WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Sunday, April 11, 2010

ONLINE CHATING YASABABISHA AMUUE MKEWE


Mwanaume mmoja nchini Jordan anashikiliwa na polisi baada ya kumuua mkewe miezi sita baaa ya ndoa yao akidai kuwa alimfumania akichat online na mwanaume mwingine.
Mtuhumiwa alimkaba koo mkewe mwenye umri wa miaka 37 kabla ya kukipasua kwa nyundo kichwa chake na kisha kujaribu kuutupa mwili wake”, alisema msemaji wa polisi.

“Alijaribu kuuchoma moto mwili wake lakini alishindwa. Alidai kuwa mkewe alikuwa na tabia mbaya ya kuchat na mwanaume kwenye internet”, aliendelea kusema msemaji huyo wa polisi.

Mtuhumiwa huyo ambaye ana umri wa miaka 30 anashikiliwa na polisi na anakabiliwa na adhabu ya kifo.

”Baada ya mauaji alitoa taarifa kwa wakwe zake kuwa mkewe amepotea na hajui alipo wakati huo huo watu wengine wawili walienda kutoa taarifa polisi”, alisema msemaji wa polisi.

Lakini hata hivyo kutokana na taarifa zake za utatanishi polisi walimhisi yeye ndiye aliyefanya mauaji ya mkewe.

Baada ya kubanwa sana na polisi mwanaume huyo aliamua kukiri kumuua mkewe akisema kuwa alikuwa hapendi tabia ya mkewe kuchat na mwanaume kwenye internet.

AJALI YA NDEGE YAUA WENGI PAMOJA RAIS WA POLAND



VIDEO - Ndege Yadondoka Rais Wa Poland Afariki
Ndege aliyokuwemo rais wa Poland na mkewe pamoja na maafisa wa serikali yake.

Rais wa Poland, Lech Kaczynski pamoja na mkewe na maafisa wa jeshi na serikali wamefariki dunia baada ya ndege iliyokuwa imebeba abiria 132 kuanguka karibu na uwanja wa ndege nchini Urusi.
Rais Lech Kaczynski wa Poland amefariki dunia kufuatia ajali mbaya ya ndege iliyotokea leo baada ya ndege yake kuanguka kwenye miti karibu na uwanja wa ndege wa Smolensk nchini Urusi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, abiria waote 132 waliokuwemo kwenye ndege hiyo wamefariki dunia.

Miongoni mwa wwaliofariki katika ajali hiyo ni mke wa rais huyo, Maria, Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Andrzej Kremer, Mkuu wa majeshi ya Poland, Franciszek Gagor, na Gavana wa Benki Kuu ya nchi hiyo, Slawomir Skrzypek.

Pia katika orodha ya watu waliofariki kutokana na ajali hiyo ya ndege ni wabunge wa Poland na wanahistoria kadhaa.

Rais huyo wa Poland pamoja na ujumbe wake walikuwa wakielekea katika mji wa Katyn karibu na Smolensk kuhudhuria kumbukumbu ya mauaji ya wafungwa wa vita wa Urusi na Poland waliouawa wakati wa utawala wa kisovieti.

Kufuatia kifo hicho, Spika wa bunge la Poland, Bronislaw Komorowski, anachukua madaraka ya nchi hiyo.

Rais Kaczynsk na mkewe ambao wote wamefariki katika ajali hiyo wameacha mtoto mmoja wa kike, Marta.