WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, April 5, 2010

KUMBUKUMBU YA KUSULUBIWA KWA YESU PHILIPINO WAIGIZA UKWELI KWA KUWAPIGILIA WATU MISUMARI YA UKWELI


Bila ya kutumia ganzi misumari ya sentimeta tano ilipigiliwa kwenye mikono na miguu ya waumini wa Kikristo katika kukumbushia kusulubiwa kwa mkombozi wa wakristo, Yesu Kristo.





Mamia ya waumini wa Kikristo nchini Philippines walitumia dakika kadhaa wakiwa kwenye maumivu makali wakati walipoadhimisha siku ya kusulubiwa kwa yesu kwa kupigiliwa misumari ya sentimeta tano kwenye miguu na mikono yao.
Bila ya kutumia ganzi misumari ya sentimeta tano ilipigiliwa kwenye mikono na miguu ya waumini wa Kikristo katika kukumbushia kusulubiwa kwa mkombozi wa wakristo, Yesu Kristo.

Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Mary-Jane Mamangun alidai kuwa hakusikia maumivu yoyote wakati misumari ya sentimeta tano ilipokuwa ikipigiliwa kwenye miguu na mikono yake.

Lakini sura yake wakati alipotundikwa msalabani ilionyesha wazi maumivu makali aliyokuwa akiyapata na alilazimika kuwahishwa kwenye hema la matibabu ambapo alipatiwa dawa za kupunguza maumivu.

Gonga linki chini kwa picha za waumini wa kikristo nchini Filipino kupigiliwa misumari.

MAAJABU YA HALF MAN KUPATA MTOTO


VIDEO - Maajabu ya Dunia - 'Mtu Nusu' Apata Mtoto
Mwanaume wa nchini Marekani maarufu kama 'Half Man' ambaye maisha yake yote amekuwa akiishi akiwa na nusu ya mwili wake tu kuanzia kiunoni ametamba kuwa yeye ndiyo baba wa mtoto wa kike aliyezaliwa na mchumba wake ingawa baadhi ya watu hawaamini kama kweli mtoto ni wake wakidai atakuwa kabambikiwa mtoto.
Kenny Easterday mwanaume wa nchini Marekani mwenye umri wa miaka 35 ambaye ana nusu mwili kuanzia kiunoni, anasubiria majibu ya DNA ili kuwathibitishia watu kuwa yeye ndio baba wa mtoto wa kike aliyezaliwa na mpenzi wake Nicky.

Katika documentary mpya itakayorushwa hewani leo kwenye televisheni ya Marekani, Kenny mkazi wa West Virginia anasema kuwa yeye ndiye baba wa mtoto Desiree aliyezaa na mpenzi wake Nicky,33 miaka saba iliyopita.

"Watu wanataka kujua kama Kenny ana sehemu za siri", alisema Nicky katika documentary hiyo itakayorushwa hewani na televisheni ya The Learning Channel (TLC).

"Tunafanya mapenzi kama watu wengine, Kenny ana sehemu za siri kama mwanaume mwingine", aliongeza Nicky.

Kenny alizaliwa akiwa na ugonjwa unaowapata watu wachache sana duniani unaoitwa sacral agenesis ambao huzuia uti wa mgongo kukua kama kawaida.

Madaktari walilazimika kuikata miguu yake miwili iliyojipinda iliyojichomoza kidogo chini ya kiuno chake na kisha kuuchukua mfupa wa ugoko wake na kuutumia kuurefusha uti wa mgongo wake.

Kenny ambaye kutembea kwake ni kwa kutumia mikono anasema kuwa ndoto yake kubwa ilikuwa ni kupata mtoto.

"Nataka niwe na mtoto atakayelibeba jina langu ambaye ataweza kusimama mbele ya watu na kusema 'HUYU NDIYO BABA YANGU'", alisema Kenny.

Angalia VIDEO hii ya kustaajabisha inayoonyesha maisha ya kila siku ya Kenny.


VIDEO - Maisha ya Kila Siku ya Nusu Mtu

BINTI WA KIZUNGU KUTENGWA NA WAZAZI KISA PENZI LA MMASAI



Binti wa Kiingereza ambaye kutokana na utajiri mkubwa wa baba yake, alizoea maisha ya kifahari akisafiri nchi mbalimbali duniani, ameangukia kwenye penzi la kijana wa kimasai nchini Kenya na kuamua kuolewa naye na kusababisha wazazi wake waamue kumtenga kupinga uamuzi wake huo.
Binti wa Kiingereza Colette Armand mwenye umri wa miaka 24 alizoea kuishi maisha ya kifahari akisafiri nchi mbali mbali na kukaa kwenye hoteli za kifahari.

Hata siku moja hakuwahi kufikiria kwamba siku moja angeangukia kwenye penzi la kijana wa kimasai anayeishi porini ambako hakuna umeme wala maji.

Baba yake Colette ni mfanyabiashara mkubwa na mkurugenzi wa kampuni moja kubwa ya madini ya nchini Uingereza wakati mama yake ni nesi katika hospitali moja nchini humo.

Mkasa wa mapenzi wa Colette ulianza miaka mitatu iliyopita wakati Colette alipoacha masomo yake ya chuo kikuu jijini Paris, Ufaransa na kuamua kuja Afrika kufanya kazi za kujitolea kwenye mashirika ya hisani.

Colette bila ya kumwambia mtu mwingine yeyote zaidi ya mama yake, ndani ya wiki moja aliacha shule na kufunga safari hadi Nairobi, Kenya kufanya kazi ya kujitolea kwenye taasisi ya watoto yatima.

Colette alitokea kupendwa kwenye taasisi hiyo ya yatima kutokana na jinsi alivyokuwa akijitolea kwa moyo wote kuwasaidia watoto yatima.

Colette alijipatia umaarufu wa ghafla baada ya mtoto wa miaka tisa aliyejulikana kwa jina la Mumbe ambaye hakuwahi kuongea hata siku moja kabla ya kuwasili kwa Colette, alipotamka neno la kwanza kumwita Colette "Mama".

Colette alijipatia umaarufu mkubwa kutokana na tukio hilo akihesabika kama mtu mwenye miujiza.

Umaarufu huo ulipelekea chifu wa kimasai Kehmini kukitembelea kituo hicho cha yatima na kumpa mwaliko Colette wa kuitembelea jamii ya wamasai.

"Nilipofika nilionyeshwa kibanda ambacho kilikuwa hakina hata mlango, kulikuwa hakuna umeme wala maji", alisema Colette.

"Usiku sikulala kabisa nikihofia nyoka wataingia ndani na kunigonga, nilikuwa nikisiliza sauti toka kila kona kuhakikisha niko salama", aliongeza Colette.

"Maji ya kuoga nayo yalikuwa ya tabu nilishindwa kuoga kwenye mto kwa kuhofia mamba. Niliamua kuchota maji na kisha kuyachemsha kabla ya kuoga".

"Hata hivyo nilitokea kupenda maisha ya kimasai, wanaume wakiondoka asubuhi kwenda kuwinda wakiacha wanawake wakilea watoto, jioni tulikusanyika pembeni ya moto na kupiga stori", alisema Colette.

Ulikuwa ni wakati huo ndipo Colette alipoangukia kwenye penzi motomoto na kijana wa kimasai Meitkini mwenye umri wa miaka 23.

Colette alimaliza miezi akiishi kwenye boma la wamasai mpaka mwaka 2008 yalipotokea machafuko ya kisiasa nchini Kenya ambapo alishauriwa na maafisa wa umoja wa mataifa arudi kwao kwakuwa maisha yake yatakuwa hatarini kutokana na rangi yake.

Colette alikata shauri atumie muda huo kurudi Uingereza kumalizia masomo yake ingawa kutokana na mapenzi aliyo nayo ilikuwa vigumu kwake kuishi mbali na Meitkini.

Colette alirudi Uingereza na kumalizia masomo yake akiwataarifu pia wazazi wake na ndugu zake uamuzi wake wa kuolewa na mmasai na kuishi kwenye boma la wamasai.

Colette hakueleweka katika familia yake na wazazi wake waliliona suala hilo kama skendo na kuamua kutotaka kulizungumzia kabisa.

Colette ingawa hivi sasa ametengwa na wazazi wake bado ameshikilia msimamo wake wa kuolewa na Meitkini na yupo kwenye hatua ya mwisho ya kumalizia maandalizi ya harusi itakayofanyika siku chache zijazo.

