WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Friday, April 16, 2010

OSAMA BIN LADEN ATISHIA USALAMA KOMBE LA DUNIA


Kundi la Al-Qaeda linaloongozwa na Osama Bin Laden limetishia usalama kwenye kombe la dunia nchini Afrika kwa kuahidi kufanya shambulizi la kigaidi litakaloua mamia ya watu wakati wa mechi kati ya Marekani na Uingereza.
Kundi la Al-Qaeda limetishia kuwaua mamia ya watu watakaohudhuria mechi kati ya Marekani na Uingereza kwenye kombe la dunia nchini Afrika Kusini mwezi juni mwaka huu.

Kundi linalojiita Al-Qaeda in the Islamic Maghreb, limetoa taarifa kwenye website likisema kuwa watu wa kujitoa mhanga wakiwa na mabomu ambayo si rahisi kugundulika kwenye mitambo ya ulinzi, wako tayari kujilipua kwenye mechi kati ya Uingereza na Marekani kwenye uwanja wa Rustenburg juni 12 mwaka huu.

Kundi hilo liliweka taarifa hiyo kwenye tovuti inayoitwa "Mushtaqun Lel Jannah" (Njia ya kuelekea peponi).

"Al-Qaeda watakuwepo kwenye mechi za kombe la dunia", ilisema taarifa hiyo ya Al-Qaeda.

"Litakuwa ni jambo la kufurahisha sana wakati wa mechi kati ya Marekani na Uingereza ikirushwa live kwenye luninga wakati sauti ya mlipuko itakaposikika kwenye majukwaa na kuugeuza uwanja mzima juu chini", iliendelea kusema taarifa hiyo ya Al-Qaeda.

Uingereza na Marekani zipo kwenye kundi moja la C pamoja na Algeria na watapimana ubavu juni 12 kwenye uwanja wa King Bafokeng mjini Rustenburg unaochukua watazamaji 44,500.

Maafisa wa Marekani wamesema kuwa vitisho hivyo vya Al-Qaeda vinachukuliwa kwa uangalifu mkubwa katika kuhakikisha usalama kwenye fainali hizo za kombe la dunia zitakazochukua mwezi mmoja.

Maafisa wa usalama wa Uingereza wamekataa kusema chochote.

Mwezi oktoba mwaka jana, maafisa wa usalama wa Afrika Kusini walisema kuwa wamefanikiwa kulizima jaribio la shambulizi la kigaidi lililokuwa limepangwa lifanyike wakati wa fainali hizo.

Iliripotiwa kuwa maafisa wa Afrika Kusini kwa kushirikiana na maafisa wa Marekani walifanikiwa kuwatia mbaroni watu wanaodaiwa kuwa ni wanachama wa Al-Qaeda nchini Somalia na Msumbiji ambao walikuwa wakijiandaa kufanya shambulizi wakati wa fainali za kombe la dunia.

Serikali ya Afrika Kusini imetangaza kuwa jumla ya polisi 44,000 watalinda usalama kwenye fainali hizo.

WATU 10 WAFARIKI DUNIA BAADA YA MTUMBUI KUPINDUKA

WATU kumi wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kutoka nchini Msumbiji kupinduka katikati ya Mto Ruvuma.
Ajali hiyo ya kusikitisha ilitokea jana , majira ya saa 7:00 mchana katika Kijiji cha Kiromba Mtwara.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mtwara, Steven Buyuya alisema watu hao walikuwa wakirejea kutoka Msumbiji ambako walikuwa wakitoka katika shughuli zao za kilimo na walipofika eneo hilo upepo mkali uliwakumba na kupoteza mwelekeo na mtumbwi huo ukazama majini.


Kamanda alisema mtumbwi huo ulikuwa umebeba abiria 12 na walionusurika ni nahodha na abiria mmoja ambao ni Idrisa Nkerewe aliyekuwa nahodha na Abdallah Kaisi, 32 abiria

Alisema kuwa tayari miili ya watu watatu imeshapatikana na majina na maeneo wanapoishi yametambulika.

