WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Monday, March 22, 2010

MGOMO WA WAFANYA KAZI TANZANIA

SHIRIKISHO la Vyama vya wafanyakazi nchini {TUCTA] umetangaza mgomo utakaofanyika nchi nzima kuaninzia Mei 5, mwaka huu kupinga mambo mbalimbali serikalini. Nacho Chama cha Walimu Tanzania [CWT] umeunga mgomo huo na umesema utashiriki ipasavyo na wameheshimu kauli ya tucta kwa kuwa ina nguvu na wanakusudia kugoma hadi hapo haki zao zitakapotekelezwa ipasavyo.

Rais wa CWT, Gratian Mukoba amesema kwa sasa anatoa taarifa kwa walimu wote nchini na wanatakiwa wafahamu kuwa chama chao kimeitikia wito wa kushiriki kwenye mgomo wa kudai mambo mbalimbali ambayo serikali imeyadharau kwa muda mrefu.

Aliongeza kuwa viongozi wa vyama vyote wamekubaliana kuwatangazia wanachama wao kuhusu mgomo huo ili washirikiane kudai haki zao chini ya mwavuli wa Tucta.

Mgomo huo unakusudia madai ya mishahara duni isiyokidhi mahitaji, mafao duni ya wastaafu kutoka kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na ulipishwaji wa kodi kubwa kwenye mishahara midogo wanayopata wafanyakazi.

Tucta imedai kuwa siku ya kusherehekea sikukuu ya wafanyakazi Mei Mosi watajadili kindani jinsi ya kuanza kufanya mgomo huo kwa kuw wafanyakazi wote hukutana siku hiyo.

No comments:

Post a Comment