WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Thursday, May 6, 2010

UTARATIBU MPYA WA KUOMBA VISA YA MAREKANI

UBALOZI wa Marekani nchini umetoa utaratibu wa maombi ya viza kwa kutumia fomu mpya za DS -160 kwa ajili ya maombi ya muda mfupi utakaoanza kutumika Mei 31, mwaka huu.
Taarifa ya balozi hiyo iliyotolewa kwenye vyombo vya habari, ilieleza kuwa waombaji wote wa viza za muda mfupi watatakiwa kujaza fomu za DS-160 zitakazopatikana kwa njia ya mtandao.

Ilisema waombaji wote wanashauriwa kuanza kutumia fomu hizo mpya bila kuchelewa ili waweze kupata viza zao.

Taarifa hiyo ilielezea kuwa Idara ya Uhamiaji na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, imeboresha fomu za DS-160 kwa waombaji wote wa viza za muda mfupi (NIV) ili kuleta mabadiliko katika fomu zinazopatikana kwenye mtandao (EVAF).

Taarifa hiyo ilisema kwua tofauti inayopatikana kwenye fomu za DS-160 ipo kwenye hatua ya kwanza ya maombi ambapo wanatakiwa kujaza kupitia mtandao.

Tovuti ambayo utaweza kupata fomu za DS-160 kwa maelezo ya hatua kwa hatua ni http://www.tanzania.usembassy.gov au wataweza kuwasiliana na Idara ya Uhamiaji kwa barua pepe: drsniv@state.gov ama kutembelea katika ofisi za balozi.

No comments:

Post a Comment