Kuhusiana na suala la mumewe kuongeza mke mwingine kama jadi ya wanaume wa kimasai ilivyo, Colette anasema kuwa yeye hatajali kuwa mke mwenza ingawa anaamini Meitkini hafikirii kuongeza mke mwingine zaidi yake.

Saturday, April 3, 2010

KIKWETE AWAOMBA WAFANYA KAZI NCHINI WASITISHE MGOMO



RAIS wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amewaomba wafanyakazi wote nchini kusitisha mgomo ambao wameuandaa kupitia shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi na kuwaahidi madai hayo yatafanyiwa kazi.
Rai hiyo ameitoa jana katika hotuba yake ya kila mwisho wa mwezi ya kungea na wananchi kwa kupitia njia ya vyombo vya habari vyfote nchini.

Ameitaka TUCTA kufikiri zaidi uamuzi huo na kusema mgomo huo utaathiri katika nyanja zote nchini.

Pia amekiri inamuwia vigumu kuzungumzia migomo hiyo kwa wakati na ameeleza kuwa serikali haipuuzi madai ya wafanyakazi wanawajali na wanawathamini.

Hivyo ameitaka TUCTA kukubali kufanya mazungumzo na serikali na waajiri wengine ili kumaliza mgogoro huo ambao hautajenga nchi bali itabomoa.

Mgomo huo unatarajiwa kuanza Mei 5, mweaka huu ambao unalenga mgomo wea wafanyakazi wote nchini kudai madai dambayo hayatekelezwi kwa muda mrefu na serikali.

Tayari vyama kadhaa vinavyounda shirikisho hilo vimeshatangaza kuunga mkono mgomo huo, ambao Kikwete amesema kama utafanyika "shughuli zote nchini zinazofanywa na watu walioajiriwa zitasimama kwa muda usiojulikana kuanzia siku hiyo".

TUCTA inataka siku hiyo watu wote walioajiriwa wagome na kwa muda usiojulikana. Tamko hilo linawahusu wafanyakazi wa umma serikalini na katika mashirika ya umma pamoja na wafanyakazi wa sekta binafsi walioajiriwa popote pale mashambani, maofisini, viwandani, majumbani, mahotelini na madereva.

MCHUNGAJI CHA POMBE ASABABISHA KASHESHE MAKABURINI


Askofu wa kanisa katoliki nchini Ufaransa ameomba radhi kufuatia kitendo cha mchungaji mmoja wa kanisa hilo kuongoza mazishi makaburini akiwa amelewa na kumtwanga ngumi ya uso mmoja wa waombelezaji.
"Mchungaji Bonaventure aliwasili makaburini akiwa amelewa katika hali ambayo haiendani na tararibu za kanisa", alisema askofu Robert le Gall katika taarifa yake ya kuwaomba radhi familia ya marehemu.

Ndugu wa mwanamke aliyefariki walielezea jinsi walivyomtaka mchungaji huyo ambaye ni raia wa Burkina Faso kuwa hawataki aongoze misa ya mazishi ya ndugu yao kwakuwa alikuwa amelewa sana.

Katika mazishi hayo yaliyofanyika siku ya jumanne katika mji wa Toulouse uliopo kusini magharibi mwa Ufaransa, mchungaji huyo alikubali kuondoka lakini alipotaka kuendesha gari lake mwenyewe, ndugu wa marehemu walijaribu kumzuia kwakuwa alikuwa hajiwezi hata kutembea akianguka chini mara kwa mara.

Kuna wakati mchungaji huyo alidondoka chini na mmoja wa waombelezaji alipojitolea kumuinua mchungaji huyo alimtandika ngumi ya uso, alisema Gerard Tillier ambaye ni kaka wa marehemu.

"Mchungaji gani huyu anakuja kwenye mazishi akiwa amelewa na kuwapiga ngumi waumini wake? ", alisema kaka huyo wa marehemu.

Thursday, April 1, 2010

ATUPWA JELA MIEZI 6 KWA KUMUONYESHA MWARABU KIDOLE CHA KATI



Raia wa Uingereza anayeishi Dubai huenda akatupwa jela miezi sita kwa kosa la kumtukana kwa kumuonyesha kidole cha kati mwanafunzi wa kiarabu toka Iraq.
Simon Andrews, raia wa Uingereza mwenye umri wa miaka 56 anakabiliwa na hukumu ya kwenda jela miezi sita iwapo atapatikana na hatia ya kumuonyesha kidole cha kati mwanafunzi wa urubani toka Iraq.

Gazeti la The Sun la Uingereza limeripoti kuwa Simon alishindwa kuzizuia hasira zake wakati wa ugomvi wake na mwanafunzi Mahmud Rasheed na kuamua kumtukana kwa kumuonyesha kidole cha kati.

Mahmud alikimbilia polisi kupeleka malalamiko yake na haikuchukua muda mrefu Simon alitiwa mbaroni na kufunguliwa mashtaka mahakamani.

Simon amepigwa marufuku kusafiri nje ya Dubai tangia alipotiwa mbaroni mwezi wa nane mwaka jana.

Akitoa ushahidi wake mahakamani siku ya jumapili, Simon alijitetea kuwa hakufanya kitendo hicho na kwamba raia huyo wa Iraq anamsingizia.

Mahmud hakujitokeza mahakamani kutoa ushahidi dhidi ya Simon na pia hakuna mtu aliyejitokeza kama shahidi wa kesi hiyo.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi aprili nne wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

DUKA LA KWANZA LA NGONO LA KIISLAMU LAZINDULIWA UHOLANZI



Duka la kwanza la bidhaa za ngono zinazodaiwa kuwa ni 'HALAL' limezinduliwa kwaajili ya waislamu nchini Uholanzi na baadhi ya mashehe wametoa ruhsa ya duka hilo la kwenye internet wakisema kuwa halivunji sheria za kiislamu.
Duka hilo linalodaiwa kuwa duka la kwanza duniani kwaajili ya waislamu wanaohitaji bidhaa za kuchombeza mapenzi yao lilizinduliwa wiki iliyopita.

Ndani ya siku nne za kuzinduliwa kwa mtandao wa tovuti hiyo kulikuwa na jumla ya cliks 70,000, alitamba mmiliki wa tovuti hiyo ya kwanza ya bidhaa za ngono kwaajili ya waislamu, Abdelaziz Aouragh.

Tovuti hiyo inayoitwa "El Asira" kwa maana ya jamii katika lugha ya kiarabu, ilizinduliwa kwa lengo la kuwauzia wanandoa wa kiislamu bidhaa za erotika.

Abdelaziz ambaye ni raia wa Uholanzi mwenye asili ya Moroko alisema kuwa alianzisha duka hilo la kwenye mtandao ili kuwaepusha waislamu kuingia kwenye tovuti zinazouza bidhaa hizo ambazo huweka picha na video za ngono ambazo ni haramu katika uislamu.

Ukurasa wa mbele wa El Asira hauna kitu chochote zaidi ya mstari unaotenganisha wanawake na wanaume, wanawake hutakiwa kuclick upande wao wa kushoto na wanaume huingia upande wa kulia.

Tovuti hiyo ina lugha tatu za kidachi, kiarabu na kiingereza na huuza zaidi mafuta kwaajili ya masaji, mafuta ya kupunguza ukinzani (lubricants) na dawa mbali mbali za malavi davi.

"Kila kinachopatikana humu ni Halal kinaruhusiwa katika uislamu' alisema Abdelaziz na kuongeza kuwa hakuna picha wala video za ngono kwenye tovuti yake.

Tovuti hiyo inaonyesha bidhaa zikiwa zimepigwa picha kwenye maboxi yake.

Abdelaziz alisema kuwa kabla ya kuanzisha duka hilo la kwenye mtandao alipata ushauri toka kwa mashehe mbalimbali na wanazuoni wa Uholanzi na Saudia ambao walimwambia kuwa hakuna sheria ya kiislamu anayoivunja.

"Ili mradi hauzi toys za ngono au vitu kama hivyo, hakuna tatizo lolote", alisema imamu wa Uholanzi, Abdul Jabbar.

"Mtume Muhammad (s.a.w) alitoa ushauri mbalimbali kuhusiana na masuala ya mapenzi kwenye ndoa, hivyo hakuna kitu cha kukionea aibu", aliongeza imamu huyo.

