Saturday, April 3, 2010
KIKWETE AWAOMBA WAFANYA KAZI NCHINI WASITISHE MGOMO
RAIS wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amewaomba wafanyakazi wote nchini kusitisha mgomo ambao wameuandaa kupitia shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi na kuwaahidi madai hayo yatafanyiwa kazi.
Rai hiyo ameitoa jana katika hotuba yake ya kila mwisho wa mwezi ya kungea na wananchi kwa kupitia njia ya vyombo vya habari vyfote nchini.
Ameitaka TUCTA kufikiri zaidi uamuzi huo na kusema mgomo huo utaathiri katika nyanja zote nchini.
Pia amekiri inamuwia vigumu kuzungumzia migomo hiyo kwa wakati na ameeleza kuwa serikali haipuuzi madai ya wafanyakazi wanawajali na wanawathamini.
Hivyo ameitaka TUCTA kukubali kufanya mazungumzo na serikali na waajiri wengine ili kumaliza mgogoro huo ambao hautajenga nchi bali itabomoa.
Mgomo huo unatarajiwa kuanza Mei 5, mweaka huu ambao unalenga mgomo wea wafanyakazi wote nchini kudai madai dambayo hayatekelezwi kwa muda mrefu na serikali.
Tayari vyama kadhaa vinavyounda shirikisho hilo vimeshatangaza kuunga mkono mgomo huo, ambao Kikwete amesema kama utafanyika "shughuli zote nchini zinazofanywa na watu walioajiriwa zitasimama kwa muda usiojulikana kuanzia siku hiyo".
TUCTA inataka siku hiyo watu wote walioajiriwa wagome na kwa muda usiojulikana. Tamko hilo linawahusu wafanyakazi wa umma serikalini na katika mashirika ya umma pamoja na wafanyakazi wa sekta binafsi walioajiriwa popote pale mashambani, maofisini, viwandani, majumbani, mahotelini na madereva.
MCHUNGAJI CHA POMBE ASABABISHA KASHESHE MAKABURINI
Askofu wa kanisa katoliki nchini Ufaransa ameomba radhi kufuatia kitendo cha mchungaji mmoja wa kanisa hilo kuongoza mazishi makaburini akiwa amelewa na kumtwanga ngumi ya uso mmoja wa waombelezaji.
"Mchungaji Bonaventure aliwasili makaburini akiwa amelewa katika hali ambayo haiendani na tararibu za kanisa", alisema askofu Robert le Gall katika taarifa yake ya kuwaomba radhi familia ya marehemu.
Ndugu wa mwanamke aliyefariki walielezea jinsi walivyomtaka mchungaji huyo ambaye ni raia wa Burkina Faso kuwa hawataki aongoze misa ya mazishi ya ndugu yao kwakuwa alikuwa amelewa sana.
Katika mazishi hayo yaliyofanyika siku ya jumanne katika mji wa Toulouse uliopo kusini magharibi mwa Ufaransa, mchungaji huyo alikubali kuondoka lakini alipotaka kuendesha gari lake mwenyewe, ndugu wa marehemu walijaribu kumzuia kwakuwa alikuwa hajiwezi hata kutembea akianguka chini mara kwa mara.
Kuna wakati mchungaji huyo alidondoka chini na mmoja wa waombelezaji alipojitolea kumuinua mchungaji huyo alimtandika ngumi ya uso, alisema Gerard Tillier ambaye ni kaka wa marehemu.
"Mchungaji gani huyu anakuja kwenye mazishi akiwa amelewa na kuwapiga ngumi waumini wake? ", alisema kaka huyo wa marehemu.
Subscribe to:
Posts (Atom)