WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Thursday, April 22, 2010

DENI LA TANZANIA LAZIDI KUONGEZEKA


DENI la Taifa limeongezeka maradufu na kufikia shilingi trillion 7.6

Hayo yaliwekwa wazi na katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Ludovick Otouh, alipokuwa akiwajulisha waandishi wahabari.

Amesema deni la taifa limeongezeka kwa kasi kutoka kiasi cha sh trilioni 6.4 mwaka 2007/08 hadi kufikia shilingi trilioni 7.6 katikka mwaka wa fedha wa 2008/09
.
Amesema kuwa deni hilo limeongezeka kwa tofauti ya shilingi trillion 1.1 kutoka lile la mwaka wa fedha wa jana.

Amesema kutokana na hali hiyo, kuna umuhumu wa serikali kusimamia vizuri makusanyo na matumizi ya fedha zake.

Amesema deni hilo limeongezeka hivyo kutokana na serikali kujiingiza katika bajeti kubwa kuliko uwezo wenyewe.

Vilevile amesema serikali imeshindwa kudhibiti matumizi ya juu, kutokuwa makini na mikataba mbalimbali, pamoja na kuzamini mambo mbalimbali kinyume na uwezo halisi.


Hivyo amesema katika taarifa zilizowasilishwa na maofisa masuuli, zilieleza bayana kuwa wizara, idara, walaka na sekretarieti za mikoa hazikuzingatia kikamilifu sheria ya manunuzi ya umma namba 21 ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2005 ambapo jumla ya sh bilioni 12.8 zilionyesha kasoro mbalimbali za ukiukwaji wa taratibu za manunuzi.

Pia alisema katik ukusanyaji wa mapato matokeo ya ukaguzi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), unaonyesha kuwa misamaha mingi iliyotolewa kwa taasisi mbalimbali na watu binafsi yenye thamani ya sh bilioni 752.3 imerudisha nyuma mapato ya serikali.

No comments:

Post a Comment