KIKWETE AZINDUA JENGO LA UPASUAJI WA MOYO



RAIS Jakaya Kikwete ameweka jiwe la msingi katika jengo la tiba la magonjwa ya upasuaji wa moyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
Pia jengo hilo ni kituo cha mafunzo ya atiba ya magonjwa hayo nchini.

Udhamini wa Ujenzi huo umetokana na ahadi ya Rais Hu Jintao wa China, aliyoahidi kuisaidia Tanzania alipokutana na Rais Kikwete mwaka 2006 kwenye mkutano wa China-Africa jiji Beijing.

Kikwete alisema nchi ilikuwa inahitaji kwa miaka mingi kujenga kituo hicho na uwezo wa kutibu na kufanya upasuaji wa moyo nchini na sasa imeshukuru Rais Jintao kwa kujenga kituo hiko na Tanzani itakuwa imejikomboa katika changamoto hiyo.

Alisema nchi ilikuwa inatumia gharama kubwa sana za matumizi kusafirisha wagonjwa kuwapeleka nje ya nchi kwa ajili ya upasuaji wa moyo.

Hivyo hatua hiyo ni chachu ya matumaini na inawapeleka wataalamu 26 kutoka nchini kwenda India kupata mafunzoya upasuaji, wakiwemo madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo wanne na madaktari wa moyo sita.

MWaka huu ilidaiwa kulikuwa na wagonjwa wapato 200 wa maradhi ya moyo na kati yao walioweza kubahatika kupelekwa nje ni 60 na wengine bado hawajapelekwa kutokana na gharama kuwa kubwa kuwatibu wagonjwa hao.

Hivyo kituo hicho kitaleta faraja ya nchi na Tanzania ditakuwea miongoni mwa nchi zitkazoweza kutibu magonjwa hayo.

VIDEO YA NYOTA WA MUZIKI MAREKANI AVUA NGUO HADHARANI



Erykah Badu katika video yake iliyosababisha mtafaruku
Mwanamuziki nyota wa Marekani, Erykah Badu ameingia kwenye mgogoro mkubwa baada ya kuvua zake zote na kubakia uchi katika sehemu ambayo rais wa Marekani, John F Kennedy aliuliwa kwa risasi.
Nyota wa muziki wa R&B, Erykah Badu ameingia kwenye mgogoro mkubwa baada ya kutengeneza video yake mpya ya muziki akivua nguo na kubakia uchi katika sehemu ambayo rais wa zamani wa Marekani, John F Kennedy alitunguliwa kwa risasi na kuuliwa.

Katika video yake hiyo mpya iliyochukuliwa mjini Dallas bila kibali wala ruhusa ya kujianika hadharani, Badu anaonekana akisaula nguo moja moja hadi kubakia mtupu wa mnyama na kisha kuigiza amepigwa risasi na kuanguka chini akijifanya amefariki.

Rais Kennedy alipigwa risasi na Lee Harvey mwaka 1963 wakati alipokuwa kwenye msafara wa magari ya rais pamoja na mkewe.

Badu ambaye alizaliwa Dallas mwaka 1971 ametoa albamu yake mpya inayoitwa "New Amerykah Part Two: Return of the Ankh".

Badu amesababisha mawazo tofauti toka kwa Wamarekani ambapo wengi wanasema kuwa ameidhalilisha sehemu ya kihistoria kwa kitendo chake hicho ambacho alikifanya mchana kweupe bila ya kujali kama kuna watoto au la.

Taarifa zinasema kuwa polisi huenda wakamkamata na kumtia mbaroni Badu kwa makosa ya kujianika hadharani.

Chini ni VIDEO ya Erykah Badu iliyozua kasheshe.


VIDEO – Nyota wa Marekani Avua Nguo Hadharani

MAITI ZA WATOTO ZATUPWA KWENYE MTO CHINA


Maiti za watoto zikiopolewa toka kwenye mto
Wafanyakazi wawili wa monchwari nchini China wanashikiliwa na polisi baada ya kuzitupa maiti 21 za watoto kwenye mto.
Wafanyakazi wawili wa ngazi za juu wa hospitali moja nchini China wamefukuzwa kazi huku wafanyakazi wawili wa monchwari wakiwa mbaroni baada ya maiti 21 za watoto kuopolewa toka kwenye mto.

Maiti za watoto wanane zilikuwa na alama za kuonyesha kuwa zilikuwa zimehifadhiwa kwenye hospitali ya chuo kikuu cha Jining Medical University katika mji wa Shandong, limeripoti shirika la habari la Xinhua.

Taarifa zinasema kuwa maiti za watoto hao zilikuwa ni za vichanga vilivyouliwa wakati wa utoaji mimba na watoto waliofariki kutokana na maradhi mbali mbali.

Taarifa za polisi zinasema kuwa wafanyakazi hao wa monchwari walilipwa na ndugu wa watoto waliofariki wazizike maiti za watoto hao lakini wao waliamua kuzitupa kwenye mto ulio mbali sana na hospitali hiyo.

Maiti za watoto zikiwa katika mifuko ya rambo ya njano ziliopolewa toka kwenye mto na kuzua hasira za wananchi walioshuhudia tukio hilo.

Angalia VIDEO ya tukio hilo chini.


VIDEO - Maiti za Watoto Zatupwa Kwenye Mto

Wednesday, March 31, 2010

TWO FOREIGN TOURISTS ROBBED AT GUN POINT IN ARUSHA NATIONAL PARK


Two foreign tourists have been robbed of various items worth several million dollars at gunpoint in Arusha National Park, raising serious doubts about the security situation in the game sanctuary.

In the rare episode, three heavily armed gangsters posing as game wardens reportedly ambushed the tourists in the park located nearly 35kms north-east of the northern safari capital of Arusha.

The thugs managed to put the tourists under siege and ransacked them before walking away with hard cash, tourist bags, digital cameras and other valuable items.

Arusha regional police commander Basilio Matei confirmed the incident.

“My men, in collaboration with Tanzania National Parks Authority game wardens, are currently working extra time hunting for the armed hooligans,” Matei said.

Jeremiah Maka, a professional tour guide with Big Expeditions who was escorting the tourists, said the incident took place at Ngurdoto crater within the national park late last week.

Maka named the victims as Christina Lazano from Spain and Paulina Elago from Namibia.

According to him, the two tourists were resolved to visit the nearest park in Arusha after taking time off from participating in an international conference.

“This is a strange incident to happen within the maximum security national park. It is unbelievable indeed, no one can buy the tale,” Maka explained.

For his part, Big Expeditions executive director Nicholaus Minja made a passionate call to the police and TANAPA to apprehend the culprits behind the shameful incident.

"The latest robbery incident will tarnish the good image of the country, but I hope the police, in collaboration with TANAPA, will do something about this,” Minja stressed.

SERIKALI YAMNG'ANG'ANIA LIYUMBA



UPANDE wa jamhuri katika kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 221 inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu, Amatus Liyumba umeiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imuone mshitakiwa ana kesi ya kujibu.

Ombi hilo liliwasilishwa mahakamani hapo jana saa tisa alasiri kwa njia ya maandishi yaliyochukua kurasa 29 na Mkuu wa Kitengo cha Sheria cha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Ben Lincoln na wakili wa serikali Prosper Mwangamila.

Kuwasilishwa kwa ombi hilo kulitokana na amri iliyotolewa Machi 15, mwaka huu, na kiongozi wa jopo la mahakimu wakazi wanaosikiliza kesi hiyo, Edson Mkasimongwa ambaye alizitaka pande zote kuwasilisha maombi kwa njia ya maandishi.

Kwa mujibu wa nakala ya ombi hilo ambalo gazeti hili lina nakala yake, upande wa jamhuri umedai kwa mujibu wa vielelezo 12 walivyotoa mahakamani na mashahidi wanane waliowaleta, wameweza kutoa ushahidi thabiti dhidi ya mshitakiwa ambao utaishawishi mahakama hiyo imuone ana kesi ya kujibu na kuongeza kuwa wanaiomba mahakama hiyo itupilie mbali ombi la utetezi lililotaka mahakama imuone mshitakiwa huyo hana kesi ya kujibu kwa sababu halina msingi.

