WAKAZI wawili wa Jiji la Dar es Salaam, wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na tuhuma za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu baada ya kudai wana uwezo wa kumfufua mtoto aliyekufa na kudai hakufa kihalali.
Watuhumiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jana, na kusomewa mashtaka na mwendesha mashtaka wa Polisi, Nassoro Sisiwaya mbele ya Hakimu Suzane Kihawa wa mahakama hiyo.
Sisiwaya alidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja walijipatia fedha taslimu za kitanzania Shilingi milion 3.6 kutoka kwa Amina Juma kwa makubaliano kwamba wana uwezo wa kumfufulia mtoto aliyekufa wa mlalamikaji huyo.
Alidai kuwa washtakiwa hao walitenda kosa hilo, Mei 5 mwaka jana katika eneo la Kimara Baruti na kwamba walidai wana uwezo wa nguvu za kichawi za kuweza kumfufua marehemu huyo na kumrudisha akiwa hai.
Washtakiwa hao ni Shabani Juma (46), mkazi wa Tandale kwa Tumbo ambaye ni mganga wa jadi na Godfrey Zakaria (26) mkazi wa Tandale fundi wa umeme wa magari wote walimuahidi mama huyo kuwa mtoto huyo angefufuka kwa kuwa hakufa kihalali.
Ilidaiwa upelelezi wa shauri hilo umeisha kamilika na kesi itaanza kusikilizwa Mei 17 mwaka huu.
Washtakiwa wako nje kwa dhamana.
Wednesday, April 28, 2010
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment