishi aingie ndani ya nyumba yake anapoishi na mumewe na baadaye kumlazimisha kufanya naye tendo la ndoa.

Sophia ni mke wa mtu na ni mama wa watoto watatu ambao wawili wa kike na mmoja ni wa kiume.

Tuesday, March 23, 2010

TANZANIA DISAPOINTED OVER CITES REJECTION ON IVORY SALE BID



THE government has expressed its disappointment over the decision by the Convention on International Trade in Endangered Species (CITES) to reject its plea to sale 100 tonnes of stockpiled ivory while blaming Kenya for spearheading negative propaganda.

The Permanent Secretary in the Ministry of Natural Resources and Tourism, Dr Ladislous Komba, said that the government was therefore planning to renew the request, saying that misinformation had failed the proposal.

“We were right and confident but what happened is that Kenya spearheaded negative campaign and all other nations relied on wrong information from Kenya and that is why the conclusions were not in our favour,” he said.

Dr Komba noted that the country was doing better in preventing elephants from being killed and that could be proven by the fact that it has a big population of elephants than any other country in the Southern and Central Africa.

Last Saturday the government blasted the CITES Secretariat for its report on the Tanzania's wildlife survey, saying it was biased, inadequate and incorrect, hence unsatisfactory.

Reports say that the 175-national convection also rejected a similar proposal from Zambia to sell off its ivory stocks which were considered later in the day (yesterday).

The Minister for Natural Resources and Tourism, Ms Shamsa Mwangunga, said earlier that the country is committed to conservation of its wildlife including elephants. Ms Mwangunga noted that the government planned to use proceeds from the trade for strengthening anti-poaching activities.

She argued that elephant population had reached the point where they were trampling crops and killing too many people. The proposal also said preventing selling of the stocks which come from natural deaths or controlled culling of problem animals would increase anger toward the beasts that are seen increasingly as pests by affected communities.

The country was asking to sell almost 90,000 kilogrammes of its stockpiled ivory that would have generated as much as 20 million US dollars (over 23bn/-). It was noted in the proposal that the elephant population has risen from 55,000 in 1989 to 110,000 last year.

The neighbouring Kenya and six other African countries, proposed a halt in what limited international trade in ivory is currently allowed and a 20-year moratorium on any attempts to relax international trade controls on African elephant ivory.

Opponents led by the United States, the European Union and several central and west African countries say the country has not done enough to combat poaching and slow the illegal trade in ivory.

They also wanted more time to assess whether a 2008 ivory sale by Zimbabwe, Botswana, South Africa, Namibia had contributed to the illegal trade. Ivory sales have in recent years been among the most contentious proposals at CITES and this time around African countries, and even some environmental groups, are divided.

The ivory would be sold to China and Japan — the only countries which have asked to purchase it. The proposal would have been the third ivory sale following ones in 1999 and 2008.

TRANSPORT IN DAR ES SALAAM REMAINS A MAJOR CHALLENGE FOR STUDENTS


A TRAFFIC policeman (centre) helps students to board a commuter bus, daladala, at the Kivukoni Bus Stop in Dar es Salaam this noon. The students, who had finished their day at school, had to wait for several hours pleading with conductors to let them into the buses.

WANAFUNZI WA CHUO CHA IFM DAR ES SALAAM WAGOMA KUPIGA ONGEZEKO LA ADA



WANAFUNZI wa Shahada ya kwanza na ya pili katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha [IFM] jana waligoma kueneelea na masomo kutokana a ongezeko la ada lililipanda ghafla. Wanafunzi hao jan waligoma kuenela na masomo na kuweka migomo baada kupinga ongezeko la ada zaidi ya asilimia hamisini chuoni hapo.

Wanafunzi hao walionekana kutka kuandama kwend kutaka kumuona mfadhili wea chuo hicho Waziri wea Fedha ili weakamueleze tatizo hilo kama ana taarifa nalo.

WAnafunzid hao waliweka mgomo huo baada ya kutopata majibu ya maokeo ya mitihani baada ya kuambiwa hadi wamalize ada na kushangazwa na kauli hiyo.

Wanafunzi hao walidai kuwa ada zimepand kutoka shulingi milioni moja hadi kufika milioni moja na laki sita jambo ambalo limewshangaza kupanda kwa ada hizo bila ya kupewa taarifa rasmi.

