WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Thursday, May 6, 2010

VIDEO YA WATU KUKAA UCHI ETI NI SANAA HUKO MAJUU


Hii nayo inaitwa sanaa huko majuu, mamia ya watu wanawake kwa wanaume nchini AUSTRALLIA wamejitolea kukaa uchi kwenye sehemu ya hadhara ili kupiga picha za sanaa kwaajili ya jumba la makumbusho.
Katika kusherehekea miaka 10 ya jumba la sanaa la OPHRA mamia ya watu wanawake kwa wanaume walikusanyika kwenye bustani wakiwa uchi wa mnyama kwaajili ya kupiga picha za sanaa.

Mpiga picha wa Kimarekani, Spencer Tunick alifanikiwa kuwakusanya mamia ya watu ambao waliamua kubakia na suti zao walizozaliwa nazo wakipangwa katika staili mbalimbali ili kutengeneza picha za maumbile tofauti tofauti.

Inakadiriwa kuwa watu 5,000 wazee kwa vijana walishiriki katika zoezi hilo.

Angalia video hii chini ujionee mwenyewe hali ilivyokuwa.

KIKWETE: MSIPONIPA KURA WENGINE WATANIPA


Hii ni moja kati ya kauli alizozitoa Rais Kikwete wakati wa hotuba yake aliyoitoa juzi jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na wazee kjatika ukumbi wa Diamond Jubilee.
Rais alitoa kauli hiyo baada ya kuonekana kukerwa na viongozi wa Tucta wanaoandaa mgomo nchi nzima.

“ Mgomo huo una lengo la kuongezewa mshahara tu au kuna lingine? Alihoji rais, mimi naona mnataka kuninyima kura zenu, basi kama mmepanga hivyo mninyime tu, wengine watanipa” alisema Rais

“Mana sitaki kuwaongopea kuwa tutalipa kima hicho kama mnataka kugoma na mshahara huo kama hatutawapa basi, ninyimeni kura zenu wengine watanipigia” alisema

Pia aliwasihi wafanyakazi hao atakayegoma atakuwa amejifukuzisha kazi na kukosa haki yake ya msingi katika miaka yake aliyoitumika serikali.

Pia alisema kwa yeyote atakayefika kazini na akae na asiendelee na kazi pia atakuwa amejifukuzisha mwenyewe na hakutakuwa na msamaha na atakayethubutu kuandamana sheria itafata mkondo wake.

UTARATIBU MPYA WA KUOMBA VISA YA MAREKANI

UBALOZI wa Marekani nchini umetoa utaratibu wa maombi ya viza kwa kutumia fomu mpya za DS -160 kwa ajili ya maombi ya muda mfupi utakaoanza kutumika Mei 31, mwaka huu.
Taarifa ya balozi hiyo iliyotolewa kwenye vyombo vya habari, ilieleza kuwa waombaji wote wa viza za muda mfupi watatakiwa kujaza fomu za DS-160 zitakazopatikana kwa njia ya mtandao.

Ilisema waombaji wote wanashauriwa kuanza kutumia fomu hizo mpya bila kuchelewa ili waweze kupata viza zao.

Taarifa hiyo ilielezea kuwa Idara ya Uhamiaji na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, imeboresha fomu za DS-160 kwa waombaji wote wa viza za muda mfupi (NIV) ili kuleta mabadiliko katika fomu zinazopatikana kwenye mtandao (EVAF).

Taarifa hiyo ilisema kwua tofauti inayopatikana kwenye fomu za DS-160 ipo kwenye hatua ya kwanza ya maombi ambapo wanatakiwa kujaza kupitia mtandao.

Tovuti ambayo utaweza kupata fomu za DS-160 kwa maelezo ya hatua kwa hatua ni http://www.tanzania.usembassy.gov au wataweza kuwasiliana na Idara ya Uhamiaji kwa barua pepe: drsniv@state.gov ama kutembelea katika ofisi za balozi.

RAIS WA NIGERIA AFARIKI DUNIA



Rais wa Nigeria Umaru Yar'Adua pichani amefariki dunia Thursday, May 06, 2010 3:48 AM
Rais wa Nigeria, Alhaji Umaru Yar'Adua ambaye kiti chake cha urais kimekuwa kikikaliwa na makamu wake kwa miezi kadhaa sasa baada ya rais huyo kuugua ugonjwa wa moyo, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 58.
Kwa mujibu wa msemaji wa rais huyo ambaye hakutaka kutaja jina lake wakati akiongea na shirika la habari la BBC, alisema kwamba rais Yar'Adua amefariki dunia jana jumatano ingawa serikali ya Nigeria bado haijatoa taarifa rasmi.

Rais Yar'Adua alichaguliwa kuwa rais mwaka 2007 lakini kutokana na matatizo ya moyo na figo hajaonekana kwa wananchi wake kwa miezi kadhaa.

Baada ya rais huyo kuugua muda mrefu huku akipatiwa matibabu nchini Saudi Arabia, hatimaye makamu wa rais, Goodluck Jonathan aliteuliwa kushikilia nafasi yake mpaka rais huyo atakapopona.

Taarifa zinasema kuwa rais huyo aliiaga dunia jana jumatano kwenye villa lake nchini Nigeria kwenye majira ya kati ya saa tatu na saa nne usiku kwa saa za Tanzania.

Yar'Adua alienda Jeddah, Saudi Arabia kwaajili ya matibabu mwezi Novemba mwaka jana na alitumia miezi mingi sana huko kiasi cha wapinzani wake na viongozi wa zamani wa Nigeria kumshauri ajiuzulu.

Wakati huo Yar'Adua alimkabidhi mikoba ya urais makamu wake, Goodluck Jonathan lakini hata aliporudi toka Saudi Arabia mwezi februari mwaka huu, Goodluck Jonathan aliendelea kukikalia kiti cha urais.

Taarifa zinasema kuwa baada ya kufariki kwa rais Yar'Adua, makamu wake wa rais ataapishwa rasmi kuwa rais katika siku zijazo.