MTU MWENYA BAHATI MBAYA KULIKO WOTE NCHINI UINGEREZA


Mkulima wa nchini Uingereza Mick Wilary ambaye anadaiwa kuwa ndiye mtu mwenye bahati mbaya kuliko wote nchini Uingereza kutokana na ajali kibao zinazomkumba, amepata ajali kwa mara nyingine tena iliyoivunja miguu yake yote miwili.
Mick Wilary, mwenye umri wa miaka 58 anadaiwa kuwa ndiye mtu ambaye hana tabasamu kutokana na bahati mbaya zinazomkumba na kumfanya akumbwe na ajali mbaya zinazoyatia maisha yake hatarini.

Mick ameishakumbwa na ajali mbaya zaidi ya 30 na ajali hizo zimepelekea kuvunjika kwa mifupa ya viungo vyake 15.

Katika tukio la hivi karibuni, Mick anaendelea kupatiwa matibabu hospitalini baada ya miguu yake kupondwa na tingatinga.

Katika tukio hilo dereva wa tingatinga akiliendesha tingatinga hilo modeli ya JCB bila ya kuwa mwangalifu, alimgonga Mick na kumbamiza ukutani.

Katika tukio hilo mguu wa kushoto wa Mick ulivunjika na kupinda kuelekea mabegani wakati mguu wake wa kulia ulijeruhiwa na kugeuka ukiangalia nyuma.

Hata hivyo pamoja na ajali hiyo mbaya ya kutisha, madaktari katika hospitali ya Newcastle wamefanikiwa kuiokoa miguu yake na wamesema kuwa ndani ya miezi sita Mick ataweza tena kuitumia miguu yake kutembea.

Ajali ya kuvunjika kwa miguu yake imetokea ikiwa ni miezi michache baada ya kuvunjika kwa enka za miguu yake yote miwili baada ya kuteleza na kuanguka chini alipokanyaga kiazi mviringo.

Miongoni mwa ajali mbaya zilizowahi kumkumba Mick ni kupasuka kwa fuvu la kichwa chake kwenye sakafu alipopigwa mweleka na paka.

Mick pia ameishawahi kuvunjika mbavu, shingo na mikono katika mfululizo wa ajali mbaya zinazoendelea kumkumba ambazo zimeifanya sura yake ikose tabasamu wakati wote.

AZINDUKA TOKA KWENYE KOMA NA KUANZA KUZUNGUMZA KIJERUMANI


Msichana mmoja wa nchini Croatia amewashangaza watu wengi baada ya kuzinduka toka kwenye koma baada ya kupoteza fahamu kwa masaa kadhaa akiwa ameisahau kabisa lugha yake halisi na kuanza kubonga kijerumani kama vile alizaliwa nacho.
Msichana huyo ambaye alipoteza fahamu kwa masaa 24 wiki mbili zilizopita, amewaacha madaktari wakiumiza vichwa kutokana na hali aliyo nayo.

Msichana huyo alizinduka akiwa ameisahau kabisa lugha yake ya Croatia na kuanza kuzungumza kijerumani fasaha kama vile alizaliwa nacho.

Wazazi wake walisema kuwa msichana huyo alikuwa akijifunza kijerumani shuleni na pia akiangalia shoo za kijerumani kwenye luninga lakini kijerumani kilikuwa hakipandi kabisa akishindwa hata kuziunga sentesi kifasaha.

"Huwezi kujua ukizinduka toka kwenye koma ubongo utakuwa katika hali gani", alinukuliwa mkurugenzi wa hospitali ya KB Hospital ambayo msichana huyo alikuwa amelazwa.

Madaktari kadhaa wamejaribu kumfanyia uchunguzi msichana huyo lakini wameshindwa kujua chanzo cha hali iliyomtokea.