Wakichambua shitaka la matumuzi mabaya ya ofisi ya umma kinyume na kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, jamhuri imejigamba kuwa imeweza kuthibitsha shitaka hilo kwa sababu mshitakiwa huyo ni kweli alikuwa mtumishi wa serikali toka mwaka 1971-2007 na kwamba alikuwa na cheo wakati wa mradi wa 10 Milambo Office Extention na alikuwa na jukumu la kuusimamia na kwamba kwa mujibu wa shahidi 1, 2, 3, 5, 6 na 8 waliithibitishia mahakama kuwa mradi huo ulikuwa ukiratibiwa na ofisi aliyokuwa akiongoza Liyumba ya Utumishi na Utawala.

Wakichambua shitaka la pili la kuisababishia serikali hasara, upande wa jamhuri umejigamba kuwa umeweza kuthibitisha shitaka hilo kwa madai kuwa hoja iliyodaiwa na upande wa utetezi kuwa haiwezekani kutambua hasara iliyopatikana bila ripoti ya mwisho ya mradi kukamilika si ya msingi kwani hata ikitolewa haiwezi kubadili makadirio ya gharama za mradi.

Kuhusu hoja ya upande wa utetezi iliyodai upande wa mashitaka umeshindwa kuthibisha kwamba mshitakiwa huyo alitenda makosa hayo akiwa na nia ovu, umedai kuwa katika kesi za jinai hoja hiyo haina msingi.

Machi 22 mwaka huu, mawakili wa utetezi Majura Magafu, Onesmo Kyauke, Hudson Ndusyepo na Jaji Mstaafu Hillary Mkate waliwasilisha hoja zao wakitaka mahakama hiyo imuachilie huru mshitakiwa huyo kwa sababu upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha kesi yao.

Kwa sababu tayari pande zote mbili katika kesi hiyo zimekwisha wasilisha hoja zao, kiongozi wa jopo la mahakimu wakazi, Mkasimongwa, Lameck Mlacha na Benedict Mwingwa, Aprili 9 mwaka huu, wanatarajiwa kutoa uamuzi wao kuhusiana na hoja hizo.

MAJAMBAZI 37 YAKAMATWA DAR



JESHI la polisi nchini lemefanikiwea kukamatwa majambazi 37 sugu katika operesheni inayoendelea nchi nzima.

Majambazi hayo yamekamatwa katika siku tofauti tofauti katika msako mkali wa jeshi hilo kuweasaka majambazi hayo yanayofanya uhalifu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleimani Kova amesema wamefanikiwa kuwakamata watu hao kwa mitego ambayo ilitegwa na jeshi hilo katika maeneo tofauti tofauti.

Amesema majambazi hayo kati yao 15 yalikamatwa yakiwa yamevaa mabaibui na madira ili kufanikisha uhalifu wao katika maeneo tofauti ya jiji.

Amesema pia waliweza kukamata bunduki aina ya SMG mopja, Short gun moja, bastola tatu pamoja na risasi kadha walizokutwa nazo wahalifu hao.

MAMA SALMA KIWEKE ANUSURIKA AJALI MBAYA




MKE wa Rais Mama Salma Kikwete anusurika kifo kwa ajali mbaya baada ya msafara wake kuingia doa kwa kuvamiwa na lori na kugonga magari matatu ya msafara huo.

Ajali hiyo ilitokea jana wilayani Rorya mkoani Mara wakati Mama Salma akiwa ziarani mkoani humo.

Kamdanda wea Polisi Tarime, Bw. Constantine Masawe alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na alisema lori hilo lilisimamishwa na askari wa barabarani lisimame ili kupisha msafara huo na kukaidi na kuingia barabarani na kusababisha ajali hiyo.

Amesema kuwa lori hilo liligonga magari matatu ya nyuma ya msafara huo na kusababisha ajali ambayo haikuwa ya lazima wka muda huo.

Amesema lori hilo lilikuwa linaokea nchini Kenya ambapo ilidaiwa pia lori hilo lilikuwa limebeba mali za magendo.

Hivyo imedaiwa dereva huyo ameshikiliwa na jeshi hilo ili kujibu tuhuma hizo.

Hata hivyo hakuna aliyeweza kupoteza masiha kaika ajali hiyo.

Monday, March 29, 2010

WORK FOR WATER IN PORTLAND OREGON WITH ERICK MWARABU


THE AMBASSADOR TO THE US HON.OMBENI SEFUE





Walk for Water-Down town Portland, was an event to drawing attention to the plight of millions of people whose access to safe drinking water is severely limited, Walk for Water raised funds to benefit Water For All, a non-profit organization dedicated to bringing clean water to families in sub-Saharan Africa. Walker registration fees, combined with local sponsor donations, went toward the goal of raising funds needed to build a series of water pumps in Tanzania. Ambassador Ombeni Sefue was the Key-note Speaker.
Eric Cliff Mwarabu
(Project Management/Marketing)
PORTLAND ROASTING.
503-236-7378 Main
800-949-3898 Free
503-841-3176 Mobile
503-231-2901 Fax

DINNER BANQUE IN LAS VEGAS


THE HONOR OF YOUR PRESENCE IS REQUESTED AT A DINNER BANQUET
WHICH WILL BE HELD ON SATURDAY 05.29TH.2010 AT 3525 E FLAMINGO RD LAS VEGAS NV 80121
R.S.VP NO LATER THAN MAY 8TH BY TELEPHONE OR EMAIL.
JACQUELINE KADIRI AT 707-290-4301 OR tonopa32@hotmail.com or
DOMICIAN MBEIKYA @ 707-290-2407 OR domcdavidy@yahoo.com
REGISTRATION WILL BEGIN AT 4:30PM AND DINNER WILL BE SERVED AT 5:30
REGISTRATION FEES OS $25 PER HEAD AND GROUP RATES FOR HOTELS ARE AVAILABLE .

MTOTO MWENYE VIDOLE 31 TOKA CHINA



Mtoto huyu wa nchini hana idadi ya vidole vya miguu na mikono kama watu wengine, amechukua rekodi ya dunia kwa kuwa na jumla ya vidole 31.
Mtoto mwenye umri wa miaka sita wa nchini China analazimika kufanyiwa operesheni ili kupunguza idadi ya vidole vyake vya mikono na miguu.

Mtoto huyo wa mji wa Shenyang katika jimbo la Liaoning kaskazini mwa China ana jumla ya vidole 16 vya miguu na vidole 15 vya mikono.

Vidole vyake vitatu katika kila mkono wake vimeungana pamoja.

Idadi ya vidole vyake inavunja rekodi ya dunia ya vidole 25 iliyokuwa ikishikiliwa na watoto wawili wa India Pranamya Menaria na Devendra Harne, ambao kila mmoja wao ana vidole 12 vya mikono na vidole 13 vya miguu.

Hata hivyo mtoto huyo wa nchini China atafanyiwa operesheni ya kupunguza idadi ya vidole vyake wiki hii.

MWANAME MWENYE MATITI MAKUBWA DUNIANI TOKA CHINA



Guo Feng mwanaume mwenye matiti makubwa Monday, March 29, 2010 4:58 AM
Madaktari nchini China wanadai kumgundua mwanaume mwenye matiti makubwa kuliko wote duniani.
Madaktari nchini China wanadai kumgundua mwanaume mwenye matiti makubwa kuliko wote duniani baada ya mwanaume huyo kujitokeza kwenye kliniki moja mjini Beijing.

Daktari wa hospitali ya Jinan Chest Hospital, Dokta Zhang Lilan alisema "Huyu ni mwanaume kamili isipokuwa ana matiti kama mwanamke".

"Yeye ni mkulima na anasema kuwa anasumbuliwa na ukubwa wa matiti yake wakati anapofanya kazi zake za kilimo".

"Anasema pia matiti yake yamekuwa gumzo kijijini kwake ambapo watu wengi wamekuwa wakimtafuta ili kumuona na imekuwa kero kubwa sana kwake kiasi cha kumfanya awe anavaa makoti makubwa hata wakati wa joto kali ili kuyaficha matiti yake", alisema dokta Lilan.

Mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la Guo Feng mwenye umri wa miaka 53, alisema "Miaka 10 iliyopita matiti yangu yalianza kuwa makubwa lakini nilikuwa nikifikiria unene wangu ndio sababu .. lakini miaka michache iliyopita nimekuwa nikizunguka hospitali moja baada ya nyingine kutafuta tiba lakini hakuna mtu anayetaka kunisaidia".

"Nimetumia pesa nyingi sana kwenye vipimo hospitalini lakini hakuna jibu lolote la maana huku matiti yangu yakiendelea kuwa makubwa", alisema Guo Feng.

