WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Friday, June 18, 2010

VIDEO - Wivu Wapelekea Amchome Moto Mpenzi Wake


Kutokana na wivu mwanamke mmoja nchini Marekani alimchoma moto mpenzi wake na kisha kujichoma moto na yeye mwenyewe na kutokana na moto huo nyumba ilishika moto na kupelekea vifo vya watu wengine watatu.
Agnes Bermudez, 50, anatuhumiwa kumuua mpenzi wake William Salazar, 32, katika tukio la kutisha lililotokea siku ya akina baba duniani mwaka 2008.

Agnes ambaye hivi sasa kesi yake inaendelea mahakamani, alimchoma moto mpenzi wake huyo na kisha yeye mwenyewe alijipiga kibiriti.

Agnes hakufariki kutokana na moto aliouanzisha lakini aliungua vibaya sura yake kiasi cha kumfanya asitambulike.

Sababu ya Agnes kumchoma moto mpenzi wake ni wivu wa kimapenzi. Agnes alimshutumu Salazar kuwa anatembea na mwanamke mwingine nje.

Video ya tukio hilo imetolewa mahakamani kama ushahidi wa tukio hilo la kusikitisha.

Video inamuonyesha Agnes na Salazar wakitoka nje ya nyumba yao wakikimbilia kwenye duka lililopo chini ya jengo lao.

Salazar anaonekana akikimbia kuingia ndani ya duka akitafuta maji wakati Agnes alilala chini mbele ya duka hilo huku akiungua na moto.

Wasamaria wema walifanikiwa kuwamwagia maji na kuokoa maisha yao hata hivyo Salazar alifariki siku nne baadae hospitalini.

Moto ulioanzishwa na Agnes ulishika pia nyumba zingine zilizopo kwenye jengo hilo na kupelekea vifo vya watu watatu.

Chini ni VIDEO ya tukio hilo iliyoonyeshwa mahakamani.

No comments:

Post a Comment