WELCOME TO TANZAMERICA'S WORLD

Tanzamerica
Is a social network page that updates you with current news from Tanzania , America and around the world. Also, gives you the opportunity to link up your business or ministry between Tanzania and America .We are also dealing with Entertainments (music,movie and art) news, and sports between the two country.
For more info on how to advertise your business, ministry, career and news
Contact us:
+1360 561 6629
Patrick.
tanzamerica@gmail.com
info@patricknworld.com
http://www.tanzamerica.blogspot.com
Detailed Info

http://www.celebafrica.blogspot.com
http://www.patricknworld.blogspot.com
http://www.reverbnation.com/patricknewman

Wednesday, April 28, 2010

NVUA KUBWA YALETA BALAA DAR


JANA jiji la Dar es salaam lilitawaliwa na shida na mapungungufu makubwa katika huduma mbalimbali kutokana na mvua kubwa iliyonyesha siku nzima hali iliyofanya wakazi wa jiji kuteseka kutokana na hali hiyo.
Mbali na kuwa na dmapungufu katika huduma nyingine tofautitofauti shida kubwa zaidi ilikuwa ni upande wa usafiri ambao ulikuwa haupatikani kutokana na mvua hiyo.


NIFAHAMISHE ilishuhudia makundi ya watu yakihaha huku na huku, na yakipita barabarani mithili ya maandamano yakitembea kwa miguuu kurudi majumbani mwao kwa kukoseskana kwea huduma hiyo.


Hali hiyo ilidumu siku nzima katika kila kituo cha mabasi jijini ambapo mabasi yalikuwa hayafiki mjini na wakazi hao kulazimika kurudi kwa miguu majumbani mwao.


Jopo la waandishsi wa nifahamishe nao dhahama hiyo iliwakumba kwa kile kilichowakuta wamefika kituoni Posta majira ya saa 11 ya jioni na hadi ilipofika majira ya saa moja kasorobo hawajapata usafiri na kulazimika watembee kwa miguu kuhamia katika kituo cha nyuma cha Akiba na hali ilikuwa hivyohivyo.

Hali ilivyozidi kuwa tata zaidi waliamua warudi nyuma na kuelekea kituo cha fire ili waweze kupata usafiri na wageuze na mabasi lakini hali hiyo walidumu nayo kwa takribani dakika 45 kituoni hapo bila kuwa na dalili yoyote ya kupata usafiri.

Hiyo ndiyo hali iliyokuwa jana katika jiji la Dar es Salaam kwa wakazi wengi waishio humo wakionekana kurudi kwa miguu kutokana na adha iliyokuwepo

No comments:

Post a Comment