"Wakati mwingine huwa nafikiria madaktari hawataki kunisaidia", alilamika Guo Feng.

Dokta Lilan alisema kuwa Guo Feng ametishia kuyakata matiti yake yeye mwenyewe iwapo hakuna daktari atakayejitokeza kumpatia tiba.

Hata hivyo madaktari wamekataa kuchukua hatua yoyote mpaka watakapogundua sababu ya matiti yake kuwa na ukubwa huo usio wa kawaida.

"Katika miaka yangu 30 ya kufanya kazi ya udaktari sijawahi kukumbana na kitu kama hichi", alisema Dokta Lilan.

"Awali tulidhania amekula kitu chenye sumu lakini vipimo vya damu yake havijaonyesha kitu chochote. Tumemfanyia X-ray hana dalili ya kansa", aliongeza mmiliki wa hospitali hiyo.

DARAU ZA RAISI WA ZAMAMNI WA MAREKANI GEORGE BUSH




Bush akiufuta mkono wake kwa kutumia shati la Bush Monday, March 29, 2010 5:45 AM
Rais wa zamani wa Marekani, George Bush ameingia katika zengwe kubwa sana baada ya kudaiwa kuonyesha dharau kwa kuufuta mkono wake kwa kutumia shati la rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton baada ya kupeana mkono na mhanga wa tetemeko la Haiti.
George W Bush ameingia kwenye zengwe kubwa sana baada ya kudaiwa kuufuta mkono wake baada ya kupeana mkono na raia wa Haiti aliyenusurika kwenye tetemeko kubwa la ardhi lililoikumba nchi hiyo na kuua maelfu ya watu.

Rais huyo wa zamani wa Marekani alinaswa live katika video akisalimiana kwa kupeana mkono na mkimbizi wa Haiti halafu alifuta mkono wake kwa kutumia shati la rais mwenzake mstaafu, Bill Clinton.

Tukio hilo limetokea wiki iliyopita wakati Bush na Clinton walipotembelea kambi ya wahanga wa tetemeko la ardhi mjini Port-au-Prince baada ya kuombwa na rais Barack Obama wafanye hivyo ili kutunisha mfuko wa kusaidia wahanga wa Haiti.

Bush anaonekana wazi akipeana mkono na mwanaume raia wa Haiti na kisha kuuzungusha mkono wake hewani akiangalia wapi ausafishe mkono wake kabla ya kuamua kutumia shati jeupe la Bill Clinton aliyekuwa amesimama pembeni yake kujifutia katika staili ambayo hata Clinton mwenyewe hakushtukia.

Video ya tukio hilo imewekwa kwenye YouTube na kuzua maoni mbali mbali mengi yao yakipigia kelele kitendo hicho.

Angalia VIDEO ya tukio hilo chini.

MADEREVA WA DALADALA DAR WATANGAZA MGOMO


MADEREVA na makondakta wa daladala wa jijini Dar es Salaam wametangaza mgomo wa kuacha huduma hiyo ambayo walidai utaanza leo.
Mgomo huo tarajio ulisambazwa kwa njia ya vipeperushi na baadhi ya madereva wa jijini humo na mgomo huo utahusisha njia zote za mkoa wa Dar es Salaam.

Sababu ya kuanzisha mgomo huo ulidaiwa na maderava hao kuwa ni maslahi duni kwa siku, na kubwa ni kero za barabarani zinazosababishwa na Kampuni ya Majembe na askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani (Trafiki) ambao wamekuwa wakiwasumbua kila siku kwa sababu ambazo hazina msingi.

Madai mengine ni kutaka kuwekewa mazingira bora ya kazi ikiwemo mishahara, na makato ya mishahara hiyo ipelekwe Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa lengo ya kuboresha kazi hiyo kama wafanyakazi wengine nchini.

ACTIVE FINANCE AND ACTIVE TOURS






Kevin William Mbogo
Chief Executive Officer
...............................
ACTIVE FINANCE AND ACTIVE TOURS
P.O.BOX 3176
Dar es salaam
Tanzania
Tel: +255 22 2134700
Fax:+255 22 2134700
Hotline: +255 787 888 884
+255 777 028 570
Email:info@activetz.com
Web:www.activetz.com

Sunday, March 28, 2010

INDIGENATION


FROM ARUSHA TO WASHINGTON DC
For all of you who resides in DC Metro Area, come join your country men in a Roots Reggae Jam Session and a debut show for Indigenation, a new Reggae Group lead by GMtui.

Thursday April 8th @ 9:30pm
Cover: Free
Location: O'Shaughnessy's Pub. 1324 King Street. Alexandria, VA 22314.

See Ad on Facebook (Indigenation Roots Reggae), CityPaper, www.tanzamerica.blogspot.com and more

Come one, Come all, Support the local.

iNdiGeNation
From Arusha to DC as it was from Hebron To Babylon.

SIMBA KUVUNJA REKODI YA MWAKA 1993



Wachezaji wa Simba wakishangilia ushindi katika mojawapo ya mechi za ligi kuu ya Bara Saturday, March 27, 2010 3:51 AM
MABINGWA wa Bara, timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam wamepania kuvunja rekodi yao ya mwaka 1993 ya kufika fainali ya Kombe la CAF, ambapo sasa wanataka kutwaa taji la Shirikisho hilo la Afrika. Simba mwaka 1993 ilitolewa katika fainali za CAF baada ya kufungwa 2-1 na timu ya Stella Abdjan katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa (sasa Uhuru).

Katika mchezo wao wa kwanza, timu hizo zilitoka suluhu na hivyo Simba ilihitaji ushindi wa angalau bao 1-0 ili kutwaa taji hilo.

Meneja wa timu hiyo, Innocent Njovu alisema jijini kuwa wana uhakika wa kutwaa taji hilo kutokana na kuwa na kikosi bora kama cha mwaka 1993.

Njovu alisema mbali na kikosi hicho kuwa bora pia wachezaji wao wamekuwa na ari ya ushindi baada ya kutwaa ubingwa wa bara mapema kabla ya ligi kumalizika, wakiwa wamesaliwa na mechi mbili kibindoni.

"Sisi tuna uhakika wa kufika kwenye fainali kwani kwa sasa kikosi ni bora, na wana ari ya kushinda katika kila mechi wanayocheza, hivyo kutokana na dhamira hiyo tuna uhakika wa kufikia hatua ya juu zaidi yaani ya fainali," alisema Njovu.

Alisema baada ya kuwapa mapumziko mafupi wachezaji wao, watapiga kambi huko Zanzibar kujiandaa na mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Lenghten ya Zimbabwe.

Katika mchezo wa awali uliofanyika Zimbabwe Ijumaa iliyopita, ambao Simba iliyofuzu hatua ya pili moja kwa moja, waliwashinda wapinzani wao kwao kwa magoli 3-0, ushindi ambao ni mnono kwa klabu hiyo.

Hata hivyo, Njovu alisema wapinzani wao sio wa kubeza kutokana na kandanda safi waliyoionyesha na wanaamini mchezo wa marudiano utakaofanyika Jumapili ijayo jijini Dar es Salaam, utakuwa wa ushindani mkubwa.

KAPUYA AWEKA UWAZIRI PEMBENI NA KUANZA KUPEKECHA



Katika hali isiyo ya kawaida kwa viongozi wa juu nchini kuonekana katika kumbi za starehe tena katika sare sambamba na waimbaji wa bendi, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya aliingia ukumbini na kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya wana wa Akudo. Huku akiwa amevalia sare sawa na waimbaji wa bendi ya Akudo, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya alijitosa ukumbini na kuanza kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya bendi ya Akudo Impact iliyokuwa ikitoa burudani kwenye ukumbi wa Msasani Beach.

Kapuya ambaye ndiye mmliki wa bendi hiyo alijimwaga stejini na kusakata muziki kwa nguvu zote huku jasho likimtoka akiwa pamoja na mpambe wake ambaye jina lake halikufahamika.

Kapuya anakuwa kiongozi wa pili wa juu serikalini kumiliki bendi wa kwanza alikuwa Waziri Mdhihiri Mdhihiri ambaye aliwahi kumiliki bendi ya Mchinga Sound ambayo baadaye ilivunjika.