AKATAA ZAWADI YA SHILINGI BILIONI 1.3


Akataa Zawadi ya Tsh. Bilioni 1.3

Mwanaume wa nchini Urusi ambaye anaishi maisha ya kifukara katika nyumba yake iliyojaa mende kibao, amekataa zawadi ya dola milioni moja aliyopewa baada ya kulipatia jibu fumbo la hesabu lililowashinda wataalamu wa mahesabu kwa miaka 100. "Nimetosheka na kile nilicho nacho", alisema Dr Grigory Perelman, 44, mwanaume anayesemekana kuwa yeye ndiye Genius wa hisabati kwani yeye ndiye mtu pekee aliyefanikiwa kulifumbua fumbo la hisabati linaloitwa "Poincare Conjecture" ambalo wanahisabati wote duniani kwa kushirikiana walishindwa kulifumbua fumbo hilo lenye miaka 100.

Dr Grigory Perelman anaishi mjini Petersburg katika nyumba yake ambayo imejaa mende wengi sana kiasi cha majirani zake kutoa malalamiko kuwa mende hawaishi kuingia kwenye nyumba zao toka kwenye nyumba ya mtaalamu huyo wa hisabati.

Dr. Perelman nyumbani kwake ana meza moja, stuli moja na kitanda chenye godoro chafu lililochakaa lililoachwa na wamiliki wa nyumba hiyo ambao walikuwa walevi kupindukia ambao ndio waliomuuzia Dr.Perelman nyumba hiyo.

Pamoja na maisha anayoishi, Dr. Perelman ameikataa zawadi ya dola milioni moja aliyopewa na taasisi ya hisabati ya Marekani akisema kuwa hana shida ya pesa ametosheka na alichonacho.

Miaka minne iliyopita, Dr. Perelman alikataa kwenda kuichukua tuzo maalumu aliyotunukiwa na umoja wa kimataifa wa wanahisabati kwa kulipatia jibu swali hilo gumu la hisabati.

Wakati huo Dr. Perelman alisema "Sina shida ya pesa wala umaarufu, sitaki nionyeshwe kwa watu kama vile wanyama kwenye bustani za wanyama".

"Mimi sio shujaa wa hisabati, sijafanikiwa kwa kiasi hicho ninachoongelewa, na hivyo sitaki watu wote wawe wananiangalia mimi", alisema Dr. Perelman.

Ilikuwa ni mwaka 2002 wakati Dr. Perelman alipokuwa akifanya kazi kwenye taasisi ya utafiti wa hisabati nchini Urusi wakati alipoanza kutuma majibu kwenye internet ya fumbo la Poincare Conjecture ambalo ni miongoni mwa mafumbo saba magumu ambayo kila fumbo moja limetengewa zawadi ya dola milioni moja kwa mtu atakayelipatia jibu.

Kupatikana kwa jibu la fumbo la Poincare Conjecture kutawawezesha wanasayansi kuweza kujua umbile la ulimwengu.

Mwaka 2003 Dr. Perelman aliacha kazi kwenye taasisi hiyo ya utafiti wa hisabati na inadaiwa na marafiki zake kuwa ameachana kabisa na masuala ya hisabati.

KAHABA AFRIKA KUSINI ASHTAKI BAADA YA KUSIMAMISHWA KUSIMAMISHWA KAZI ZAKE



ngawa ni kinyume cha sheria kufanya ukahaba, Kahaba mmoja nchini Afrika Kusini ameenda mahakamani kupinga kusimamishwa kazi isivyo halali kwenye danguro moja lililopo mjini Cape Town. Kahaba huyo anayejulikana kwa jina la Kylie alisimamishwa kazi kutokana na tabia yake ya kuchagua wateja na kutumia muda mwingi na mpenzi wake ambaye alikuwa hataki kulipa kwa huduma ya ngono anayopewa.

Jaji wa kesi alishikwa na butwaa akisema kuwa haamini inakuwaje mtu anayefanya kazi haramu akaenda mahakamani kuitetea kazi haramu anayofanya.

