WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Thursday, April 22, 2010

JESHI LA POLISI LACHAPISHA KITABU CHA MUONGONZO KWA WAPIGA KURA


JESHI la Polisi Nchini, limetoa kitabu maalum kinachofafanua na kumuongoza mwananchi mchakato mzima wa uchaguzi kwa lengo la kuwezesha uchaguzi, huo kufanyika kwa utulivu na amani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam , Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema alisema kitabu cha Haki na wajibu wa Mpigakura, kimebeba ujumbe mzito unaohusu kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.


Mwema alisema ni haki ya kila Mtanzania aliyetimiza vigezo wa kupiga kura kitabu hicho kitamuongoza katika kuhakikisha kuwa sheria za nchi hazikiukwi kabla na baada ya uchaguzi

Alisema kitabu hicho kinalenga kuufanya uchaguzi huo uwe wa haki katika kuchagua viongozi na kutekeleza wajibu wa usalama, amani na utulivu vinadumu katika jamii.

Alisema kitabu hicho kinaelezea umuhimu wa kujiandikisha kupiga kura, uteuzi wa wagombea katika vyama vya siasa, kampeni za wagombea na vyama vyao na matangazo yatakayowekwa na vyama vya siasa na wagombea.

Mambo mengine ni wajibu na umuhimu wa polisi katika mchakato wa uchaguzi, haki na wajibu wa mpigakura, siku ya uchaguzi, jinsi ya kupiga kura, kusubiri matokeo, kupokea matokeo na uvunjaji wa sheria wakati wa uchaguzi.


Pia alisema “askari polisi watakaovujisha siri za taarifa mbalimbali zinazohusu mitaa katika uchaguzi watachukuliwa hatua kali, pia na mwananchi yeyote atakayehatarisha hatari ama kugundulika kuvunja amani sheria itafata mkondo wake” alisema.

No comments:

Post a Comment