Kutokana na jinsi anavyoithamini bendi yake, waziri Kapuya amefanikiwa kuifanya bendi ya Akudo iwe miongoni mwa bendi zinazopendwa sana nchini kiasi cha kuleta ushindani mkubwa katika medani ya muziki wa dansi hapa nchini.

BABU WA MIAKA 96 AMUOA MWANAMKE WA MIAKA 30



Babu mwenye umri wa miaka 96 wa nchini Taiwan amekuwa gumzo nchini humo baada ya kufunga ndoa na mwanamke aliyemzidi miaka 66. Babu Lin Chung ameweka rekodi ya kuwa bwana harusi mwenye umri mkubwa kuliko wote nchini Taiwan baada ya kufunga ndoa na mwanamke mwenye umri wa miaka 30.

Chung amekuwa gumzo kwenye kitongoji cha Tainan baada ya kumuoa mwanamke huyo anayetoka maeneo ya ukanda wa kati nchini China katika jimbo la Hunan.

Chung ambaye hakuwahi kuoa katika ujana wake, ana watoto wawili aliojitolea kuwalea tangia walipokuwa wadogo ambao hivi sasa mmoja kati ya watoto hao ana umri wa miaka 68.

Chung anadai kwamba miaka mitatu iliyopita, alipewa maelezo na Mungu aende kwenye jimbo la Hunan nchini China ili kumtafuta mwanamke anayekuja kuwa mke wake.

Chung alifunga ndoa na mwanamke huyo hivi karibuni pamoja na upinzani mkali toka kwa mwanae huyo wa kujitolea ambaye alikuwa akimuona babu huyo kama amelaghaiwa.

"Inanibidi niwe na mwenza katika uzee wangu... sikuwahi kuwa na mke, kwanini hivi sasa hataki mimi nioe", alisema Mzee Chung.

Chung hivi sasa anashughulikia taratibu za kisheria kumwezesha mkewe ahamie Taiwan toka China ili waishi pamoja.

Saturday, March 27, 2010

"FROM ARUSHA TO DC AS ITS WAS FROM HEBRON TO BABILON



CAME ON PEOPLE LETS SHOW SOME LOVE TO OUR FOX FROM HOME.
DC ARE YOU READY???????????????????
ITS GOING DOWN FOX!!!!!!!!!!ITS REALLY GOING DOWN .LETS GIVE IT UP FOR OUR BROTHERS.
DON'T MISS IT DC ITS GOING DOWN.

MAYALA WEBTECH SOLUTIONS




Hallow fellow Tanzanians; this is Isack Mayala presenting MAYALA WEBTECH SOLUTIONS (M.W.S). This is a global full service firm that offers web designing from scratch, re-designing old websites, logo designing, flash designing, business card design, online website solution e.g. e-commerce and database management.

Our product/service is purchased by corporations, universities, and organizations around the world. Below is a list of just a few of our clients that we have provided our services for over the years.

http://www.angellalubala.com

http://www.holifrench.org

http://www.themissionband.org

http://www.christianmissionschurch.org

We are here to create, implement and provide the most needed web services and educate consumers to use those products as an integrated part of their business. We are currently based in United States of America; soon we will be opening our offices in Dar Es Salaam, Tanzania. Please visit our website http://www.mayalawebtech.com for more information. Send us an email at info@mayalawebtech.com if you have any question.

Thanks in advance for your business

Friday, March 26, 2010

APOTEZA MAISHA KWA MOTO KISA KUKATALIWA


Mwanaume mmoja wa nchini Uingereza ambaye alitoswa na mkewe wa ndoa ya miaka 14 ambaye alipata mwanaume mwingine nje, amefariki dunia kutokana na moto aliouanzisha ili kuichoma moto nyumba yake ili mkewe asiambulie kitu watakapoachana. Wakati Timothy Flood alipoimiminia petroli nyumba yake ili ndoa yake na mkewe itakapovunjika, mkewe asiambulie kitu, hakungundua kuwa kuna kiasi kidogo cha petroli kilimwagikia kwenye nguo zake.

Na wakati alipoipiga kiberiti nyumba yake alishangaa kujikuta na yeye mwenyewe akiwaka moto.

Timothy ambaye ni baba wa watoto watatu alijaribu kuuzima moto uliokuwa ukimteketeza kwa kutumia maji ya mvua lakini hadi wakati anaokolewa alikuwa ameishangua asilimia 90 ya mwili wake na alifariki dunia siku mbili baadae hospitalini.

Timothy mwenye umri wa miaka 42, aliamua kuichoma moto nyumba yake baada ya mkewe kuamua kuivunja ndoa yao alipoanza uhusiano na mwanaume aliyesoma naye shule.

Ingawa Timothy na mkewe, Catherine, 39, walikuwa wakiendelea kuishi kwenye nyumba moja walikuwa hawazungumzi wala kujuliana hali.

Mgogoro mkubwa ulikuwa kwenye nyumba yao ambapo Catherine alimtaka Timothy aondoke amuachie yeye nyumba hiyo.

Timothy kwa kuhofia kuwa watakapoachana rasmi kisheria kutokana na sheria mkewe anaweza akapewa nyumba kwa sababu ya watoto wao,
aliamua kuichoma moto ili wakose wote.

Mahakama katika mji wa Newport, kusini mwa Wales iliambiwa kuwa Timothy ili kuichoma moto nyumba hiyo alinunua lita 51 za petroli na viberiti kadhaa ili kuhakikisha kuwa hakitoki kitu.

Siku ya tukio, alimpeleka mkewe kwa wazazi wake na ndipo aliporudi na kuipiga moto nyumba hiyo baada ya kumtumia meseji mkewe akimwambia "Nimeishapata suluhisho la kuishi bila wewe".

Moto mkubwa ulizuka ambao uliiteketeza sehemu kubwa ya nyumba hiyo.

Majirani wanasema kuwa Timothy alisikika akipiga kelele za kuomba msaada wakati moto aliouanzisha akitegemea kuiteketeza nyumba yake ulipokuwa ukimchoma yeye mwenyewe.

Timothy alifariki siku mbili baadae hospitalini baada ya ndugu zake kukubali kuzizima mashine zilizokuwa zikimsaidia aendelee kuishi.

DR,SLAA AMFURISHA KIKWETE

BAADA ya Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa kuibana serikali kuhusu vipengele vilivyoongezwa kinyemela katika muswada uliosaniwa na Rais Jakaya Kikwete kwa mbwembwe wiki iliyopita, taarifa mpya zinasema Rais amefura, akitaka maelezo ya kina ya walioingiza vipengele hivyo.

Tanzania Daima lilipozungumza na mmoja wa wasaidizi wa Rais Kikwete kuhusu sakata hilo jana, alidokeza kwa maneno machache, na kwa msisitizo, akisema: “Rais amefura.”

Msaidizi huyo wa rais alisema kutokana na kasoro hiyo ya kwanza ya aina yake kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii, Rais Kikwete ametaka maelezo ya kina ili kubaini waliohusika kuchomeka vipengele hivyo.

Naye Dk Slaa, ambeye ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amezidi kuibana serikali akiitaka irejeshe bungeni Muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi ili kifungu kilichochomekwa kinyemela kiondolewe.

Alisema hilo ni hitaji la lazima la kisheria; na kwamba serikali isipofanya hivyo katika mkutano ujao wa 19 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, itachukuliwa hatua za kisheria. Alitaka waliohusika wawajibishwe.

Dk. Slaa, mmoja wa wabunge wanaosoma sana na wenye upeo mkubwa bungeni, ndiye aliyeibua sakata la kasoro hiyo wiki hii.

Jana alisema: “Naomba serikali ichukue hatua kuwasilisha Miscellaneous Amendment katika mkutano wa 19, yaani Bunge la Aprili, ili kifungu hiki ambacho ni kinyume na demokrasia kiondolewe kwenye Sheria ambayo rais ameisaini, vinginevyo tutachukua hatua za kisheria.

“Kama ilivyoripotiwa na gazeti la Tanzania Daima, Mhe. Spika jana wakati anajibu kwenye taarifa ya saa mbili usiku ya TBC1 ni dhahiri alionyesha kuwa hajasoma na hakuwa ameelewa vizuri kinacholalamikiwa.

“(Kama) Angekuwa amesoma, Spika angekuwa mwangalifu kutamka aliyoyatamka. Mheshimiwa Spika anakiri kulikuwa na mjadala, lakini hakutamka mjadala ulihusu nini na wala hakumnukuu Mwenyekiti wa siku hiyo ambayo alikuwa Mhe. Naibu Spika alitoa maagizo gani.