Hata hivyo wanasheria wa Kylie wanasema kuwa kesi ya Kylie si kuhusiana na kufanya kwake ukhaba ambao ni kinyume cha sheria bali ni kufukuzwa kwake kazi isivyo halali.

Mahakama kadhaa za nchini Afrika Kusini zimekataa kuisikiliza kesi hiyo zikisema kuwa kufanya ukahaba ni kinyume cha sheria, vimeripoti vyombo vya habari vya Afrika Kusini.

Majaji watatu wa mahakama ya kazi wanakuna vichwa vyao kujua kama waisikilize kesi hiyo au la.

"Wakati unaposimamishwa kufanya kitu haramu.. haiingii akilini kusimama na kupigania watu wakurudishe kufanya kazi ya haramu", alisema rais wa majaji, Raymond Zondo.

Kylie amekuwa akipigania kurudishwa kwenye kazi yake haramu kwa miaka saba sasa tangia aliposimamishwa kazi mwaka 2003.

WA State African Community Leadership Conference

Invitation to the 1st annual Washington State African Communities Leadership Conference 2010 on March 27, 2010


Dear Brothers and Sisters, Greetings:
I hope this letter finds you and yours well!

It gives me great pleasure in inviting you on behalf of the African Affairs Council of Washington State (AACWA) to the 1st annual Washington State African Communities Leadership Conference 2010 to be held at St. John’s Episcopal Church in Olympia (114 20th Ave SE, Olympia WA 98501-2999) on March 27, 2010 from 09:30 a.m. to 4:30 p.m.

=====================================

THE AFRICAN AFFAIRS COUNCIL OF WASHINGTON STATE

A Non Profit Corporation

WASHINGTON STATE AFRICAN COMMUNITIES

LEADERSHIP CONFERENCE 2010

Saturday March 27th 2010

Saint John’s Episcopal Church, Olympia, Washington

AGENDA
9:30 Registration

10:00 Welcome and breakfast

AM SESSION

10:30 Introduction of the upcoming A DAY FOR AFRICA

September 17th&18th 2010 in Tumwater

11:00 Brainstorming – A DAY FOR AFRICA – activities, events

11:50 BREAK

12:00 Activity prioritization, organization and program development

and responsibility assignments

13:15 NETWORKING / PRAYER BREAK

13:30 Lunch

PM SESSION

14:00 THE AFRICAN COMMUNITIES IN WASHINGTON STATE

15:45 Break and networking

16:00 Questions & answers from participants

16:30 End of Conference

Monday, March 22, 2010

MGOMO WA WAFANYA KAZI TANZANIA

SHIRIKISHO la Vyama vya wafanyakazi nchini {TUCTA] umetangaza mgomo utakaofanyika nchi nzima kuaninzia Mei 5, mwaka huu kupinga mambo mbalimbali serikalini. Nacho Chama cha Walimu Tanzania [CWT] umeunga mgomo huo na umesema utashiriki ipasavyo na wameheshimu kauli ya tucta kwa kuwa ina nguvu na wanakusudia kugoma hadi hapo haki zao zitakapotekelezwa ipasavyo.

Rais wa CWT, Gratian Mukoba amesema kwa sasa anatoa taarifa kwa walimu wote nchini na wanatakiwa wafahamu kuwa chama chao kimeitikia wito wa kushiriki kwenye mgomo wa kudai mambo mbalimbali ambayo serikali imeyadharau kwa muda mrefu.

Aliongeza kuwa viongozi wa vyama vyote wamekubaliana kuwatangazia wanachama wao kuhusu mgomo huo ili washirikiane kudai haki zao chini ya mwavuli wa Tucta.

Mgomo huo unakusudia madai ya mishahara duni isiyokidhi mahitaji, mafao duni ya wastaafu kutoka kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na ulipishwaji wa kodi kubwa kwenye mishahara midogo wanayopata wafanyakazi.

Tucta imedai kuwa siku ya kusherehekea sikukuu ya wafanyakazi Mei Mosi watajadili kindani jinsi ya kuanza kufanya mgomo huo kwa kuw wafanyakazi wote hukutana siku hiyo.

