WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Sunday, May 23, 2010

MTOTO YATIMA AJARIBU KULIPUA UBALOZI WA MAREKANI DAR

MWANAFUNZI Nassib [16] anayekabiliwa na tuhuma za kutaka kujaribu kulipua ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam uchunguzi umebaini kuwa ni yatima anaishi na shangazi yake Kinondoni Moscow.
Habari hizo za uhakika kutoka ndani ya jeshi la polisi, zimebaini hilo na mwanafunzi huyo anaishi na shangazi yake aitwae Chiku Simba baada ya wazazi wake kufariki.

Imefahamika kuwa mtandao wa kigaidi wa Al Qaeda umekuwa ukitumia watoto yatima, watoto wa mitaani na wajane kuwatumia kufanya vitendo vya ugaidi.

Hata hivyo shangazi yake alishangaa kutokana na kitendo hicho na alisema ameshitushwa na taarifa alizozipata kutoka kwenye vyombo vya habari kwa kuwa mtoto wake huyo hakuwa na vitendo vya kihuni na vya ajabu na majirani walithibitisha kuwa mwanafunzi huyo alikuwa ni mkarimu na hakuwa mtu wa makundi na hana tabia ya kukaa vijiweni.

Hata hivyo kati ya wanafunzi nane waliokamatwa juzi na maafisa wa polisi waliounganishwa katika tuhuma hizo saba wameachiwa huru na mmoja ambaye ni Amani Thomas anaendelea kushikiliwa kwa kuwa yeye ndiye aliongozana na Nassib hadi katika jengo hilo la ubalozi .

No comments:

Post a Comment