WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, March 29, 2010

MADEREVA WA DALADALA DAR WATANGAZA MGOMO


MADEREVA na makondakta wa daladala wa jijini Dar es Salaam wametangaza mgomo wa kuacha huduma hiyo ambayo walidai utaanza leo.
Mgomo huo tarajio ulisambazwa kwa njia ya vipeperushi na baadhi ya madereva wa jijini humo na mgomo huo utahusisha njia zote za mkoa wa Dar es Salaam.

Sababu ya kuanzisha mgomo huo ulidaiwa na maderava hao kuwa ni maslahi duni kwa siku, na kubwa ni kero za barabarani zinazosababishwa na Kampuni ya Majembe na askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani (Trafiki) ambao wamekuwa wakiwasumbua kila siku kwa sababu ambazo hazina msingi.

Madai mengine ni kutaka kuwekewa mazingira bora ya kazi ikiwemo mishahara, na makato ya mishahara hiyo ipelekwe Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa lengo ya kuboresha kazi hiyo kama wafanyakazi wengine nchini.

No comments:

Post a Comment