BIBI CINHTIA NI MWANAMKE ALIYEIBIWA MME WAKE AENDA KUSHTAKI MAHAKAMANI NAKULIPWA FIDIA YA DOLLA MILIONI 9


Mwanamke wa nchini Marekani aliyemfikisha mahakamani mwanamke aliyempora mumewe, ameshinda kesi aliyomfungulia mwanamke huyo kwa kumuibia mumewe na atalipwa fidia ya dola milioni 9. Cynthia Shackelford mwenye umri wa miaka 60 aliiambia mahakama ya North Carolina kuwa aliacha kazi yake ya ualimu ili kulea watoto na kumsaidia mumewe Allan katika kuziendeleza shughuli zake za kisheria.

Kwa kutumia kipengele cha sheria ambacho huwa hakitumiki sana, Bi Cynthia alisema kuwa mumwe alikuwa ni mtu mwenye furaha na mwenye kuonyesha mapenzi kwake kabla ya bi Anne Lundquist, 49, kuuingilia uhusiano wao na kuanza uhusiano na mumewe.

Baada ya siku mbili za kuisikiliza kesi hiyo, majaji waliamuru bi Cynthia alipwe fidia ya dola milioni 9 baada ya bi Cynthia kuithibitishia mahakama jinsi mapenzi yao yalivyokuwa motomoto kabla ya Anne kuanza uhusiano na mumewe.

Mahakama ilitaka bi Cynthia alipwe fidia kwa kitendo cha mumewe kutembea nje ya ndoa yao na kumuumiza kihisia bi Cynthia.

Anne ambaye hivi sasa anaishi na Allan, alisema kuwa atakata rufaa kupinga hukumu hiyo akidai kuwa alianza uhusiano na Allan baada ya ndoa ya Allan na mkewe kuvunjika.

Jimbo la North Carolina ni miongoni mwa majimbo machache ya Marekani ambayo yanaruhusu wanandoa kuwafikisha mahakamani wenzao wanaozisaliti ndoa zao.

A VICTORY FOR THE AMERICAN PEOPLE


The passage of health insurance reform legislation represents a historic victory for the American people. America's families and businesses will not only get relief from skyrocketing health care costs but will now have more control over their health care. No longer will the insurance companies get the final say when it comes to rates and rights.

Health Reform

  • Reduce long-term growth of health care costs for businesses and government
  • Protect families from bankruptcy or debt because of health care costs
  • Guarantee choice of doctors and health plans
  • Invest in prevention and wellness
  • Improve patient safety and quality of care
  • Assure affordable, quality health coverage for all Americans
  • Maintain coverage when you change or lose your job
  • End barriers to coverage for people with pre-existing medical conditions

Health Reform & the Budget

“Under this budget, we will provide the health and human services that Americans depend on more effectively, slashing waste and focusing programs on results.”
-- Secretary Sebelius

The President’s budget helps build the foundation for health insurance reform. The budget strengthens the health care system and improves access to care by investing $995 million to address the shortage of health care providers in underserved areas, increasing funding to expand services at Health Centers by $290 million and allocating nearly $80 million for work to spread the adoption and use of health information technology.

Read the President’s Budget

Get Health Insurance
Reform Updates

Families across the country have seen their health insurance premiums skyrocket, with one insurance company promising increases of up to 39 percent in the months ahead. Health insurance reform will give families the relief they need and ensure Americans have secure, stable, affordable health insurance. Sign up here to get the latest information about rising health insurance premiums and the latest on efforts to reform the system.


ASKOFU KAKOBE BADO VITANI NA SERIKALI



kuonesha Serikali ipo katika juhudi za kuboresha huduma za nishati ya umeme nchini, jana mabango la Kanisa la Full Gospel Fellowship linaloonyehsa na kuwaelekeza watu kufika kanisani hapo limetolewa na mafundi wa Tanesco chini ya ulinzi mkali wa polisi.

Mabango hayo mawili yalisimikwa nje ya kanisa la Full Gospel Bibilia Fellowship(FGBFC) Linaliongozwa na askof Zakaria kakobe Jijini Dar es Salaam.