“Ni hatari kwa viongozi wetu kutoa matamko kwa mambo mazito bila kufanya utafiti angalau mdogo. Mhe. Spika atakubali kuwa kwenye Hansard, hakuna popote ambapo imejadiliwa achilia mbali kukubaliwa kuwa ‘Timu ya Kampeni itathibitishwa na Msajili (kwa
mgombea urais) au Katibu Tawala (kwa mgombea ubunge) au na Mtendaji wa Kata kwa (mgombea udiwani).’ Hii ni dhana mpya kabisa, siyo tu haijajadiliwa wala haikufikiriwa kama Hansard inavyoonyesha.”

Dk. Slaa alitoa kauli hii ya jana wakati akijibu kauli ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye juzi alizungumza kupitia kituo cha Televisheni cha TBCI, akitetea udhaifu huo wa kuchomeka kipengele hicho kiholela.

Dk. Slaa alifafanua kuwa kilichojadiliwa ambacho yeye alishiriki ni hoja aliyoleta Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge kutaka kufanyia mabadiliko pendekezo la serikali kwa kifungu cha 7(2).

Alisema katika kifungu hicho, Chenge alitaka makundi ya sanaa yaingizwe baada ya neno voters.

“Hivyo ni vyema naye Spika akiri tu kuwa utaratibu wa kutunga sheria umekiukwa. Haifai kubishana kwa sababu ya kubishana wakati Hansard ndiyo ushahidi wa wazi wa jambo hilo.

“Mimi ndiye namwomba Mwanasheria Mkuu, rafiki na ndugu yangu, aisome vizuri kwa kuwa yeye ndiye hajasoma. Amesema vizuri kututaja ambao tulikuwa na mjadala ukumbini, sasa anionyeshe mahali popote katika mjadala huo ni wapi approving authority ilijadiliwa, na kuwa hiyo approving authority iwe Msajili, DAS na WEO.

“Hivyo, ni ustaarabu tu kukiri kuwa kifungu hiki kimechomekwa na kuwa akubali,” alisema Dk. Slaa.

Hata hivyo, tayari Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema juzi aliliambia gazeti hili kwamba iwapo itabainika kuwa kauli ya Dk. Slaa ni ya kweli, serikali itaomba radhi na kupeleka muswada bungeni kwa ajili ya masahihisho hayo.

Dk. Slaa alidai Rais Kikwete amepotoshwa katika baadhi ya vipengele, kikiwamo kipengele kinachohusu uthitibishwaji wa wajumbe wanaounda timu za kampeni kwa ajili ya wagombea urais, wabunge na udiwani.

Alisema Bunge halikukubaliana kuhusu kipengele hicho, wala hakimo katika kumbukumbu za Bunge; na kwamba kiliongezwa baadaye, kabla ya Rais Kikwete kusaini muswada huo kuwa sheria.

Kifungu kinachodaiwa kuchomekwa ni cha 7 (3), ambacho hakikuwepo kabisa kwenye muswada uliojadiliwa na kupitishwa bungeni.

Kwa mujibu wa sheria hiyo, kifungu kidogo cha pili, kinaeleza maana ya timu ya kampeni kuwa ni kundi la watu lililoundwa na mgombea wakati wa zoezi la uteuzi lenye madhumuni ya kumwakilisha au kumsaidia mgombea kwenye kampeni za uchaguzi ambaye amepitishwa kuwania.

“(a) Kwa kesi ya urais watathibitishwa na Msajili, (b) Kwa kesi ya Mbunge watathibishwa na Katibu Tawala wa Wilaya na (c) Kwa kesi ya Diwani watathibitishwa na Katibu Tarafa...,” ilieleza sehemu ya sheria hiyo iliyosainiwa na Rais Kikwete ambayo nakala yake tunayo.

Muswada huo wa sheria ulioasisiwa na Rais Kikwete mwenyewe, ulipitishwa kwa mbinde Februari 12 mjini Dodoma huku ukiibua malumbano makubwa baina ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Werema, na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, pamoja na wabunge wengine kuhusu vipengele mbalimbali vya muswada huo.

MREMA AFUNGUA KESI MAHAKAMANI,ADAI BIL 1/-

HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema amefungua kesi ya madai ya sh bilioni moja dhidi ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Kesi hiyo ya madai namba 32/10 imefunguliwa na mwenyekiti huyo anayeongoza chama chenye wafuasi wasiozidi 500,000 nchini kote kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya chama hicho Magomeni, Dar es Salaam jana, Mrema alieleza dhamira yake ni kutaka kupata uthibitisho kutoka kwa spika huyo wa Bunge kama amefilisika na kwa sasa anahongwa na makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kadhalika, Mrema anadai kwamba kitendo cha Sitta kuieleza jamii kupitia gazeti kwamba amechanganyikiwa na amepewa fedha kwa ajili ya kuipigia debe CCM kina lengo la kumdhoofisha katika kampeni zake za kuwania ubunge wa Vunjo kwa tiketi ya TLP.

“Katika barua niliyopeleka kwa Spika nilitaka aniombe radhi kwa uzito ule ule katika kipindi cha siku saba na kunilipa fidia, lakini akawa kimya kwa muda wote huo,” alisema Mrema na kuongeza kwamba washitakiwa wengine katika kesi hiyo ambayo haijapangiwa jaji ni gazeti lililochapisha habari hiyo na mhariri wake akiamini kuwa ndiyo chombo kilichotumika kumchafua na kumpotezea hadhi aliyojijengea.

“Hivi kweli mimi nimechanganyikiwa? Kwanini anivunjie hadhi yangu?… Nimekuwa Naibu Waziri Mkuu wa nchi hii, nimefanya mengi sana nilipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, kwa miaka 30 nimeitumikia Tanzania,” alisema Mrema.

NYUKI WENYE HASIRA WAUA MIFUGO NA KUJERUHI WATU 40


Nyuki wenye hasira walikitesa kijiji kizima nchini Niger kwa masaa kadhaa na kuua mifugo kadhaa pamoja na kuwafanya watu zaidi ya 40 wakimbizwe hospitali wakiwa majeruhi. Kundi la nyuki waliokuwa na hasira baada ya mzinga wao kwenye mti kung'olewa, walikitesa kijiji kimoja kusini mwa nchi ya Niger kwa kuwashambulia watu na mifugo kwa masaa kadhaa.

Watu zaidi ya 40 wakiwemo watoto 14 waliwahishwa hospitali baada ya kushambuliwa na nyuki wakati mzinga wa nyuki uliokuwa kwenye mti mkubwa kwa zaidi ya miaka 50 ulipodondoshwa chini kutokana na upepo mkali.

Punda mmoja na farasi mmoja walifariki dunia huku ng'ombe na mbuzi 95 wakiachwa wakiwa wamepooza miili yao baada ya kudungwa sindano za nyuki hao wenye hasira.

Kwa mujibu wa radio Anfani ya nchini Niger, nyuki walikivamia kijiji cha Dake-Garka katika mji wa Birni-N'Konni baada ya tawi la mti lililokuwa na mzinga wao, lilipoangushwa chini na upepo mkali.

Iliripotiwa kuwa masaa kadhaa baada ya uvamizi wa nyuki hao, wanakijiji walikuwa bado wanahofia kurudi kwenye majumba yao kwa kuhofia mashambulizi ya nyuki.

CALIFORNIA NEW LAW WONT HURT ECONOMY

SAN FRANCISCO

California's economy will not be damaged by the state's 2006 climate change law, a state agency said in a report yesterday that counters the business community's arguments that the economically troubled state will lose more jobs and businesses.

The analysis by the state Air Resources Board, the chief regulator of the law, forecast higher energy prices from new regulations and a cap-and-trade system for greenhouse gases, but said greater energy efficiency would keep costs manageable in the trend-setting environmental state.

It concluded that the measure will yield modest job gains statewide, will have a negligible effect on the state's overall economy -- the eighth largest in the world -- and could benefit some sectors like alternative energy businesses.

In sharp contrast to a 2008 report that was panned as shallow and full of faulty assumptions, the Wednesday analysis was received with cautious approval from academics at Stanford and other universities who consulted on the process.

Business groups however said the state was still making rosy assumptions.

