WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, March 29, 2010

MWANAME MWENYE MATITI MAKUBWA DUNIANI TOKA CHINA



Guo Feng mwanaume mwenye matiti makubwa Monday, March 29, 2010 4:58 AM
Madaktari nchini China wanadai kumgundua mwanaume mwenye matiti makubwa kuliko wote duniani.
Madaktari nchini China wanadai kumgundua mwanaume mwenye matiti makubwa kuliko wote duniani baada ya mwanaume huyo kujitokeza kwenye kliniki moja mjini Beijing.

Daktari wa hospitali ya Jinan Chest Hospital, Dokta Zhang Lilan alisema "Huyu ni mwanaume kamili isipokuwa ana matiti kama mwanamke".

"Yeye ni mkulima na anasema kuwa anasumbuliwa na ukubwa wa matiti yake wakati anapofanya kazi zake za kilimo".

"Anasema pia matiti yake yamekuwa gumzo kijijini kwake ambapo watu wengi wamekuwa wakimtafuta ili kumuona na imekuwa kero kubwa sana kwake kiasi cha kumfanya awe anavaa makoti makubwa hata wakati wa joto kali ili kuyaficha matiti yake", alisema dokta Lilan.

Mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la Guo Feng mwenye umri wa miaka 53, alisema "Miaka 10 iliyopita matiti yangu yalianza kuwa makubwa lakini nilikuwa nikifikiria unene wangu ndio sababu .. lakini miaka michache iliyopita nimekuwa nikizunguka hospitali moja baada ya nyingine kutafuta tiba lakini hakuna mtu anayetaka kunisaidia".

"Nimetumia pesa nyingi sana kwenye vipimo hospitalini lakini hakuna jibu lolote la maana huku matiti yangu yakiendelea kuwa makubwa", alisema Guo Feng.

"Wakati mwingine huwa nafikiria madaktari hawataki kunisaidia", alilamika Guo Feng.

Dokta Lilan alisema kuwa Guo Feng ametishia kuyakata matiti yake yeye mwenyewe iwapo hakuna daktari atakayejitokeza kumpatia tiba.

Hata hivyo madaktari wamekataa kuchukua hatua yoyote mpaka watakapogundua sababu ya matiti yake kuwa na ukubwa huo usio wa kawaida.

"Katika miaka yangu 30 ya kufanya kazi ya udaktari sijawahi kukumbana na kitu kama hichi", alisema Dokta Lilan.

"Awali tulidhania amekula kitu chenye sumu lakini vipimo vya damu yake havijaonyesha kitu chochote. Tumemfanyia X-ray hana dalili ya kansa", aliongeza mmiliki wa hospitali hiyo.

No comments:

Post a Comment