Mbali na kuondolewa mabango hayo pia askofu huyo ametakiwa na serikali kwa kupitia wakala wa barabara nchini (TANROAD)kuwajibika kulipa gharama za uondoaji wa mabango hayo kutokana na kuchelewa kufanya kazi hiyo kama alivyoelekezwa'

Mabango hayo yaliondolewa baada ya kudai kuwa mabango hayo yapo kwenye njia ya mradi wa umeme wa magawati 1332 na ni lazima yangetolewa kupisha mradi huo na kanisa hilo limetakiwa kuwajibika kulipa gharama hizo kwa kuwa yamechelewesha kazi ya utandazaji wa waya za umeme huo,amabapo kazi hiyo ilipangwakukamilika machi 15,mwaka huu.
Hata hivyo wakati kazi hiyo ukiendelea askofu kakobe na waumini wake hawakushiriki zoezi lake na walijifungia kanisani wakifanya maombi



MAKONTENA YA BIDAA BANDIA YAKAMAKWA BANDARINI DAR


Shehena ya makontena 20 za betri aina ya tiger head kutoka China zimekamatwa kutokana na kukosa ubora wa viwango vya matumizi ya bidaa hiyo.
Kontena hizo zimekamatwa katika operesheni ya Shirika la viwango nchini (TBS) katika kukagua bidaa ziingiazo nchini ambazo hazina viwango vya matumzi.
Mkurugenzi Mkuu wa TBS nchini Charles Ekerege alisema shehena walioyakamata ya betri hizo ilifika nchini januari mwaka huu, lakini walipozikagua waligundua kuwa hazina ubora uliowekwa na shirika hilo.
Alisema betri hizo zinaingizwa nchini na wafanya biashara wakubwa na wakati mwingine imedaiwa kuwa wanaziingiza kwa njia ya panya.

Alisema betri hizo huingizwa nhini na huuzwa kwa bei za rejareja shilingi 350 na zinazotengenezwa hapa nchini huuzwa kwa shilingi 450 kila moja na watanzania wengu hukimbilia betri hizo kutokana na unafuu wa bei.

SKENDO ZA VATICAN


Papa Benedict XVI ametoa tamko rasmi la kuwaomba radhi wahanga wa skendo la wachungaji kuwalawiti na kuwanyanyasa kijinsia watoto waliokuwa wakienda kanisani. Skendo hilo limeyakumba makanisa ya kanisa katoliki katika nchi mbali mbali duniani lakini Ireland ndio iliyotajwa zaidi kwa idadi kubwa ya watoto walionyanyaswa kijinsia na wachungaji huku kanisa katoliki nchini Ireland likifunika maovu ya wachungaji wake ili kanisa lisiharibiwe sifa yake.

"Najua mmenyanyasika sana na kufanyiwa ukatili na nawaomba radhi sana wote waliokumbwa na maovu haya", alisema Papa katika taarifa yake kwa makanisa ya Ireland.

"Najua hakuna kitu kinachoweza kuuondosha uovu mliofanyiwa, Imani zenu kwa kanisa zimesalitiwa".

"Sote tumekumbwa na skendo linalotokana madhambi ya baadhi ya wadau wa kanisa".

"Madhambi makubwa yamefanyika dhidi ya watoto wasio na utetezi wowote".

"Najua baadhi yenu mnaona ni vigumu hata kuingia tena kwenye milango ya kanisa baada ya yote haya yaliyotokea", aliendelea kusema Papa Benedict.

Kwa miaka zaidi ya 10 wachungaji na viongozi wa kanisa wameharibu imani za watu ndani ya kanisa, alisema Papa katika taarifa yake ambayo itasomwa kwenye makanisa karibia yote nchini Ireland wakati wa misa ya jumapili.

Maskendo ya ngono yanayowahusisha wachungaji na watoto wa kiume yamekuwa yakiripotiwa katika nchi mbali mbali duniani huku nchi zilizokumbwa zaidi na maskendo hayo zikitajwa kuwa ni Austria, Uswizi, Uholanzi, Brazil, Mexico na hata dayosisi ya kanisa la zamani la Papa nchini Ujerumani imo kwenye skendo hilo.

Papa alisema kuwa miaka ya kuficha maovu ya wachungaji waovu imeisha na ametaka wachungaji watakaogundulika kuendeleza maovu yao waripotiwe polisi.

Papa aliongeza kuwa katika miaka iliyopita ameishakutana na baadhi ya wahanga wa skendo hilo kutoka nchi mbalimbali duniani na anatarajia kufanya hivyo tena baadae.