In 2006, California's Legislature passed and Republican Governor Arnold Schwarzenegger signed a law committing the state to developing regulations to reduce greenhouse gas emissions -- blamed for global climate change -- to 1990 levels by 2020.

"These policies can shift the driver of economic growth from polluting energy sources to clean energy and efficient technologies, with little or no economic penalty," the report said.

Thousands of manufacturing, mining and utilities industry jobs will be lost, but service, finance, and other sectors will gain similar numbers, leaving the most populous US state about the same in terms of total jobs, income and growth, the report said. Five scenarios found a maximum effect of tens of billions of dollars on state output of $2.5 trillion in 2020.

Much will depend on what happens outside California, including whether California is at the leading edge of a move away from fossil fuels.

"It might hasten the arrival of regional, national or other international policies, and I think that is what California is betting on," said Stanford economist Larry Goulder, one of the academics on the panel advising state researchers.

California aims to reduce greenhouse gas emissions through a variety of steps such as tighter standards on car fuel efficiency, standards on energy efficiency in buildings, and a "cap and trade" market for pollution credits.

Under cap-and-trade, carbon dioxide and other greenhouse gas emissions would be capped. Companies would need permits for the pollution they send into the atmosphere and those permits could be traded on a regulated market.

Three US senators -- Democrat John Kerry, Republican Senator Lindsey Graham and independent Senator Joseph Lieberman -- are working to resuscitate climate change legislation in the US Senate after the House of Representatives passed its version of the measure last year.

A parallel study by consultancy Charles River Associates, which worked at the request of the Air Resources Board, put the cost of the climate law at a few hundred dollars per person in 2020 and said success would depend on the state giving itself room to respond to issues, such as high gasoline prices.

"It is clear that flexibility matters," said Charles River consultant Paul Bernstein.

Many businesses still fear tens or hundreds of thousands of jobs could be lost, spurred by higher energy prices from the law, known locally as AB32.

"Their conclusion is that AB32, the most far-reaching regulation in history, won't impact jobs in California," Shelly Sullivan, spokeswoman for the AB 32 Implementation Group, which includes several chambers of commerce, said skeptically.

Goulder and the other economists called the new report "valuable information" and said it addressed key concerns by creating a better scenario if the law did not take effect and scenarios if parts of the law did not work as planned.

Mary Nichols, chair of the Air Resources Board, told reporters that the new analysis was better than 2008.

"We made all the changes and found that the results were pretty much the same as they had been the first time around, which is very modest, almost undetectable overall effect on gross state product by 2020 but some modest improvement in areas of job growth and personal income," she said.

AJALI MBAYA DAR, HIACE YAKANDAMIZWA NA LORI




ZAIDI ya watu nane wamepoteza maisha papohapo kwa ajali mbaya iliyotokea huko maeneo ya Kibamba Darajani nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Ajali hiyo ilitokea jana, majira ya saa 11 alfajiri ambapo ilihusisha gari aina ya lori lililokuwa na namba za usajili T 189 na basi dogo la abiria aina Toyota Hiace lililokuwa na namba za usajili T 616 AJW.


Ajali hiyo imetokea baada ya lori hilo lililokuwa likitoka Dar es Salaam kuelekea Pwani kupoteza mwelekeo na kuingia kulia zaidi na kuivaa basi hilo uso kwa uso lililokuwa na abiria na kulilalia na kupoteza maisha ya watu hao.

Hiace hiyo ilikuwa inatoka Lugoba mkoani Pwani ilikuwa inaelekea Dar es Salaam na ndipo ilipovamiwa na lori hilo na abiria wote waliokuwemo humo kufariki dunia papohapo na kati yao kulikuwa na mamda mjamzito.


Hata hivyo ilidaiwa kuwa lori hilo lilikuwa imeshindwa kuhimili breki na kudaiwa halikuwa na breki na ndicho chanzo kikuu cha ajali hiyo mbaya.

Hata hivyo mara baada ya kutokea kwa ajali hiyo dereva wa lori na utingo wake wlikimbia na kuacha lori hilo papohapo na hawakujulikana mara moja walikimbilia wapi kwa muda huo.

Katika hali ya kushangaza wananchi bado hawajifunzi na baadhi ya maelfu waliokimbilia katika ajali hiyo kuonekana kuzoa mafuta ya taa yaliyomwagika barabarani na kusahau kuwa siku za karibuni watu walipoteza maisha kutokana na matukio kama hayo walikuw wnazoa mafuta na ghafla lori kulipuka na kupoteza maisha na wengine walipata vilema vya maisha kutokana na

MAHABUSU WAJIPAKA KINYESI MAHAKAMANI DAR.

MAHABUSU watano jana walitoa kioja cha mwaka katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni walijipaka kinyesi kwa kugoma kurudi mahabusu. Washitakiwa hao wanaokabiliwa na kesi ya wizi wa kutumia silaha wote kwa pamoja walichukua uamuzi huo baada ya kugoma kurudi mahabusu kwa kutaka wafutiwe mashitaka yao ambayo yamedumu wka muda mrefu.


Hivyo washitakiwa hao walipotakiwa na askari magereza kutoka mahabusu na kuelekea mahakamani walichukua vinyesi na kujipaka mwilini.


Hali ilikuwa tata walipofika mahakamani hapo hali iliyoradhimu hakimu kushindwa kuendelea kusikiliza shauri hilo kwa siku hiyo.


Mahabusu hao walionekana kugoma kupanda basi maalum linalowarudisha rumande kwa madai ya kutaka kufutiwa shauri hilo hali iliyofanya wapakiwe kwenye gari dogo na kupelekwa kituo cha polisi Magomeni.

EASTER SPECIAL AT MENAI BAY BEACH BUNGALOWS!!!


SUNSET VIEW AT MENAI BAY BEACH BUNGALOWS!!! IT'S LOVELY

YOU WILL GET A CHANCE TO RELAX AND ENJOY ON THE LOCALLY BEDS.

SINGLE ROOM AT MENAI FRESH WEATHER AND CLEAN!!!



DOUBLE ROOM

MENAI BUNGALOWS FROM OUTSIDE
NAI BAY BEACH BUNGALOWS

Menai Bay Beach Bungalows (Unguja Ukuu) Consisting of five beach bungalows set in a shady palm grove direct on the beach.

THE BEACH BUNGALOWS.
The hotel Menai consists of ten rooms in bungalows, built of local materials. The rooms are equipped with double or king size beds, mosquito nets, 4 rooms with fans & 6rooms with fan and Air Conditions.
The private verandah overlooks the lush tropical gardens and the Indian Ocean beyond. All rooms have their own bathroom with toilet, washing basin, shower and hair dryers.

THE BEACH RESTAURANT (NEW MASAI RESTAURANT)
Is situated direct on the beach under a huge baobab tree. Our specialty is all kind of fresh caught seafood, prepared in international or traditional local style.
Enjoy romantic sunsets over the bay while sipping a glass of wine.

We are proud of our lush tropical garden.
1000 years old Baobab trees, Mango and Almond trees, Bougainvilleas and Barbados Pride illuminate the hotel ground.

EASTER SPECIAL OFFER FOR TANZANIAN AND EST AFRICANS.
ROOMS WITH FANS
SINGLE ROOM ON BB Tshs. 25,000 per night
DOUBLE ROOM ON BB Tshs. 30,000 per night
TRIPLE ROOM ON BB Tshs. 50,000 per night
ROOMS WITH AC
SINGLE ROOM ON BB Tshs. 30,000 per night
DOULBE ROOM ON BB Tshs. 35,000 per night
TRIPLE ROOM ON BB Tshs. 55,000 per night
HB SUPPLEMENT
ADULT ON HB Tshs. 15,000 per person
CHILD ON HB Tshs. 10,000 per child
FB SUPPLEMENT
ADULT ON FB Tshs. 20,000 per person
CHILD ON FB Tshs. 15,000 per child
Includes 1 soda, a glass of juice or bottle of water
during the meal.
TWO NIGHTS STAY – you get free tour to Jozani Forest where you can see Red Colobus Monkeys and etc.

BEACH PARTY ON 3RD APRIL 2010
ENTRANCE FEE: TSHS 5,000 FOR MEN (includes 1 drink)
LADIES FREE.

Enjoy with us UNFORGETTABLE HOLIDAY in an untouched nature far off the beaten track.
Contact: +255 0 777 422008 / 0 715 422009 / 0 769 662662