WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Tuesday, June 1, 2010

AMPENDA DADA YAKE, AKAAMUA KUMUONA

Mwanaume mmoja nchini Ireland amejikuta akimzalisha dada yake bila kutarajia baada ya kuangukia kwenye mapenzi bila kujua kuwa mwanamke huyo ni dada yake. Ameamua kufunga naye ndoa ili waweze kumtunza mtoto aliyezaa naye.
Mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la Mark wa nchini Ireland alijikuta akizaa na dada yake wa baba mmoja mama tofauti, baada ya kuanza naye uhusiano bila kufahamu kuwa ni dada yake.

Wazazi wa Mark waliachana wakati Mark akiwa mdogo sana ambapo kwa jinsi ndoa hiyo ilivyovunjika kwa mgogoro mkubwa mahakamani, Mark alipewa jina tofauti la baba na mahakama iliamuru mtoto huyo asiambiwe baba yake anaitwa nani.

Kasheshe liliibuka baada ya Mark kukutana na mwanamke disco katika mji tofauti na anaoishi. Mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Maura naye alienda kwenye disco hilo akitoka kwenye mji mwingine tofauti.

Mark alianza uhusiano wa kimapenzi na Maura wakati huo. Miaka miwili baadae Maura alipopata ujauzito ndipo wawili hao walipoamua kuishi pamoja.

Baada ya Maura kujifungua, Mark aliamua kumtambulisha Maura kwa mama yake na ndipo ukweli ulipofichuka.

Mama yake Mark alimuuliza Maura baba yake anaitwa nani, alipolitaja jina lake ndipo mama huyo alipomwambia Mark "Mwanangu huyo ni dada yako".

Matokeo ya vipimo vya DNA yaliyotolewa mwezi uliopita yalithibitisha kuwa Mark na Maura ni mtu na dada yake.

Hata baada kugundua kuwa uhusiano wao ni haramu, wawili hao wameamua kuuendeleza na wamepanga kuzaa watoto wengi zaidi.

"Najua watu watatufikiria vibaya, kama tusingekuwa na mtoto tungeweza kufikiria kusitisha uhusiano wetu lakini kwakuwa tuna mtoto mmoja, tutafunga ndoa tuzae watoto wengi zaidi", alisema Mark.

Mark na Maura wanatoa lawama zao kwa mfumo wa sheria ambao ulizuia Mark kumjua baba yake.

Wamepanga kumfungulia kesi ya fidia jaji aliyeamuru Mark asijulishwe baba yake.

No comments:

Post a Comment